< مزامیر 57 >

برای سالار مغنیان برلاتهلک. مکتوم داود وقتی که از حضور شاول به مغاره فرار کرد ای خدا بر من رحم فرما، بر من رحم فرما! زیرا جانم در تو پناه می‌برد، و درسایه بالهای تو پناه می‌برم تا این بلایا بگذرد. ۱ 1
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
نزدخدای تعالی آواز خواهم داد، نزد خدایی که همه‌چیز را برایم تمام می‌کند. ۲ 2
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
از آسمان فرستاده، مرا خواهد رهانید. زیرا تعاقب کننده سخت من ملامت می‌کند، سلاه. خدا رحمت و راستی خودرا خواهد فرستاد. ۳ 3
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
جان من در میان شیران است. در میان آتش افروزان می‌خوابم یعنی آدمیانی که دندانهایشان نیزه‌ها و تیرهاست. و زبان ایشان شمشیر برنده است. ۴ 4
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
‌ای خدا بر آسمانها متعال شو و جلال تو بر تمامی جهان. ۵ 5
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
دامی برای پایهایم مهیا ساختند و جانم خم گردید. چاهی پیش رویم کندند، و خود در میانش افتادند، سلاه. ۶ 6
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
دل من مستحکم است خدایا دل من مستحکم است. سرود خواهم خواند و ترنم خواهم نمود. ۷ 7
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
‌ای جلال من بیدار شو! ای بربط وعود بیدار شو! صبحگاهان من بیدار خواهم شد. ۸ 8
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
‌ای خداوند تو را در میان امت‌ها حمد خواهم گفت. تو را در میان قوم‌ها تسبیح خواهم خواند. ۹ 9
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
زیرا رحمت تو تا آسمانها عظیم است وراستی تو تا افلاک. ۱۰ 10
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
خدایا بر آسمانها متعال شو. و جلال تو بر تمامی جهان. ۱۱ 11
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< مزامیر 57 >