< مرقس 4 >

و باز به کناره دریا به تعلیم دادن شروع کردو جمعی کثیر نزد او جمع شدند بطوری که به کشتی سوار شده، بر دریا قرار گرفت و تمامی آن جماعت بر ساحل دریا حاضر بودند. ۱ 1
Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
پس ایشان را به مثلها چیزهای بسیار می‌آموخت و درتعلیم خود بدیشان گفت: ۲ 2
Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
«گوش گیرید! اینک برزگری بجهت تخم پاشی بیرون رفت. ۳ 3
“Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
و چون تخم می‌پاشید، قدری بر راه ریخته شده، مرغان هوا آمده آنها را برچیدند. ۴ 4
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
و پاره‌ای بر سنگلاخ پاشیده شد، در جایی که خاک بسیار نبود. پس چون که زمین عمق نداشت به زودی رویید، ۵ 5
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
وچون آفتاب برآمد، سوخته شد و از آنرو که ریشه نداشت خشکید. ۶ 6
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
و قدری در میان خارها ریخته شد و خارها نمو کرده، آن را خفه نمود که ثمری نیاورد. ۷ 7
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
و مابقی در زمین نیکو افتاد و حاصل پیدا نمود که رویید و نمو کرد و بارآورد، بعضی سی وبعضی شصت و بعضی صد.» ۸ 8
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
پس گفت: «هر‌که گوش شنوا دارد، بشنود!» ۹ 9
Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
و چون به خلوت شد، رفقای او با آن دوازده شرح این مثل را از او پرسیدند. ۱۰ 10
Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
به ایشان گفت: «به شما دانستن سر ملکوت خدا عطاشده، اما به آنانی که بیرونند، همه‌چیز به مثلهامی شود، ۱۱ 11
Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
تا نگران شده بنگرند و نبینند و شنواشده بشنوند و نفهمند، مبادا بازگشت کرده گناهان ایشان آمرزیده شود.» ۱۲ 12
ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
و بدیشان گفت: «آیا این مثل رانفهمیده‌اید؟ پس چگونه سایر مثلها را خواهیدفهمید؟ ۱۳ 13
Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
برزگر کلام را می‌کارد. ۱۴ 14
Yule mpanzi hupanda neno.
و اینانند به کناره راه، جایی که کلام کاشته می‌شود؛ و چون شنیدند فور شیطان آمده کلام کاشته شده درقلوب ایشان را می‌رباید. ۱۵ 15
Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
و ایض کاشته شده درسنگلاخ، کسانی می‌باشند که چون کلام رابشنوند، در حال آن را به خوشی قبول کنند، ۱۶ 16
Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
ولکن ریشه‌ای در خود ندارند بلکه فانی می‌باشند؛ و چون صدمه‌ای یا زحمتی به‌سبب کلام روی دهد در ساعت لغزش می‌خورند. ۱۷ 17
Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
و کاشته شده در خارها آنانی می‌باشند که چون کلام راشنوند، ۱۸ 18
Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
اندیشه های دنیوی و غرور دولت وهوس چیزهای دیگر داخل شده، کلام را خفه می‌کند و بی‌ثمر می‌گردد. (aiōn g165) ۱۹ 19
lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
و کاشته شده درزمین نیکو آنانند که چون کلام را شنوند آن رامی پذیرند و ثمر می‌آورند، بعضی سی و بعضی شصت و بعضی صد.» ۲۰ 20
Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
پس بدیشان گفت: «آیا چراغ را می‌آورند تازیر پیمانه‌ای یا تختی و نه بر چراغدان گذارند؟ ۲۱ 21
Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
زیرا که چیزی پنهان نیست که آشکارا نگردد وهیچ‌چیز مخفی نشود، مگر تا به ظهور آید. ۲۲ 22
Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
هرکه گوش شنوا دارد بشنود.» ۲۳ 23
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
و بدیشان گفت: «باحذر باشید که چه می‌شنوید، زیرا به هر میزانی که وزن کنید به شما پیموده شود، بلکه از برای شماکه می‌شنوید افزون خواهد گشت. ۲۴ 24
Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
زیرا هر‌که دارد بدو داده شود و از هر‌که ندارد آنچه نیز داردگرفته خواهد شد.» ۲۵ 25
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
و گفت: «همچنین ملکوت خدا مانند کسی است که تخم بر زمین بیفشاند، ۲۶ 26
Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
و شب و روزبخوابد و برخیزد و تخم بروید و نمو کند. چگونه؟ او نداند. ۲۷ 27
Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
زیرا که زمین به ذات خودثمر می‌آورد، اول علف، بعد خوشه، پس از آن دانه کامل در خوشه. ۲۸ 28
Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
و چون ثمر رسید، فور داس را بکار می‌برد زیرا که وقت حصاد رسیده است.» ۲۹ 29
Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
و گفت: «به چه چیز ملکوت خدا را تشبیه کنیم و برای آن چه مثل بزنیم؟ ۳۰ 30
Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
مثل دانه خردلی است که وقتی که آن را بر زمین کارند، کوچکترین تخمهای زمینی باشد. ۳۱ 31
Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
لیکن چون کاشته شد، می‌روید و بزرگتر از جمیع بقول می‌گردد و شاخه های بزرگ می‌آورد، چنانکه مرغان هوا زیر سایه‌اش می‌توانند آشیانه گیرند.» ۳۲ 32
Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
و به مثلهای بسیار مانند اینهابقدری که استطاعت شنیدن داشتند، کلام رابدیشان بیان می‌فرمود، ۳۳ 33
Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
و بدون مثل بدیشان سخن نگفت. لیکن در خلوت، تمام معانی را برای شاگردان خود شرح می‌نمود. ۳۴ 34
Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
و در همان روز وقت شام، بدیشان گفت: «به کناره دیگر عبور کنیم.» ۳۵ 35
Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
پس چون آن گروه رارخصت دادند، او را همانطوری که در کشتی بودبرداشتند و چند زورق دیگر نیز همراه او بود. ۳۶ 36
Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
که ناگاه طوفانی عظیم از باد پدید آمد وامواج بر کشتی می‌خورد بقسمی که برمی گشت. ۳۷ 37
Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
و او در موخر کشتی بر بالشی خفته بود. پس اورا بیدار کرده گفتند: «ای استاد، آیا تو را باکی نیست که هلاک شویم؟» ۳۸ 38
Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
در ساعت اوبرخاسته، باد را نهیب داد و به دریا گفت: «ساکن شو و خاموش باش!» که باد ساکن شده، آرامی کامل پدید آمد. ۳۹ 39
Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
و ایشان را گفت: «از بهر‌چه چنین ترسانید و چون است که ایمان ندارید؟» ۴۰ 40
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
پس بی‌نهایت ترسان شده، به یکدیگر گفتند: «این کیست که باد و دریا هم او را اطاعت می‌کنند؟» ۴۱ 41
Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< مرقس 4 >