< متّی 25 >

«در آن زمان ملکوت آسمان مثل ده باکره خواهد بود که مشعلهای خود رابرداشته، به استقبال داماد بیرون رفتند. ۱ 1
“Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni utakuwa kama wanawali kumi waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana arusi.
و ازایشان پنج دانا و پنج نادان بودند. ۲ 2
Watano wao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.
اما نادانان مشعلهای خود را برداشته، هیچ روغن با خودنبردند. ۳ 3
Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
لیکن دانایان، روغن در ظروف خود بامشعلهای خویش برداشتند. ۴ 4
lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
و چون آمدن دامادبطول انجامید، همه پینکی زده، خفتند. ۵ 5
Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
و درنصف شب صدایی بلند شد که “اینک دامادمی آید به استقبال وی بشتابید.” ۶ 6
“Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
پس تمامی آن باکره‌ها برخاسته، مشعلهای خود را اصلاح نمودند. ۷ 7
“Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
و نادانان، دانایان را گفتند: “از روغن خود به ما دهید زیرا مشعلهای ما خاموش می‌شود.” ۸ 8
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
اما دانایان در جواب گفتند: “نمی شود، مبادا ما و شما را کفاف ندهد. بلکه نزدفروشندگان رفته، برای خود بخرید.” ۹ 9
“Lakini wale wenye busara wakawajibu, ‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu.’
و درحینی که ایشان بجهت خرید می‌رفتند، داماد برسید و آنانی که حاضر بودند، با وی به عروسی داخل شده، در بسته گردید. ۱۰ 10
“Nao walipokuwa wakienda kununua mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa.
بعد از آن، باکره های دیگر نیز آمده، گفتند: “خداوندا برای ماباز کن.” ۱۱ 11
“Baadaye wale wanawali wengine nao wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mlango!’
او در جواب گفت: “هرآینه به شمامی گویم شما را نمی شناسم.” ۱۲ 12
“Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’
پس بیدار باشیدزیرا که آن روز و ساعت را نمی دانید. ۱۳ 13
“Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.
«زیرا چنانکه مردی عازم سفر شده، غلامان خود را طلبید و اموال خود را بدیشان سپرد، ۱۴ 14
“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu aliyetaka kusafiri, naye akawaita watumishi wake na kuweka mali yake kwenye uangalizi wao.
یکی را پنج قنطار و دیگری را دو وسومی را یک داد؛ هر یک را بحسب استعدادش. و بی‌درنگ متوجه سفر شد. ۱۵ 15
Mmoja akampa talantatano, mwingine talanta mbili, na mwingine talanta moja. Kila mmoja alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye akasafiri.
پس آنکه پنج قنطار یافته بود، رفته و با آنها تجارت نموده، پنج قنطار دیگر سود کرد. ۱۶ 16
Yule aliyepewa talanta tano akaenda mara moja akafanya nazo biashara akapata talanta nyingine tano zaidi.
و همچنین صاحب دوقنطار نیز دو قنطار دیگر سود گرفت. ۱۷ 17
Yule aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo, akapata nyingine mbili zaidi.
اما آنکه یک قنطار گرفته بود، رفته زمین را کند و نقد آقای خود را پنهان نمود. ۱۸ 18
Lakini yule mtumishi aliyekuwa amepokea talanta moja, alikwenda akachimba shimo ardhini na kuificha ile fedha ya bwana wake.
«و بعد از مدت مدیدی، آقای آن غلامان آمده، از ایشان حساب خواست. ۱۹ 19
“Baada ya muda mrefu, yule bwana wa wale watumishi akarudi na kufanya hesabu nao.
پس آنکه پنج قنطار یافته بود، پیش آمده، پنج قنطار دیگرآورده، گفت: خداوندا پنج قنطار به من سپردی، اینک پنج قنطار دیگر سود کردم.” ۲۰ 20
Yule mtumishi aliyepokea talanta tano akaja, akaleta nyingine tano zaidi. Akasema, ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta tano zaidi.’
آقای او به وی گفت: آفرین‌ای غلام نیک متدین! بر چیزهای اندک امین بودی، تو را بر چیزهای بسیار خواهم گماشت. به شادی خداوند خود داخل شو! ۲۱ 21
“Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
وصاحب دو قنطار نیز آمده، گفت: ای آقا دو قنطارتسلیم من نمودی، اینک دو قنطار دیگر سودیافته‌ام. ۲۲ 22
“Yule mwenye talanta mbili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, uliweka kwenye uangalizi wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa talanta mbili zaidi.’
آقایش وی را گفت: آفرین‌ای غلام نیک متدین! بر چیزهای کم امین بودی، تو را بر چیزهای بسیار می‌گمارم. در خوشی خداوندخود داخل شو! ۲۳ 23
“Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache; nami nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo ushiriki katika furaha ya bwana wako!’
پس آنکه یک قنطار گرفته بود، پیش آمده، گفت: ای آقا چون تو رامی شناختم که مرد درشت خویی می‌باشی، ازجایی که نکاشته‌ای می‌دروی و از جایی که نیفشانده‌ای جمع می‌کنی، ۲۴ 24
“Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya mbegu.
پس ترسان شده، رفتم و قنطار تو را زیر زمین نهفتم. اینک مال توموجود است. ۲۵ 25
Kwa hiyo niliogopa, nikaenda, nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa ile iliyo mali yako.’
آقایش در جواب وی گفت: ای غلام شریر بیکاره! دانسته‌ای که از جایی که نکاشته‌ام میدروم و از مکانی که نپاشیده‌ام، جمع می‌کنم. ۲۶ 26
“Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna mahali nisipopanda na kukusanya mahali nisipotawanya mbegu.
از همین جهت تو را می‌بایست نقد مرابه صرافان بدهی تا وقتی که بیایم مال خود را باسود بیابم. ۲۷ 27
Vyema basi, ingekupasa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, ili nirudipo, nichukue ile iliyo yangu na faida yake.
الحال آن قنطار را از او گرفته، به صاحب ده قنطار بدهید. ۲۸ 28
“‘Basi mnyangʼanyeni hiyo talanta, mkampe yule mwenye talanta kumi.
زیرا به هر‌که داردداده شود و افزونی یابد و از آنکه ندارد آنچه داردنیز گرفته شود. ۲۹ 29
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
و آن غلام بی‌نفع را در ظلمت خارجی اندازید، جایی که گریه و فشار دندان خواهد بود. ۳۰ 30
Nanyi mtupeni huyo mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
«اما چون پسر انسان در جلال خود باجمیع ملائکه مقدس خویش آید، آنگاه بر کرسی جلال خود خواهد نشست، ۳۱ 31
“Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake.
و جمیع امت‌ها درحضور او جمع شوند و آنها را از همدیگر جدامی کند به قسمی که شبان میشها را از بزها جدامی کند. ۳۲ 32
Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.
و میشها را بر دست راست و بزها را برچپ خود قرار دهد. ۳۳ 33
Atawaweka kondoo upande wake wa kuume, na mbuzi upande wake wa kushoto.
آنگاه پادشاه به اصحاب طرف راست گوید: بیایید‌ای برکت یافتگان از پدر من و ملکوتی را که از ابتدای عالم برای شما آماده‌شده است، به میراث گیرید. ۳۴ 34
“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njooni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu; urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
زیرا چون گرسنه بودم مرا طعام دادید، تشنه بودم سیرآبم نمودید، غریب بودم مرا جا دادید، ۳۵ 35
Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha,
عریان بودم مراپوشانیدید، مریض بودم عیادتم کردید، در حبس بودم دیدن من آمدید. ۳۶ 36
nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’
آنگاه عادلان به پاسخ گویند: ای خداوند، کی گرسنه ات دیدیم تاطعامت دهیم، یا تشنه ات یافتیم تا سیرآبت نماییم، ۳۷ 37
“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu, ‘Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa tukakulisha, au ukiwa na kiu tukakunywesha?
یا کی تو را غریب یافتیم تا تو را جادهیم یا عریان تا بپوشانیم، ۳۸ 38
Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha, au ukiwa uchi tukakuvika?
و کی تو را مریض یامحبوس یافتیم تا عیادتت کنیم؟ ۳۹ 39
Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza, au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’
پادشاه درجواب ایشان گوید: هرآینه به شما می‌گویم، آنچه به یکی از این برادران کوچکترین من کردید، به من کرده‌اید. ۴۰ 40
“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi mlivyomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.’
«پس اصحاب طرف چپ را گوید: ای ملعونان، از من دور شوید در آتش جاودانی که برای ابلیس و فرشتگان او مهیا شده است. (aiōnios g166) ۴۱ 41
“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. (aiōnios g166)
زیراگرسنه بودم مرا خوراک ندادید، تشنه بودم مراآب ندادید، ۴۲ 42
Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha,
غریب بودم مرا جا ندادید، عریان بودم مرا نپوشانیدید، مریض و محبوس بودم عیادتم ننمودید. ۴۳ 43
nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza, na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’
پس ایشان نیز به پاسخ گویند: ای خداوند، کی تو را گرسنه یا تشنه یاغریب یا برهنه یا مریض یا محبوس دیده، خدمتت نکردیم؟ ۴۴ 44
“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi, au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’
آنگاه در جواب ایشان گوید: هرآینه به شما می‌گویم، آنچه به یکی از این کوچکان نکردید، به من نکرده‌اید. ۴۵ 45
“Naye atawajibu, ‘Amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’
و ایشان درعذاب جاودانی خواهند رفت، اما عادلان درحیات جاودانی.» (aiōnios g166) ۴۶ 46
“Ndipo hawa watakapoingia kwenye adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)

< متّی 25 >