< امثال 31 >
کلام لموئیل پادشاه، پیغامی که مادرش به او تعلیم داد. | ۱ 1 |
Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
چه گویمای پسر من، چه گویمای پسر رحم من! و چه گویمای پسر نذرهای من! | ۲ 2 |
“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
قوت خود را به زنان مده، و نه طریقهای خویش را به آنچه باعث هلاکت پادشاهان است. | ۳ 3 |
Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
پادشاهان را نمی شایدای لموئیل، پادشاهان را نمی شاید که شراب بنوشند، و نه امیران را که مسکرات را بخواهند. | ۴ 4 |
“Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
مبادا بنوشند و فرایض را فراموش کنند، وداوری جمیع ذلیلان را منحرف سازند. | ۵ 5 |
wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
مسکرات را به آنانی که مشرف به هلاکتندبده. و شراب را به تلخ جانان، | ۶ 6 |
Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
تا بنوشند و فقر خود را فراموش کنند، ومشقت خویش را دیگر بیاد نیاورند. | ۷ 7 |
Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
دهان خود را برای گنگان باز کن، و برای دادرسی جمیع بیچارگان. | ۸ 8 |
“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
دهان خود را باز کرده، به انصاف داوری نما، و فقیر و مسکین را دادرسی فرما. | ۹ 9 |
Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
زن صالحه را کیست که پیدا تواند کرد؟ قیمت او از لعلها گرانتر است. | ۱۰ 10 |
Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
دل شوهرش بر او اعتماد دارد، و محتاج منفعت نخواهد بود. | ۱۱ 11 |
Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
برایش تمامی روزهای عمر خود، خوبی خواهد کرد و نه بدی. | ۱۲ 12 |
Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
پشم و کتان را میجوید. و بهدستهای خودبا رغبت کار میکند. | ۱۳ 13 |
Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
او مثل کشتیهای تجار است، که خوراک خود را از دور میآورد. | ۱۴ 14 |
Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
وقتی که هنوز شب است برمی خیزد، و به اهل خانهاش خوراک و به کنیزانش حصه ایشان را می دهد. | ۱۵ 15 |
Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
درباره مزرعه فکر کرده، آن را میخرد، و ازکسب دستهای خود تاکستان غرس مینماید. | ۱۶ 16 |
Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
کمر خود را با قوت میبندد، و بازوهای خویش را قوی میسازد. | ۱۷ 17 |
Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
تجارت خود را میبیند که نیکو است، وچراغش در شب خاموش نمی شود. | ۱۸ 18 |
Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
دستهای خود را به دوک دراز میکند، وانگشتهایش چرخ را میگیرد. | ۱۹ 19 |
Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
کفهای خود را برای فقیران مبسوطمی سازد، و دستهای خویش را برای مسکینان دراز مینماید. | ۲۰ 20 |
Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
به جهت اهل خانهاش از برف نمی ترسد، زیرا که جمیع اهل خانه او به اطلس ملبس هستند. | ۲۱ 21 |
Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
برای خود اسبابهای زینت میسازد. لباسش از کتان نازک و ارغوان میباشد. | ۲۲ 22 |
Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
شوهرش در دربارها معروف میباشد، و در میان مشایخ ولایت مینشیند. | ۲۳ 23 |
Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
جامه های کتان ساخته آنها را میفروشد، وکمربندها به تاجران میدهد. | ۲۴ 24 |
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
قوت و عزت، لباس او است، و درباره وقت آینده میخندد. | ۲۵ 25 |
Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
دهان خود را به حکمت میگشاید، و تعلیم محبتآمیز بر زبان وی است. | ۲۶ 26 |
Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
به رفتار اهل خانه خود متوجه میشود، وخوراک کاهلی نمی خورد. | ۲۷ 27 |
Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
پسرانش برخاسته، او را خوشحال میگویند، و شوهرش نیز او را میستاید. | ۲۸ 28 |
Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
دختران بسیار اعمال صالحه نمودند، اما توبر جمیع ایشان برتری داری. | ۲۹ 29 |
“Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
جمال، فریبنده و زیبایی، باطل است، اما زنی که از خداوند میترسد ممدوح خواهدشد. | ۳۰ 30 |
Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
وی را از ثمره دستهایش بدهید و اعمالش او را نزد دروازهها بستاید. | ۳۱ 31 |
Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.