< امثال 25 >

اینها نیز از امثال سلیمان است که مردان حزقیا، پادشاه یهودا آنها را نقل نمودند. ۱ 1
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
مخفی داشتن امر جلال خدا است، و تفحص نمودن امر جلال پادشاهان است. ۲ 2
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
آسمان را در بلندیش و زمین را در عمقش، ودل پادشاهان را تفتیش نتوان نمود. ۳ 3
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
درد را از نقره دور کن، تا ظرفی برای زرگربیرون آید. ۴ 4
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
شریران را از حضور پادشاه دور کن، تاکرسی او در عدالت پایدار بماند. ۵ 5
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
در حضور پادشاه خویشتن را برمیفراز، و درجای بزرگان مایست، ۶ 6
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
زیرا بهتر است تو را گفته شود که اینجا بالابیا، از آنکه به حضور سروری که چشمانت او رادیده است تو را پایین برند. ۷ 7
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
برای نزاع به تعجیل بیرون مرو، مبادا درآخرش چون همسایه ات تو را خجل سازد، ندانی که چه باید کرد. ۸ 8
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
دعوی خود را با همسایه ات بکن، اما رازدیگری را فاش مساز، ۹ 9
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
مبادا هر‌که بشنود تو را ملامت کند، وبدنامی تو رفع نشود. ۱۰ 10
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
سخنی که در محلش گفته شود، مثل سیبهای طلا در مرصعکاری نقره است. ۱۱ 11
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
مودب حکیم برای گوش شنوا، مثل حلقه طلا و زیور زر خالص است. ۱۲ 12
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
رسول امین برای فرستندگان خود، چون خنکی یخ در موسم حصاد می‌باشد، زیرا که جان آقایان خود را تازه می‌کند. ۱۳ 13
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
کسی‌که از بخششهای فریبنده خود فخرمی کند، مثل ابرها و باد بی‌باران است. ۱۴ 14
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
با تحمل داور را به رای خود توان آورد، وزبان ملایم، استخوان را می‌شکند. ۱۵ 15
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
اگر عسل یافتی بقدر کفایت بخور، مبادا ازآن پر شده، قی کنی. ۱۶ 16
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
پای خود را از زیاد رفتن به خانه همسایه ات باز دار، مبادا از تو سیر شده، از تونفرت نماید. ۱۷ 17
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
کسی‌که درباره همسایه خود شهادت دروغ دهد، مثل تبرزین و شمشیر و تیر تیز است. ۱۸ 18
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
اعتماد بر خیانتکار در روز تنگی، مثل دندان کرم زده و پای مرتعش می‌باشد. ۱۹ 19
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
سراییدن سرودها برای دلتنگ، مثل کندن جامه در وقت سرما و ریختن سرکه بر شوره است. ۲۰ 20
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
اگر دشمن تو گرسنه باشد او را نان بخوران، و اگر تشنه باشد او را آب بنوشان، ۲۱ 21
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
زیرا اخگرها بر سرش خواهی انباشت، وخداوند تو را پاداش خواهد داد. ۲۲ 22
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
چنانکه باد شمال باران می‌آورد، همچنان زبان غیبتگو چهره را خشمناک می‌سازد. ۲۳ 23
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
ساکن بودن در گوشه پشت بام بهتر است ازبودن با زن جنگجو در خانه مشترک. ۲۴ 24
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
خبر خوش از ولایت دور، مثل آب سردبرای جان تشنه است. ۲۵ 25
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
مرد عادل که پیش شریر خم شود، مثل چشمه گل آلود و منبع فاسد است. ۲۶ 26
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
زیاد عسل خوردن خوب نیست، همچنان طلبیدن جلال خود جلال نیست. ۲۷ 27
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
کسی‌که بر روح خود تسلط ندارد، مثل شهر منهدم و بی‌حصار است. ۲۸ 28
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< امثال 25 >