< مکاشفهٔ یوحنا 2 >

«به فرشته کلیسای در افسس بنویس که این را می‌گوید او که هفت ستاره را بدست راست خود دارد و در میان هفت چراغدان طلامی خرامد. ۱ 1
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
می‌دانم اعمال تو را و مشقت و صبرتو را و اینکه متحمل اشرار نمی توانی شد و آنانی را که خود را رسولان می‌خوانند و نیستندآزمودی و ایشان را دروغگو یافتی؛ ۲ 2
Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
و صبرداری و بخاطر اسم من تحمل کردی و خسته نگشتی. ۳ 3
Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
«لکن بحثی بر تو دارم که محبت نخستین خود را ترک کرده‌ای. ۴ 4
“Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
پس بخاطر آر که از کجاافتاده‌ای و توبه کن و اعمال نخست را بعمل آوروالا بزودی نزد تو می‌آیم و چراغدانت را از مکانش نقل می‌کنم اگر توبه نکنی. ۵ 5
Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
لکن این راداری که اعمال نقولاویان را دشمن داری، چنانکه من نیز از آنها نفرت دارم. ۶ 6
Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
«آنکه گوش دارد بشنود که روح به کلیساهاچه می‌گوید: هر‌که غالب آید، به او این را خواهم بخشید که از درخت حیاتی که در وسط فردوس خداست بخورد. ۷ 7
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
«و به فرشته کلیسای در اسمیرنا بنویس که این را می‌گوید آن اول و آخر که مرده شد و زنده گشت. ۸ 8
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
اعمال و تنگی و مفلسی تو را می‌دانم، لکن دولتمند هستی و کفر آنانی را که خود رایهود می‌گویند و نیستند بلکه از کنیسه شیطانند. ۹ 9
Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
از آن زحماتی که خواهی کشید مترس. اینک ابلیس بعضی از شما را در زندان خواهد انداخت تا تجربه کرده شوید و مدت ده روز زحمت خواهید کشید. لکن تا به مرگ امین باش تا تاج حیات را به تو دهم. ۱۰ 10
Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
آنکه گوش دارد بشنود که روح به کلیساها چه می‌گوید: هر‌که غالب آید ازموت ثانی ضرر نخواهد یافت. ۱۱ 11
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
«و به فرشته کلیسای در پرغامس بنویس این را می‌گوید او که شمشیر دودمه تیز را دارد. ۱۲ 12
“Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
اعمال و مسکن تو را می‌دانم که تخت شیطان در آنجاست و اسم مرا محکم داری و ایمان مراانکار ننمودی، نه هم در ایامی که انطیپاس شهیدامین من در میان شما در جایی که شیطان ساکن است کشته شد. ۱۳ 13
Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
لکن بحث کمی بر تو دارم که در آنجا اشخاصی را داری که متمسکند به تعلیم بلعام که بالاق را آموخت که در راه بنی‌اسرائیل سنگی مصادم بیندازد تا قربانی های بتها رابخورند و زنا کنند. ۱۴ 14
“Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
و همچنین کسانی را داری که تعلیم نقولاویان را پذیرفته‌اند. ۱۵ 15
Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
پس توبه کن والا بزودی نزد تو می‌آیم و به شمشیر زبان خود باایشان جنگ خواهم کرد. ۱۶ 16
Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
آنکه گوش دارد، بشنود که روح به کلیساها چه می‌گوید: و آنکه غالب آید، از من مخفی به وی خواهم داد وسنگی سفید به او خواهم بخشید که بر آن سنگ اسمی جدید مرقوم است که احدی آن رانمی داند جز آنکه آن را یافته باشد. ۱۷ 17
“Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
«و به فرشته کلیسای در طیاتیرا بنویس این را می‌گوید پسر خدا که چشمان او چون شعله آتش و پایهای او چون برنج صیقلی است. ۱۸ 18
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
اعمال و محبت و خدمت و ایمان و صبر تو رامی دانم و اینکه اعمال آخر تو بیشتر از اول است. ۱۹ 19
Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
لکن بحثی بر تو دارم که آن زن ایزابل نامی راراه می‌دهی که خود را نبیه می‌گوید و بندگان مراتعلیم داده، اغوا می‌کند که مرتکب زنا و خوردن قربانی های بتها بشوند. ۲۰ 20
“Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
و به او مهلت دادم تاتوبه کند، اما نمی خواهد از زنای خود توبه کند. ۲۱ 21
Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
اینک او را بر بستری می‌اندازم و آنانی را که بااو زنا می‌کنند، به مصیبتی سخت مبتلا می‌گردانم اگر از اعمال خود توبه نکنند، ۲۲ 22
Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
و اولادش را به قتل خواهم رسانید. آنگاه همه کلیساها خواهنددانست که منم امتحان کننده جگرها و قلوب و هریکی از شما را برحسب اعمالش خواهم داد. ۲۳ 23
Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
لکن باقی ماندگان شما را که در طیاتیرا هستیدو این تعلیم را نپذیرفته‌اید و عمقهای شیطان راچنانکه می‌گویند نفهمیده‌اید، بار دیگری بر شمانمی گذارم، ۲۴ 24
Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
جز آنکه به آنچه دارید تا هنگام آمدن من تمسک جویید. ۲۵ 25
Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
و هر‌که غالب آید واعمال مرا تا انجام نگاه دارد، او را بر امت هاقدرت خواهم بخشید ۲۶ 26
“Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
تا ایشان را به عصای آهنین حکمرانی کند و مثل کوزه های کوزه‌گرخرد خواهند شد، چنانکه من نیز از پدر خودیافته‌ام. ۲۷ 27
“‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
و به او ستاره صبح را خواهم بخشید. ۲۸ 28
Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
آنکه گوش دارد بشنود که روح به کلیساها چه می‌گوید. ۲۹ 29
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.

< مکاشفهٔ یوحنا 2 >