< Men Epijuj 1 >

1 PAULUJ wanporon en Iejuj Krijtuj amen pan kupur en Kot on me jaraui o lelapok kan ren Krijtuj Iejuj me mi Epijuj.
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Mak o popol jan ren Kot Jam atail o atail Kaun Iejuj Krijtuj en mi re omail!
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Meid iajanai Kot o Jam en atail Kaun Iejuj Krijtuj, me kapaia kin kitail lar jon en pai nenin karoj jan nanlan ren Krijtuj.
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 A kotin pil kitail dar re a, mon jappa jaikenta pajondier, pwe kitail en jaraui o minla mo a ni limpok.
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 Me pil kileledier, me kitail, en wiala japwilim a jeri ki Iejuj Krijtuj, duen a kotin kupura mauki.
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 Pwen kalinanada a mak lapalap, me a kotin make kin kitail ren Kompoke pa a,
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 Me kotin dore kin kitail la nta o lapwadan dip akan ki a mak lapalap.
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 Me a kotiki on kitail ni jon en lolekon o koiok karoj,
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 Ni a kotin diarok on kitail er me rir en kupur a duen a kotin kupuramauki o duen a kileledier ren pein i.
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 Pwen pwaida anjau lao leler en wijik penan tapwi ta ieu meakaroj, ren Krijtuj, men nanlan kan o men jappa kan on pein i.
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 Me pil kare on kitail jojo eu, kitail me kileledier duen kupur en i, me kin wiada meakan karoj, duen a kotin kupura,
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 Pwe kitail en wiala men kalinanada i, kitail, me kaporoporeki Krijtuj,
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 Me komail pil kaporoporeki murin omail roner maj an en melel o ronamau en kamaur; me pil kilele komail kidier Nen jaraui en inau, ni omail pojonlar.
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 lei men kamelele en atail jojo, lao lel anjau en atail konodi maur joutuk, pwen wiala japwilim en Kot o men kapina a linan.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 Ari, i lao ronadar duen omail pojon Kaun Iejuj o duen omail limpok on jaraui kan karoj,
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 I jota kin dukedi jan ai danke pweki komail, o i kin tamatamanda komail ni ai kapakap akan;
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 Pwe Kot en atail Kaun Iejuj Krijtuj, Jam en linan, en kotiki on komail nen en erpit o kaudial, pwen ajada i,
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 O kotin kamaraini maj en monion omail, pwe komail en kak dedeki kaporopor en omail paeker, o linan laud en jojo, me onoper on jaraui kan,
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 O a manaman kaualap on kitail, me pojonlar, duen a dodok manaman,
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 Me a kotin kajanjaledar ren Krijtuj ni a kotin kaiajada i jan ren me melar akan, ap kajapwiladan pali maun nanlan,
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 Ilela jan meakan karoj, o manaman karoj, o kelail o men poa kan o mar karoj, kaidin ni muei wet eta, pwe pil ni muei kokodo. (aiōn g165)
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
22 O a kotiki on meakaroj pan aluwilu a kan, o kotin kajapwiladan tapwin meakaroj ren momodijou,
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 lei war a, iei kadir pan me kadirela meakaroj.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.

< Men Epijuj 1 >