< Timoteuj II 2 >

1 ARI nai jeri keleki mak o, me mi ren Krijtuj Iejuj.
Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
2 O me koe roner jan ia impan jaunkadede toto, koe en ujai on aramaj lelapok kan, me koiok on padaki me tei kan.
Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
3 Koe ian ia kamekam duen jaunpei en Krijtuj Iejuj mau amen.
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
4 Jaunpei amen jota kin kadoki pein kan a mana, pwen kon on me ale i.
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
5 O ma amen pan weir, a jota pan ale katin, ma a jota weir mau.
Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
6 A jaumat amen, me kin japajap en tunole maj wa kan.
Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
7 Madamadaue duen me i inda, pwe Kaun o pan kotin kalolekon kin uk ni meakaroj.
Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
8 Tamataman Iejuj Krijtuj, me aijada jan ren me melar akan, kadaudok en Dawid duen ai ronamau,
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
9 Me i kamekameki o jalikidi dueta me jued amen, a majan en Kot me jo jalidier.
ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
10 Mepukat karoj i kin kamekameki me piladar akan, pwe ren pil konodi maur joutuk ren Krijtuj Iejuj ianaki a linan joutuk. (aiōnios g166)
Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
11 Meid melel, ma kitail ian matala, kitail pil pan ian ieiajata;
Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12 Ma kitail dadaurata, kitail pan ian kaunda; ma kitail ponjaja, a pil pan ponjaja kitail;
Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
13 Ma kitail jota pan dadaurata, a pn kotin melel weita, pwe a jo kak kalikame pein i.
Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
14 Kataman kin irail mepukat, kadede on irail mon Kaun o, ren der akamai ki jip en lokaia kan, me jota pan katepai on meakot, pwe a pan kajapune ir ala, me karon akan.
Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
15 Nantion konekonela ren Kot dueta toun dodok amen, me jo karepen namenokala mia, me kin padak weita pun majan melel.
Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
16 A koe en kan poupou mal akan, pwe ar japun pan lapalapala.
Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
17 Arail padak me pan paraparada due kinj. Kijan irail Imenauj o Piletuj,
Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
18 Me pirok jan melel ni a inda me dene mauredan aramaj wiauier, rap kawela pojon en akai.
ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
19 A pajon en Kot pan duedueta, a iet kilel: Kaun o kotin mani japwilim a kan, o: Karoj, me aja mar en Kaun o, en muei jan me japun.
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
20 Nan im lapalap kaidin dal kold o jilper eta me mia, pwe pil dal tuka o dal pwel, akai men kalinan, o akai kaidin men kalinan.
Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
21 A ma amen pan muei jan jon en aramaj due met, a pan rajon dal men kalinan me kajarauiala, o katepa on Kaun o mau on jon en wiawia mau karoj.
Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
22 Tan wei jan inon jued en manakap, ap tan won pun, o pojon o limpok, o popol ianaki karoj, me kin kapakapaki on Kaun o jan nan monion ar makelekel;
Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
23 A padak mal o likam kan kan, pwe koe aja, me re pan naitikada akamai.
Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
24 Ladu en Kaun men endor akamai, a en kadek on karoj, o koiok on padak o kanonama on me jued akan.
Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
25 O opampap ni a kapun on me katiwo kan, pwe ele Kot pan kotin jauaja ir, pwe ren wukilan lolekon en melel.
Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
26 O ren pil piti jan ni injar en tewil, me a injara kin ir di on injen a.
ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.

< Timoteuj II 2 >