< لوقا 3 >

و در سال پانزدهم از سلطنت طیباریوس قیصر، در وقتی که پنطیوس پیلاطس، والی یهودیه بود و هیرودیس، تیترارک جلیل وبرادرش فیلپس تیترارک ایطوریه تراخونیتس ولیسانیوس تیترارک آبلیه ۱ 1
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
و حنا و قیافا روسای کهنه بودند، کلام خدا به یحیی ابن زکریا در بیابان نازل شده، ۲ 2
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
به تمامی حوالی اردن آمده، به تعمیدتوبه بجهت آمرزش گناهان موعظه می‌کرد. ۳ 3
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
چنانچه مکتوب است در صحیفه کلمات اشعیای نبی که می‌گوید: «صدای ندا کننده‌ای دربیابان که راه خداوند را مهیا سازید و طرق او راراست نمایید. ۴ 4
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
هر وادی انباشته و هر کوه و تلی پست و هر کجی راست و هر راه ناهموار صاف خواهد شد ۵ 5
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
و تمامی بشر نجات خدا را خواهنددید.» ۶ 6
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
آنگاه به آن جماعتی که برای تعمید وی بیرون می‌آمدند، گفت: «ای افعی‌زادگان، که شمارا نشان داد که از غضب آینده بگریزید؟ ۷ 7
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
پس ثمرات مناسب توبه بیاورید و در خاطر خود این سخن را راه مدهید که ابراهیم پدر ماست، زیرا به شما می‌گویم خدا قادر است که از این سنگها، فرزندان برای ابراهیم برانگیزاند. ۸ 8
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
و الان نیز تیشه بر ریشه درختان نهاده شده است، پس هر درختی که میوه نیکو نیاورد، بریده و در آتش افکنده می‌شود.» ۹ 9
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
پس مردم از وی سوال نموده گفتند: «چه کنیم؟» ۱۰ 10
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
او در جواب ایشان گفت: «هر‌که دوجامه دارد، به آنکه ندارد بدهد. و هرکه خوراک دارد نیز چنین کند.» ۱۱ 11
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
و باجگیران نیز برای تعمید آمده، بدو گفتند: «ای استاد چه کنیم؟» ۱۲ 12
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
بدیشان گفت: «زیادتر از آنچه مقرر است، مگیرید.» ۱۳ 13
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
سپاهیان نیز از او پرسیده، گفتند: «ماچه کنیم؟» به ایشان گفت: «بر کسی ظلم مکنید وبر هیچ‌کس افترا مزنید و به مواجب خود اکتفاکنید.» ۱۴ 14
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
و هنگامی که قوم مترصد می‌بودند و همه در خاطر خود درباره یحیی تفکر می‌نمودندکه این مسیح است یا نه، ۱۵ 15
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
یحیی به همه متوجه شده گفت: «من شما را به آب تعمیدمی دهم، لیکن شخصی تواناتر از من می‌آید که لیاقت آن ندارم که بند نعلین او را باز کنم. اوشما را به روح‌القدس و آتش تعمید خواهد داد. ۱۶ 16
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
او غربال خود را به‌دست خود دارد وخرمن خویش را پاک کرده، گندم را در انبارخود ذخیره خواهد نمود و کاه را در آتشی که خاموشی نمی پذیرد خواهد سوزانید.» ۱۷ 17
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
وبه نصایح بسیار دیگر، قوم را بشارت می‌داد. ۱۸ 18
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
اما هیرودیس تیترارک چون به‌سبب هیرودیا، زن برادر او فیلپس و سایر بدیهایی که هیرودیس کرده بود از وی توبیخ یافت، ۱۹ 19
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
این رانیز بر همه افزود که یحیی را در زندان حبس نمود. ۲۰ 20
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
اما چون تمامی قوم تعمید یافته بودند وعیسی هم تعمید گرفته دعا می‌کرد، آسمان شکافته شد ۲۱ 21
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
و روح‌القدس به هیات جسمانی، مانند کبوتری بر او نازل شد. و آوازی از آسمان در‌رسید که تو پسر حبیب من هستی که به توخشنودم. ۲۲ 22
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
و خود عیسی وقتی که شروع کرد، قریب به سی ساله بود. و حسب گمان خلق، پسر یوسف ابن هالی ۲۳ 23
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
ابن متات، بن لاوی، بن ملکی، بن ینا، بن یوسف، ۲۴ 24
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
ابن متاتیا، بن آموس، بن ناحوم، بن حسلی، بن نجی، ۲۵ 25
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
ابن مات، بن متاتیا، بن شمعی، بن یوسف، بن یهودا، ۲۶ 26
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
ابن یوحنا، بن ریسا، بن زروبابل، بن سالتیئیل، بن نیری، ۲۷ 27
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
ابن ملکی، بن ادی، بن قوسام، بن ایلمودام، بن عیر، ۲۸ 28
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
ابن یوسی، بن ایلعاذر، بن یوریم، بن متات، بن لاوی، ۲۹ 29
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
ابن شمعون، بن یهودا، بن یوسف، بن یونان، بن ایلیاقیم، ۳۰ 30
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
ابن ملیا، بن مینان، بن متاتا بن ناتان، بن داود، ۳۱ 31
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
ابن یسی، بن عوبید، بن بوعز، بن شلمون، بن نحشون، ۳۲ 32
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
ابن عمیناداب، بن ارام، بن حصرون، بن فارص، بن یهودا، ۳۳ 33
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
ابن یعقوب، بن اسحق، بن ابراهیم، بن تارح، بن ناحور، ۳۴ 34
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
ابن سروج، بن رعور، بن فالج، بن عابر، بن صالح، ۳۵ 35
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
ابن قینان، بن ارفکشاد، بن سام، بن نوح، بن لامک، ۳۶ 36
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
ابن متوشالح، بن خنوخ، بن یارد، بن مهللئیل، بن قینان، ۳۷ 37
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
ابن انوش، بن شیث، بن آدم، بن الله. ۳۸ 38
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< لوقا 3 >