< لوقا 22 >

و چون عید فطیر که به فصح معروف است نزدیک شد، ۱ 1
Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
روسای کهنه وکاتبان مترصد می‌بودند که چگونه او را به قتل رسانند، زیرا که از قوم ترسیدند. ۲ 2
Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
اما شیطان در یهودای مسمی به اسخریوطی که از‌جمله آن دوازده بود داخل گشت، ۳ 3
Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
و اورفته با روسای کهنه و سرداران سپاه گفتگو کرد که چگونه او را به ایشان تسلیم کند. ۴ 4
Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
ایشان شادشده با او عهد بستند که نقدی به وی دهند. ۵ 5
Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
و اوقبول کرده در صدد فرصتی برآمد که اورا درنهانی از مردم به ایشان تسلیم کند. ۶ 6
Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
اما چون روز فطیر که در آن می‌بایست فصح را ذبح کنند رسید، ۷ 7
Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
پطرس و یوحنا را فرستاده، گفت: «بروید و فصح را بجهت ما آماده کنید تابخوریم.» ۸ 8
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
به وی گفتند: «در کجا می‌خواهی مهیا کنیم؟» ۹ 9
Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
ایشان را گفت: «اینک هنگامی که داخل شهر شوید، شخصی با سبوی آب به شمابرمی خورد. به خانه‌ای که او درآید، از عقب وی بروید، ۱۰ 10
Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
و به صاحب‌خانه گویید، استاد تو را می گوید مهمانخانه کجا است تا در آن فصح را باشاگردان خود بخورم. ۱۱ 11
Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
او بالاخانه‌ای بزرگ ومفروش به شما نشان خواهد داد در آنجا مهیاسازید.» ۱۲ 12
Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
پس رفته چنانکه به ایشان گفته بودیافتند و فصح را آماده کردند. ۱۳ 13
Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
و چون وقت رسید با دوازده رسول بنشست. ۱۴ 14
Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
و به ایشان گفت: «اشتیاق بی‌نهایت داشتم که پیش از زحمت دیدنم، این فصح را باشما بخورم. ۱۵ 15
Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
زیرا به شما می‌گویم از این دیگرنمی خورم تا وقتی که در ملکوت خدا تمام شود.» ۱۶ 16
Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
پس پیاله‌ای گرفته، شکر نمود و گفت: «این رابگیرید و در میان خود تقسیم کنید. ۱۷ 17
Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
زیرا به شما می‌گویم که تا ملکوت خدا نیاید، از میوه مودیگر نخواهم نوشید.» ۱۸ 18
Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
و نان را گرفته، شکرنمود و پاره کرده، به ایشان داد و گفت: «این است جسد من که برای شما داده می‌شود، این را به یادمن به‌جا آرید.» ۱۹ 19
Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
و همچنین بعد از شام پیاله راگرفت و گفت: «این پیاله عهد جدید است در خون من که برای شما ریخته می‌شود. ۲۰ 20
Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
لیکن اینک دست آن کسی‌که مرا تسلیم می‌کند با من در سفره است. ۲۱ 21
Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
زیرا که پسر انسان برحسب آنچه مقدراست، می‌رود لیکن وای بر آن کسی‌که او را تسلیم کند.» ۲۲ 22
Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
آنگاه از یکدیگر شروع کردند به پرسیدن که کدام‌یک از ایشان باشد که این کار بکند؟ ۲۳ 23
Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
و در میان ایشان نزاعی نیز افتاد که کدام‌یک ازایشان بزرگتر می‌باشد؟ ۲۴ 24
Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
آنگاه به ایشان گفت: «سلاطین امت‌ها بر ایشان سروری می‌کنند وحکام خود را ولی‌نعمت می‌خوانند. ۲۵ 25
Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
لیکن شماچنین مباشید، بلکه بزرگتر از شما مثل کوچکترباشد و پیشوا چون خادم. ۲۶ 26
Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
زیرا کدام‌یک بزرگتراست آنکه به غذا نشیند یا آنکه خدمت کند آیانیست آنکه نشسته است؟ لیکن من در میان شماچون خادم هستم. ۲۷ 27
Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
و شما کسانی می‌باشید که در امتحانهای من با من به‌سر بردید. ۲۸ 28
Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
و من ملکوتی برای شما قرار می‌دهم چنانکه پدرم برای من مقرر فرمود. ۲۹ 29
Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
تا در ملکوت من از خوان من بخورید و بنوشید و بر کرسیها نشسته بردوازده سبط اسرائیل داوری کنید.» ۳۰ 30
ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
پس خداوند گفت: «ای شمعون، ای شمعون، اینک شیطان خواست شما را چون گندم غربال کند، ۳۱ 31
Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
لیکن من برای تو دعا کردم تاایمانت تلف نشود و هنگامی که تو بازگشت کنی برادران خود را استوار نما.» ۳۲ 32
Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
به وی گفت: «ای خداوند حاضرم که با تو بروم حتی در زندان و درموت.» ۳۳ 33
Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
گفت: «تو را می‌گویم‌ای پطرس امروزخروس بانگ نزده باشد که سه مرتبه انکار خواهی کرد که مرا نمی شناسی.» ۳۴ 34
Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
و به ایشان گفت: «هنگامی که شما را بی‌کیسه و توشه‌دان و کفش فرستادم به هیچ‌چیز محتاج شدید؟» گفتند هیچ. ۳۵ 35
Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
پس به ایشان گفت: «لیکن الان هر‌که کیسه دارد، آن را بردارد و همچنین توشه‌دان را و کسی‌که شمشیر ندارد جامه خود را فروخته آن رابخرد. ۳۶ 36
Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
زیرا به شما می‌گویم که این نوشته در من می‌باید به انجام رسید، یعنی با گناهکاران محسوب شد زیرا هر‌چه در خصوص من است، انقضا دارد. ۳۷ 37
Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
گفتند: «ای خداوند اینک دوشمشیر.» به ایشان گفت: «کافی است.» ۳۸ 38
Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
و برحسب عادت بیرون شده به کوه زیتون رفت و شاگردانش از عقب او رفتند. ۳۹ 39
Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
و چون به آن موضع رسید، به ایشان گفت: «دعا کنید تا درامتحان نیفتید.» ۴۰ 40
Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
و او از ایشان به مسافت پرتاپ سنگی دور شده، به زانو درآمد و دعا کرده، گفت: ۴۱ 41
Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
«ای پدر اگر بخواهی این پیاله را از من بگردان، لیکن نه به خواهش من بلکه به اراده تو.» ۴۲ 42
akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
وفرشته‌ای از آسمان بر او ظاهر شده او را تقویت می‌نمود. ۴۳ 43
Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
پس به مجاهده افتاده به سعی بلیغتردعا کرد، چنانکه عرق او مثل قطرات خون بود که بر زمین می‌ریخت. ۴۴ 44
Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
پس از دعا برخاسته نزدشاگردان خود آمده ایشان را از حزن در خواب یافت. ۴۵ 45
Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
به ایشان گفت: «برای چه در خواب هستید؟ برخاسته دعا کنید تا در امتحان نیفتید.» ۴۶ 46
Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
و سخن هنوز بر زبانش بود که ناگاه جمعی آمدند و یکی از آن دوازده که یهودا نام داشت بردیگران سبقت جسته نزد عیسی آمد تا او راببوسد. ۴۷ 47
Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
و عیسی بدو گفت: «ای یهودا آیا به بوسه پسر انسان را تسلیم می‌کنی؟» ۴۸ 48
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
رفقایش چون دیدند که چه می‌شود عرض کردند خداوندابه شمشیر بزنیم. ۴۹ 49
Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
و یکی از ایشان، غلام رئیس کهنه را زده، گوش راست او را از تن جدا کرد. ۵۰ 50
Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
عیسی متوجه شده گفت: «تا به این بگذارید.» وگوش او را لمس نموده، شفا داد. ۵۱ 51
Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
پس عیسی به روسای کهنه و سرداران سپاه هیکل و مشایخی که نزد او آمده بودند گفت: «گویا بر دزد با شمشیرها و چوبها بیرون آمدید. ۵۲ 52
Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
وقتی که هر روزه در هیکل با شما می‌بودم دست بر من دراز نکردید، لیکن این است ساعت شما و قدرت ظلمت.» ۵۳ 53
Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
پس او را گرفته بردند و به‌سرای رئیس کهنه آوردند و پطرس از دور از عقب می‌آمد. ۵۴ 54
Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
و چون در میان ایوان آتش افروخته گردش نشسته بودند، پطرس در میان ایشان بنشست. ۵۵ 55
Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
آنگاه کنیزکی چون او را در روشنی آتش نشسته دید بر او چشم دوخته گفت: «این شخص هم با او می‌بود.» ۵۶ 56
Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
او وی را انکار کرده گفت: «ای زن او را نمی شناسم.» ۵۷ 57
Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
بعد از زمانی دیگری او را دیده گفت: «تو از اینها هستی.» پطرس گفت: «ای مرد، من نیستم.» ۵۸ 58
Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
و چون تخمین یک ساعت گذشت یکی دیگر با تاکیدگفت: «بلاشک این شخص از رفقای او است زیراکه جلیلی هم هست.» ۵۹ 59
Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
پطرس گفت: «ای مردنمی دانم چه می‌گویی؟» در همان ساعت که این رامی گفت خروس بانگ زد. ۶۰ 60
Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
آنگاه خداوندروگردانیده به پطرس نظر افکند پس پطرس آن کلامی را که خداوند به وی گفته بود به‌خاطرآورد که قبل از بانگ زدن خروس سه مرتبه مراانکار خواهی کرد. ۶۱ 61
Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
پس پطرس بیرون رفته زارزار بگریست. ۶۲ 62
Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
و کسانی که عیسی را گرفته بودند، او راتازیانه زده استهزا نمودند. ۶۳ 63
Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
و چشم او را بسته طپانچه بر رویش زدند و از وی سوال کرده، گفتند: «نبوت کن که تو را زده است؟» ۶۴ 64
Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
و بسیارکفر دیگر به وی گفتند. ۶۵ 65
Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
و چون روز شد اهل شورای قوم یعنی روسای کهنه و کاتبان فراهم آمده در مجلس خوداو را آورده، ۶۶ 66
Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
گفتند: «اگر تو مسیح هستی به مابگو: «او به ایشان گفت: «اگر به شما گویم مراتصدیق نخواهید کرد. ۶۷ 67
Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
و اگر از شما سوال کنم جواب نمی دهید و مرا رها نمی کنید. ۶۸ 68
Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
لیکن بعداز این پسر انسان به طرف راست قوت خداخواهد نشست.» ۶۹ 69
Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
همه گفتند: «پس تو پسر خداهستی؟» او به ایشان گفت: «شما می‌گویید که من هستم.» ۷۰ 70
Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
گفتند: «دیگر ما را چه حاجت به شهادت است، زیرا خود از زبانش شنیدیم.» ۷۱ 71
Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”

< لوقا 22 >