< مکاشفهٔ یوحنا 20 >

و دیدم فرشته‌ای را که از آسمان نازل می شود و کلید هاویه را دارد و زنجیری بزرگ بر دست وی است. (Abyssos g12) ۱ 1
Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos g12)
و اژدها یعنی مار قدیم را که ابلیس و شیطان می‌باشد، گرفتار کرده، او راتا مدت هزار سال در بند نهاد. ۲ 2
Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ndiye ibilisi au Shetani, naye akamfunga kwa muda wa miaka 1,000.
و او را به هاویه انداخت و در را بر او بسته، مهر کرد تا امت‌ها رادیگر گمراه نکند تا مدت هزار سال به انجام رسد؛ و بعد از آن می‌باید اندکی خلاصی یابد. (Abyssos g12) ۳ 3
Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia lakiri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa mpaka hiyo miaka 1,000 itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. (Abyssos g12)
و تختها دیدم و بر آنها نشستند و به ایشان حکومت داده شد و دیدم نفوس آنانی را که بجهت شهادت عیسی و کلام خدا سر بریده شدند و آنانی را که وحش و صورتش را پرستش نکردند و نشان او را بر پیشانی و دست خود نپذیرفتند که زنده شدند و با مسیح هزار سال سلطنت کردند. ۴ 4
Kisha nikaona viti vya enzi vilivyokuwa vimekaliwa na hao waliopewa mamlaka ya kuhukumu, na nikaona roho za wale waliokatwa vichwa kwa sababu ya ushuhuda wa Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawakuwa wamemsujudu huyo mnyama wala sanamu yake wala hawakupokea ile chapa yake kwenye vipaji vya nyuso zao au kwenye mikono yao. Wakawa hai na kutawala pamoja na Kristo miaka 1,000.
و سایر مردگان زنده نشدند تاهزار سال به اتمام رسید. این است قیامت اول. ۵ 5
(Wafu waliosalia hawakufufuka mpaka ilipotimia hiyo miaka 1,000.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
خوشحال و مقدس است کسی‌که از قیامت اول قسمتی دارد. بر اینها موت ثانی تسلط ندارد بلکه کاهنان خدا و مسیح خواهند بود و هزار سال با اوسلطنت خواهند کرد. ۶ 6
Waliobarikiwa na walio watakatifu ni wale walio na sehemu katika ufufuo wa kwanza. Hao mauti ya pili haina nguvu juu yao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka 1,000.
و چون هزار سال به انجام رسد، شیطان اززندان خود خلاصی خواهد یافت ۷ 7
Hiyo miaka 1,000 itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka kifungoni mwake,
تا بیرون رودو امت هایی را که در چهار زاویه جهانند، یعنی جوج و ماجوج را گمراه کند و ایشان را بجهت جنگ فراهم آورد که عدد ایشان چون ریگ دریاست. ۸ 8
naye atatoka ili kuyadanganya mataifa yaliyopo katika pembe nne za dunia, yaani, Gogu na Magogu apate kuwakusanya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga ulioko pwani.
و بر عرصه جهان برآمده، لشکرگاه مقدسین و شهر محبوب را محاصره کردند. پس آتش از جانب خدا از آسمان فرو ریخته، ایشان رابلعید. ۹ 9
Nao walitembea katika eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya watakatifu na ule mji unaopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.
و ابلیس که ایشان را گمراه می‌کند، به دریاچه آتش و کبریت انداخته شد، جایی که وحش و نبی کاذب هستند؛ و ایشان تا ابدالابادشبانه‌روز عذاب خواهند کشید. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442) ۱۰ 10
Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442)
و دیدم تختی بزرگ سفید و کسی را بر آن نشسته که از روی وی آسمان و زمین گریخت وبرای آنها جایی یافت نشد. ۱۱ 11
Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha enzi pamoja na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikaukimbia uso wake wala mahali pao hapakuonekana.
و مردگان را خرد وبزرگ دیدم که پیش تخت ایستاده بودند؛ و دفترهارا گشودند. پس دفتری دیگر گشوده شد که دفترحیات‌است و بر مردگان داوری شد، بحسب اعمال ایشان از آنچه در دفترها مکتوب است. ۱۲ 12
Nami nikawaona wafu wakubwa na wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni kitabu cha uzima. Hao wafu wakahukumiwa sawasawa na matendo yao kama yalivyoandikwa ndani ya hivyo vitabu.
و دریا مردگانی را که در آن بودند باز داد؛ و موت و عالم اموات مردگانی را که در آنها بودندباز دادند؛ و هر یکی بحسب اعمالش حکم یافت. (Hadēs g86) ۱۳ 13
Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. (Hadēs g86)
و موت و عالم اموات به دریاچه آتش انداخته شد. این است موت ثانی، یعنی دریاچه آتش. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442) ۱۴ 14
Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442)
و هر‌که در دفتر حیات مکتوب یافت نشد، به دریاچه آتش افکنده گردید. (Limnē Pyr g3041 g4442) ۱۵ 15
Iwapo mtu jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. (Limnē Pyr g3041 g4442)

< مکاشفهٔ یوحنا 20 >