< مزامیر 36 >

برای سالار مغنیان. مزمور داود بنده خداوند معصیت شریر در اندرون دل من می گوید که ترس خدا در مد نظر اونیست. ۱ 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
زیرا خویشتن را در نظر خود تملق می‌گوید تا گناهش ظاهر نشود و مکروه نگردد. ۲ 2
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
سخنان زبانش شرارت و حیله است. ازدانشمندی و نیکوکاری دست برداشته است. ۳ 3
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
شرارت را بر بستر خود تفکر می‌کند. خود را به راه ناپسند قائم کرده، از بدی نفرت ندارد. ۴ 4
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
‌ای خداوند رحمت تو در آسمانها است وامانت تو تا افلاک. ۵ 5
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
عدالت تو مثل کوههای خداست و احکام تو لجه عظیم. ای خداوندانسان و بهایم را نجات می‌دهی. ۶ 6
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
‌ای خدارحمت تو چه ارجمند است. بنی آدم زیر سایه بالهای تو پناه می‌برند. ۷ 7
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
از چربی خانه تو شاداب می‌شوند. از نهر خوشیهای خود ایشان را می نوشانی. ۸ 8
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
زیرا که نزد تو چشمه حیات‌است ودر نور تو نور را خواهیم دید. ۹ 9
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
رحمت خود رابرای عارفان خود مستدام فرما و عدالت خود رابرای راست دلان. ۱۰ 10
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
پای تکبر بر من نیاید و دست شریران مرا گریزان نسازد. ۱۱ 11
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
در آنجا بدکرداران افتاده‌اند. ایشان انداخته شده‌اند و نمی توانندبرخاست. ۱۲ 12
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< مزامیر 36 >