< I Kronik 23 >

1 A tak Dawid będąc stary i pełen dni, postanowił królem Salomona, syna swego nad Izraelem.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 I zgromadził wszystkich książąt Izraelskich, i kapłanów, i Lewitów;
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 A policzono Lewitów od trzydziestu lat i wyżej; i był poczet ich według głów ich osób trzydzieści i ośm tysięcy.
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 Z których postanowiono na posługę domu Pańskiego dwadzieścia i cztery tysiące, a przełożonych i sędziów sześć tysięcy.
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 Nadto cztery tysiące odźwiernych, i cztery tysiące chwalących Pana na instrumentach, których nasprawiał Dawid ku chwaleniu Boga.
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 I rozdzielił ich Dawid na pewne hufy według synów Lewiego, to jest, Giersona, Kaata, i Merarego.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Z Giersona byli Laadam, i Semej.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Synowie Laadanowi: przedniejszy Jachijel, i Zetam, i Joel, ci trzej.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Synowie Semejowi: Salomit, i Hazyjel, i Haran, ci trzej. Cić byli przedniejsi domów ojcowskich z Laadana.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 A synowie Semejowi: Jachat, Zyna, i Jehus, i Baryjasz; cić synowie Semejowi czterej.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 A Jachat był pierwszym, a Zyza wtóry; ale Jehus i Baryjasz nie mieli wiele synów; przetoż byli w domu ojcowskim policzeni za jednę familiję.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Synowie Kaatowi: Amram, Izaar, Hebron, i Husyjel, czterej.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Synowie Amramowi: Aaron i Mojżesz. Lecz Aaron był odłączony, aby służył w świątnicy najświętszej, sam i synowie jego aż na wieki, i aby kadzili przed Panem, a służyli mu, i błogosławili w imieniu jego aż na wieki.
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 Ale synowie Mojżesza, męża Bożego, policzeni są w pokoleniu Lewiego.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Synowie Mojżeszowi: Gierson i Eliezer.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Synowie Giersonowi: Sebujel pierwszy.
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 A synowie Eliezerowi byli Rechabijasz pierwszy. I nie miał Eliezer synów innych; ale synowie Rechabijaszowi rozmnożyli się bardzo.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 Synowie Izaarowi: Salomit pierwszy.
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Synowie Hebronowi: Jeryjasz pierwszy, Amaryjasz wtóry, Jehazyjel trzeci, a Jekmaan czwarty.
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Synowie Husyjelowi: Micha pierwszy, a Jesyjasz wtóry.
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Synowie Merarego: Mahelin i Musy; a synowie Mahelego: Eleazar i Cys.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 I umarł Eleazar, a nie miał synów, tylko córki, które pojmowali synowie Cysowi, bracia ich.
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Synowie Musy: Maheli, i Eder, i Jerymot, trzej.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Cić są synowie Lewiego według domów ojców swych, przedniejsi domów ojcowskich, którzy policzeni byli według pocztu imion i osób swych z osobna, którzy odprawowali prace usługiwania w domu Pańskim od dwudziestu lat i wyżej.
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 Albowiem rzekł Dawid: Dał odpocznienie Pan, Bóg Izraelski, ludowi swemu, i będzie mieszkał w Jeruzalemie aż na wieki.
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 Do tego i Lewitowie nie będą więcej nosić przybytku i wszystkiego naczynia jego ku posługiwaniu jego;
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 Ale według postanowienia Dawidowego ostatniego, byli policzeni synowie Lewiego od dwudziestu lat i wyżej;
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Aby zostawali pod ręką synów Aaronowych ku usłudze domu Pańskiego w przysionkach i w gmachach, i ku oczyszczaniu wszelkich rzeczy poświęconych, i ku pracy około usługi domu Bożego;
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 I około chleba pokładnego, i około mąki na ofiarę, i około placków niekwaszonych, i około panewek, i około rzeczy smażonych, i około wszelkiej miary i odmierzania;
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 A iżby stali na każdy poranek ku wysławianiu, i ku chwaleniu Pana, także i w wieczór;
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 Nadto, przy każdem ofiarowaniu całopalenia Panu w sabaty, na nowiu miesiąca, i w uroczyste święta, według liczby i porządku ich ustawicznie przed Panem;
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 A tak aby pilnowali straży namiotu zgromadzenia, i straży świątnicy, i straży synów Aaronowych, braci swych, w usłudze domu Pańskiego.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< I Kronik 23 >