< I Samuela 31 >

1 A Filistynowie zwiedli bitwę z Izraelem; i uciekli mężowie Izraelscy przed Filistynami, a polegli zranieni na górze Gielboe.
Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli. Waisraeli wakakimbia mbele ya Wafilisti na wakaanguka chini wakafa katika mlima wa Gilboa.
2 I gonili Filistynowie Saula i syny jego, i zabili Filistynowie Jonatana, i Abinadaba, i Melchisuego, syny Saulowe.
Wafilisti wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu. Wakawaua wanawe Yonathani, Abinadabu, and Malkishua.
3 A gdy się wzmagała bitwa przeciwko Saulowi, trafili nań strzelcy, mężowie strzelający z łuku, i zraniony jest bardzo od strzelców.
Vita vikamwelemea Sauli, na wapiga upinde wakampata. Akapata maumivu makali kwa sababu yao.
4 I rzekł Saul do wyrostka swego, który nosił broń jego: Dobądź miecza twego, a przebij mię nim, by snać nie przyszli ci nieobrzezańcy, i nie przebili mię, a nie czynili igrzyska ze mnie. Ale nie chciał wyrostek jego, bo się bardzo bał. Przetoż Saul porwał miecz i upadł nań.
Kisha Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Chomoa upanga wako unichome nao. Vinginevyo, hawa wasiotahiriwa watakuja na kuninyanyasa.” Lakini mbeba silaha wake hakukubali, kwa kuwa aliogopa sana. Hivyo Sauli alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 A widząc wyrostek jego, iż umarł Saul, padł i on na miecz swój, i umarł z nim.
Yule mbeba silaha akaona kwamba Sauli amekufa, yeye naye vivyo hivyo akauangukia upanga wake akafa pamoja naye.
6 Umarł tedy Saul, i trzej synowie jego, i wyrostek jego, co za nim broń nosił, i wszyscy mężowie jego dnia onego wespół.
Kwa hiyo Sauli alikufa, wanawe watatu, na mbeba silaha wake - watu hawa wote walikufa pamoja siku iyo hiyo.
7 Co gdy ujrzeli mężowie Izraelscy, którzy za doliną, i za Jordanem mieszkali, iż uciekali mężowie Izraelscy, a iż umarł Saul, i synowie jego, odbieżawszy miast, pouciekali też, a przyszedłszy Filistynowie mieszkali w nich.
Watu wa Israeli waliokuwa upande mwingine wa bonde, na hao waliokuwa ng'ambo ya Yordani, walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliiacha miji yao na kukimbia, nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 A nazajutrz przyszli Filistynowie, aby odzierali pobite; i znaleźli Saula, i trzech synów jego leżących na górze Gielboe.
IKawa katika siku iliyofuata, Wafilisti wakafika kuchukua nyara za waliokufa, ndipo wakamuona Sauli na wanawe watatu wameanguka juu ya mlima wa Gilboa.
9 A uciąwszy głowę jego, zdarli z niego zbroję jego, i posłali po ziemi Filistyńskiej wszędzie, aby to opowiadano w kościele bałwanów ich, i między ludem.
Nao wakakata kichwa chake na kuondoa silaha zake, na wakawatuma wajumbe kwenda pande zote katika nchi ya Wafilisti kutangaza habari hizo katika mahekalu yao ya sanamu na kwa watu.
10 I położyli zbroję jego w kościele Astarot; ale ciało jego przybili na murze Betsan.
Wakaziweka silaha zake katika hekalu la Ashtorethi, nao wakakitundika kiwiliwili chake kwenye ukuta wa mji wa Bethi Shani.
11 Tedy usłyszawszy o tem obywatele Jabes Galaad, co uczynili Filistynowie Saulowi;
Na wenyeji wa Yabeshi Gileadi waliposikia kile Wafilisti walichomfanyia Sauli,
12 Wstali wszyscy mężowie mocni, i szli przez onę całą noc, i wzięli ciało Saulowe, i ciała synów jego z muru Betsan, a przyszedłszy do Jabes spalili je tam.
wapiganaji wote wakainuka na kwenda usiku wote na wakauondoa mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Bethi Shani. Nao wakaenda Yabeshi na wakaichoma moto hiyo miili huko.
13 A wziąwszy kości ich, pogrzebli je pod drzewem w Jabes, i pościli siedm dni.
Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, na wakafunga siku saba.

< I Samuela 31 >