< Lukas 19 >

1 I ARI kotilong ong nan kanim Ieriko, ap kotin daulula.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 A kilang, ol kapwapwa men mia, ad a Sakäus, me saumas en saunopwei kan.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 A men kilang Iesus, pwen asa, is i, ap sota kak, pweki pokon o, o a sakakair.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 I ari tiong mo’rail, dauda nin tuka pot, pwen kak kilang i, pwe a pan kotin daulul wasa o.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 A lao lel wasa o Iesus ap kotin masanda diar i, masani ong i: Sakäus, madang daudi, pwe I pan pedelong ong nan im om ran wet.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 I ari madang daudi kasamo i pereperen.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Irail lao kilanger met, karos ap lipanedeki inda: A pedelonger, pwen kairu ren ol dipan amen.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 A Sakäus potodo potoan ong Kaun o: Maing re kotin mangi, apali en ai kapwa i pan kisakisaki me samama kan, o ma i kotaue amen, i kin kasapal wong i pan pa pak laude sang.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Iesus kotin masani ong i: Maur me pwara dong nan im wet ran wet, pwe a pil nain Apraam amen.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 Pwe Nain aramas pwara don rapaki o kamaureda me salongalar.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 A ni ar rongadar mepukat, a pil kotin masani karaseras eu, aki koren iong Ierusalem, o re kiki ong, me wein Kot pan madang sansaleda.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 A kotin masani: Ol lapalap amen kolang sap doo eu, pwen nine mar a, ap pan puredo.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 I me eker pena na ladu ek, o ki ong irail paun eisok, indang irail: Komail dodokki, i lao puredo.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 A na aramas akan kailongki i, kadarala mur i kaireki lang i: Se sota mauki, ol men et en kaun kit.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 Kadekadeo a lao puredo, murin a aleer wei o, ap ilakelang ladu kan, me a ki ong na moni, pwen asa duen en amen amen ar kalaudelar na moni.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Men mas ap pwarado indada: Maing, omui paun kareda paun eisok.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 A indang i: Meid pai ladu mau koe, aki om apapwali mau me tikitik, koe pan id kaunda kanim eisok.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 O kariamen ap pwarado indada: Maing, omui paun me kareda paun limau.
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 A pil indang i: Koe pan kaunda kanim limau.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 O pil amen pwarado indada: Maing, mangi, ietet sapwilim omui paun, me i nekidala nan lim en pudo.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 Pwe i masak komui, pwe ol petik amen komui. Komui kin aleda, me kaidin komui kidier, o dolung sang, me kaidin komui padukedier.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 A indang i: Sang nan au om i pan kadeik kin uk ada ladu sued koe. Koe asaer, me ol petik amen ngai, me kin ale, me kaidin ngai kidier o dolung sang, me kaidin ngai padukidier.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Menda koe sota wala nai moni wasan kanaitik, o i lao puredo, i pan ale me udan ai iangaki moni naitik.
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 A indai ong irail me u impa: Ale sang i paun o, ki ong ren me a paun eisok!
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 Irail indai ong i: Maing, nan a nainekier paun eisok.
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 Pwe I indai ong komail, meamen, me a mia, ekis pan ko ong, a me sota a mia, nan a pwitikatik pil pan katia sang.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 A ir, ai imwintiti, me kang, i en kakaun ir, wa ir do, o kame ir ala mo i!
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 A lao kotin kaimwisokala a masan pukat, ap kotiwei kotidala Ierusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 Kadekadeo a lao koti dong Petpake o Petanien impan dol me ad a Oliwe, ap kotin poronela sapwilim a tounpadak riamen,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 Masani: Koma ko ong nan kanim monen, koma lao pedelong, koma pan diarada esel pul amen salidi, me aramas amen saik mondi poa. Lapwada i, ap karedo!
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 A ma meamen pan idok re oma: Da me koma lapwa kida i? Koma ap pan inda: Kaun o men dake.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 A ira me pakadara wei, ap kola o diarada, duen a kotin masani ong ira.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 A ni ara lawada esel pul o, ol oko, me naineki, ap indang ira: Da me koma lawa kida esel pul en?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 Ira ap indada: Kaun o men dake.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 Ira ari wado ren Iesus, ap irepadi pon esel pul arail likau kan ap potoan dang Iesus poa.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 Ni a kotikot kokowei, irail ap irepakidi arail likau kan nani al.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 A lao kotin korendor kotidila dol Oliwe tounpadak kan karos ap wiaki eu ngil laudeda kapinga Kot, pweki manaman akan karos, me re kilanger,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 Indada: Kapinga ong Nanmarki, me kotido ni mar en Kaun! Nanlang en popol o lingan wasa ileile!
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 A Parisär kai kisan pokon o indai ong i: Saunpadak, kotin kidaue sapwilim omui tounpadak kan.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 I ari kotin sapeng masani ong irail: I indai ong komail, ma mepukat pan nenenla, takai pan id kadededa.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 A lao kotin korendor, ap masani kanim o, ap tontonireki,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 Masani: O i men, koe en dedeki om ran mau wet, me pan kare ong uk popol: Ari, a rir sanger mon mas om.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Pwe ran apwal ko pan lel ong uk, me om imwintiti pan kele kin uk pena o it pena sang ni pali karos;
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 O irail pan kase uk ala iangaki noum seri kan, o re pan karongk uk ala; sota eu takai pan mimieta pon eu, pweki om sota dedeki ansaun om kasosong.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 I ari kotilong ong nan im en kaudok, ap sikon sang me netinet lole,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 Masani ong ir: Nan a intingidier: Im ai im en kapakap, a komail wiaki deun lolap akan.
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 I ari kotin kaukawewe nan im en kaudok ran karos. A samero lapalap, o saunkawewe, o me lapalap akan ren aramas raparapaki, en kamatala i.
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 A re sota kak diar, me ren wiada, pwe aramas karos apwali i kaualap o men rong i.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Lukas 19 >