< نحمیا 11 >

و سروران قوم در اورشلیم ساکن شدند وسایر قوم قرعه انداختند تا از هر ده نفریکنفر را به شهر مقدس اورشلیم، برای سکونت بیاورند و نه نفر باقی، در شهرهای دیگر ساکن شوند. ۱ 1
Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
و قوم، همه کسانی را که به خوشی دل برای سکونت در اورشلیم حاضر شدند، مبارک خواندند. ۲ 2
Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
و اینانند سروران بلدانی که دراورشلیم ساکن شدند، (و سایر اسرائیلیان وکاهنان و لاویان و نتینیم و پسران بندگان سلیمان، هر کس در ملک شهر خود، در شهرهای یهوداساکن شدند). ۳ 3
Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
پس در اورشلیم، بعضی از بنی یهودا وبنی بنیامین سکنی گرفتند. و اما از بنی یهودا، عنایاابن عزیا ابن زکریا ابن امریا ابن شفطیا ابن مهللئیل از بنی فارص. ۴ 4
ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
و معسیا ابن باروک بن کلحوزه ابن حزیا ابن عدایا ابن یویاریب بن زکریا ابن شیلونی. ۵ 5
Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
جمیع بنی فارص که در اورشلیم ساکن شدند، چهار صد و شصت و هشت مرد شجاع بودند. ۶ 6
Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
واینانند پسران بنیامین: سلو ابن مشلام بن یوعید بن فدایا ابن قولایا ابن معسیا ابن ایتئیل بن اشعیا. ۷ 7
Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
وبعد از او جبای و سلای، نه صد و بیست و هشت نفر. ۸ 8
na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
و یوئیل بن زکری، رئیس ایشان بود و یهوداابن هسنوآه، رئیس دوم شهر بود. ۹ 9
Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
و از کاهنان، یدعیا ابن یویاریب و یاکین. ۱۰ 10
Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
و سرایا ابن حلقیاابن مشلام بن صادوق بن مرایوت بن اخیطوب رئیس خانه خدا. ۱۱ 11
Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
و برادران ایشان که درکارهای خانه مشغول می‌بودند هشتصد و بیست و دو نفر. و عدایا ابن یروحام بن فللیا ابن امصی ابن زکریا ابن فشحور بن ملکیا. ۱۲ 12
pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
و برادران او که روسای آبا بودند، دویست و چهل و دو نفر. وعمشیسای بن عزرئیل بن اخزای بن مشلیموت بن امیر. ۱۳ 13
na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
و برادرانش که مردان جنگی بودند، صد وبیست و هشت نفر. و زبدیئیل بن هجدولیم رئیس ایشان بود. ۱۴ 14
na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
و از لاویان شمعیا ابن حشوب بن عزریقام بن حشبیا ابن بونی. ۱۵ 15
Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
و شبتای و یوزابادبر کارهای خارج خانه خدا از روسای لاویان بودند. ۱۶ 16
Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
و متنیا ابن میکا ابن زبدی بن آساف پیشوای تسبیح که در نماز، حمد بگوید و بقبقیاکه از میان برادرانش رئیس دوم بود و عبدا ابن شموع بن جلال بن یدوتون. ۱۷ 17
Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
جمیع لاویان درشهر مقدس دویست و هشتاد و چهار نفر بودند. ۱۸ 18
Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
و دربانان عقوب و طلمون و برادران ایشان که درها را نگاهبانی می‌کردند، صد و هفتاد و دو نفر. ۱۹ 19
Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
و سایر اسرائیلیان و کاهنان و لاویان هر کدام در ملک خویش در جمیع شهرهای یهودا (ساکن شدند). ۲۰ 20
Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
و نتینیم در عوفل سکنی گرفتند وصیحا و جشفا روسای نتینیم ۲۱ 21
Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
و رئیس لاویان در اورشلیم بر کارهای خانه خدا عزی ابن بانی ابن حشبیا ابن متنیا ابن میکا از پسران آساف که مغنیان بودند، می‌بود. ۲۲ 22
Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
زیرا که درباره ایشان حکمی ازپادشاه بود و فریضه‌ای به جهت مغنیان برای امرهر روز در روزش. ۲۳ 23
Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
و فتحیا ابن مشیزبئیل ازبنی زارح بن یهودا از جانب پادشاه برای جمیع امور قوم بود. ۲۴ 24
Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
و بعضی از بنی یهودا در قصبه هاو نواحی آنها ساکن شدند. در قریه اربع و دهات آن و دیبون و دهات آن و یقبصیئیل و دهات آن. ۲۵ 25
Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
و در یشوع و مولاده و بیت فالط. ۲۶ 26
katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
و در حصرشوعال و بئرشبع و دهات آن. ۲۷ 27
katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
و در صقلغ ومکونه و دهات آن. ۲۸ 28
katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
و در عین رمون و صرعه ویرموت. ۲۹ 29
katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
و زانوح و عدلام و دهات آنها ولاکیش و نواحی آن و عزیقه و دهات آن. پس ازبئرشبع تا وادی هنوم ساکن شدند. ۳۰ 30
Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
وبنی بنیامین از جبع تا مکماش ساکن شدند. در عیاو بیت یل و دهات آن. ۳۱ 31
Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
و عناتوت و نوب وعننیه، ۳۲ 32
katika Anathothi, Nobu na Anania,
و حاصور و رامه و جتایم، ۳۳ 33
katika Hazori, Rama na Gitaimu,
و حادیدو صبوعیم و نبلاط، ۳۴ 34
katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
و لود و اونو و وادی حراشیم. ۳۵ 35
katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
و بعضی فرقه های لاویان در یهودا وبنیامین ساکن شدند. ۳۶ 36
Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.

< نحمیا 11 >