< اعداد 8 >

و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۱ 1
Bwana akamwambia Mose,
«هارون را خطاب کرده، به وی بگو: هنگامی که چراغها را برافرازی، هفت چراغ پیش شمعدان روشنایی بدهد.» ۲ 2
“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
پس هارون چنین کرد، و چراغها را برافراشت تا پیش شمعدان روشنایی بدهد، چنانکه خداوند موسی را امرفرموده بود. ۳ 3
Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
و صنعت شمعدان این بود: ازچرخکاری طلا از ساق تا گلهایش چرخکاری بود، موافق نمونه‌ای که خداوند به موسی نشان داده بود، به همین طور شمعدان را ساخت. ۴ 4
Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۵ 5
Bwana akamwambia Mose:
«لاویان را از میان بنی‌اسرائیل گرفته، ایشان راتطهیر نما. ۶ 6
“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
و بجهت تطهیر ایشان، به ایشان چنین عمل نما، آن کفاره گناه را بر ایشان بپاش و بر تمام بدن خود استره بگذرانند، و رخت خود را شسته، خود را تطهیر نمایند. ۷ 7
Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
و گاوی جوان و هدیه آردی آن، یعنی آرد نرم مخلوط با روغن بگیرند، وگاو جوان دیگر بجهت قربانی گناه بگیر. ۸ 8
Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
ولاویان را پیش خیمه اجتماع نزدیک بیاور، وتمامی جماعت بنی‌اسرائیل را جمع کن. ۹ 9
Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
ولاویان را به حضور خداوند نزدیک بیاور، وبنی‌اسرائیل دستهای خود را بر لاویان بگذارند. ۱۰ 10
Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
و هارون لاویان را از جانب بنی‌اسرائیل به حضور خداوند هدیه بگذراند، تا خدمت خداوندرا بجا بیاورند. ۱۱ 11
Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
و لاویان دستهای خود را بر سرگاوان بنهند، و تو یکی را بجهت قربانی گناه ودیگری را بجهت قربانی سوختنی برای خداوندبگذران، تا بجهت لاویان کفاره شود. ۱۲ 12
“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
و لاویان را پیش هارون و پسرانش برپا بدار، و ایشان رابرای خداوند هدیه بگذران. ۱۳ 13
Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
و لاویان را از میان بنی‌اسرائیل جدا نما و لاویان از آن من خواهندبود. ۱۴ 14
Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
«و بعد از آن لاویان داخل شوند تا خدمت خیمه اجتماع را بجا آورند، و تو ایشان را تطهیرکرده، ایشان را هدیه بگذران. ۱۵ 15
“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
زیراکه ایشان ازمیان بنی‌اسرائیل به من بالکل داده شده‌اند، و به عوض هر گشاینده رحم، یعنی به عوض همه نخست زادگان بنی‌اسرائیل، ایشان را برای خودگرفته‌ام. ۱۶ 16
Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
زیرا که جمیع نخست زادگان بنی‌اسرائیل خواه از انسان و خواه از بهایم، از آن من‌اند، در روزی که جمیع نخست زادگان را درزمین مصر زدم، ایشان را برای خود تقدیس نمودم. ۱۷ 17
Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
پس لاویان را به عوض همه نخست زادگان بنی‌اسرائیل گرفتم. ۱۸ 18
Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
و لاویان رااز میان بنی‌اسرائیل به هارون و پسرانش پیشکش دادم تا خدمت بنی‌اسرائیل را در خیمه اجتماع بجا آورند، و بجهت بنی‌اسرائیل کفاره نمایند، وچون بنی‌اسرائیل به قدس نزدیک آیند، وبا به بنی‌اسرائیل عارض نشود.» ۱۹ 19
Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
پس موسی و هارون و تمامی جماعت بنی‌اسرائیل به لاویان چنین کردند، برحسب هرآنچه خداوند موسی را درباره لاویان امرفرمود، همچنان بنی‌اسرائیل به ایشان عمل نمودند. ۲۰ 20
Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
و لاویان برای گناه خود کفاره کرده، رخت خود را شستند، و هارون ایشان را به حضور خداوند هدیه گذرانید، و هارون برای ایشان کفاره نموده، ایشان را تطهیر کرد. ۲۱ 21
Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
و بعداز آن لاویان داخل شدند تا در خیمه اجتماع به حضور هارون و پسرانش به خدمت خودبپردازند، و چنانکه خداوند موسی را درباره لاویان امر فرمود، همچنان به ایشان عمل نمودند. ۲۲ 22
Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۲۳ 23
Bwana akamwambia Mose,
«این است قانون لاویان که از بیست و پنج ساله و بالاتر داخل شوند تا در کار خیمه اجتماع مشغول خدمت بشوند. ۲۴ 24
“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
و از پنجاه ساله از کارخدمت بازایستند، و بعد از آن خدمت نکنند. ۲۵ 25
lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
لیکن با برادران خود در خیمه اجتماع به نگاهبانی نمودن مشغول شوند، و خدمتی دیگرنکنند. بدین طور با لاویان درباره ودیعت ایشان عمل نما.» ۲۶ 26
Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”

< اعداد 8 >