< لوقا 16 >

و به شاگردان خود نیز گفت: «شخصی دولتمند را ناظری بود که از او نزد وی شکایت بردند که اموال او را تلف می‌کرد. ۱ 1
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
پس او را طلب نموده، وی را گفت، این چیست که درباره تو شنیده‌ام؟ حساب نظارت خود را باز بده زیرا ممکن نیست که بعد از این نظارت کنی. ۲ 2
Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
ناظر با خود گفت چکنم؟ زیرا مولایم نظارت رااز من می‌گیرد. طاقت زمین‌کندن ندارم و از گدایی نیز عار دارم. ۳ 3
“Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
دانستم چکنم تا وقتی که از نظارت معزول شوم، مرا به خانه خود بپذیرند. ۴ 4
Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
پس هریکی از بدهکاران آقای خود را طلبیده، به یکی گفت آقایم از تو چند طلب دارد؟ ۵ 5
“Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
گفت صدرطل روغن. بدو گفت سیاهه خود را بگیر ونشسته پنجاه رطل بزودی بنویس. ۶ 6
“Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
باز دیگری را گفت از تو چقدر طلب دارد؟ گفت صد کیل گندم. وی را گفت سیاهه خود را بگیر و هشتادبنویس. ۷ 7
“Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
«پس آقایش، ناظر خائن را آفرین گفت، زیراعاقلانه کار کرد. زیرا ابنای این جهان در طبقه خویش از ابنای نور عاقل تر هستند. (aiōn g165) ۸ 8
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn g165)
و من شمارا می‌گویم دوستان از مال بی‌انصافی برای خودپیدا کنید تا چون فانی گردید شما را به خیمه های جاودانی بپذیرند. (aiōnios g166) ۹ 9
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios g166)
آنکه در اندک امین باشد درامر بزرگ نیز امین بود و آنکه در قلیل خائن بود در کثیر هم خائن باشد. ۱۰ 10
“Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
و هرگاه در مال بی‌انصافی امین نبودید، کیست که مال حقیقی را به شمابسپارد؟ ۱۱ 11
Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
و اگر در مال دیگری دیانت نکردید، کیست که مال خاص شما را به شما دهد؟ ۱۲ 12
Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
هیچ خادم نمی تواند دو آقا را خدمت کند. زیرا یا از یکی نفرت می‌کند و با دیگری محبت، یا با یکی می‌پیوندد و دیگری را حقیر می‌شمارد. خدا و مامونا را نمی توانید خدمت نمایید. ۱۳ 13
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
و فریسیانی که زر دوست بودند همه این سخنان را شنیده، او را استهزا نمودند. ۱۴ 14
Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
به ایشان گفت، شما هستید که خود را پیش مردم عادل می‌نمایید، لیکن خدا عارف دلهای شماست. زیرا که آنچه نزد انسان مرغوب است، نزد خدا مکروه است. ۱۵ 15
Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
تورات و انبیا تا به یحیی بود و از آن وقت بشارت به ملکوت خدا داده می‌شود و هر کس بجد و جهد داخل آن می‌گردد. ۱۶ 16
“Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
لیکن آسانتر است که آسمان و زمین زایل شود، از آنکه یک نقطه از تورات ساقط گردد. ۱۷ 17
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
هر‌که زن خود را طلاق دهد و دیگری را نکاح کند زانی بود و هر‌که زن مطلقه مردی را به نکاح خویش درآورد، زنا کرده باشد. ۱۸ 18
“Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
شخصی دولتمند بود که ارغوان و کتان می‌پوشید و هر روزه در عیاشی با جلال بسرمی برد. ۱۹ 19
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
و فقیری مقروح بود ایلعازر نام که او رابر درگاه او می‌گذاشتند، ۲۰ 20
Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
و آرزو می‌داشت که از پاره هایی که از خوان آن دولتمند می‌ریخت، خود را سیر کند. بلکه سگان نیز آمده زبان برزخمهای او می‌مالیدند. ۲۱ 21
Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
باری آن فقیر بمرد و فرشتگان، او را به آغوش ابراهیم بردند و آن دولتمند نیز مرد و او را دفن کردند. ۲۲ 22
“Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
پس چشمان خود را در عالم اموات گشوده، خود رادر عذاب یافت. و ابراهیم را از دور و ایلعازر را درآغوشش دید. (Hadēs g86) ۲۳ 23
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs g86)
آنگاه به آواز بلند گفت، ای پدرمن ابراهیم، بر من ترحم فرما و ایلعازر را بفرست تا سر انگشت خود را به آب تر ساخته زبان مراخنک سازد، زیرا در این نار معذبم. ۲۴ 24
Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
ابراهیم گفت‌ای فرزند به‌خاطر آور که تو در ایام زندگانی چیزهای نیکوی خود را یافتی و همچنین ایلعازرچیزهای بد را، لیکن او الحال در تسلی است و تودر عذاب. ۲۵ 25
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
و علاوه بر این در میان ما و شماورطه عظیمی است، چنانچه آنانی که می‌خواهنداز اینجا به نزد شما عبور کنند، نمی توانند و نه نشینندگان آنجا نزد ما توانند گذشت. ۲۶ 26
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
گفت‌ای پدر به تو التماس دارم که او را به خانه پدرم بفرستی. ۲۷ 27
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
زیرا که مرا پنج برادر است تا ایشان راآگاه سازد، مبادا ایشان نیز به این مکان عذاب بیایند. ۲۸ 28
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
ابراهیم وی را گفت موسی و انبیا رادارند سخن ایشان را بشنوند. ۲۹ 29
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
گفت نه‌ای پدرما ابراهیم، لیکن اگر کسی از مردگان نزد ایشان رود، توبه خواهند کرد. ۳۰ 30
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
وی را گفت هرگاه موسی و انبیا را نشنوند اگر کسی از مردگان نیزبرخیزد، هدایت نخواهند پذیرفت.» ۳۱ 31
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”

< لوقا 16 >