< لاویان 4 >

و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۱ 1
Bwana akamwambia Mose,
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، بگو: اگرکسی سهو گناه کند، در هر کدام از نواهی خداوند که نباید کرد، و به خلاف هریک از آنهاعمل کند، ۲ 2
“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:
اگر کاهن که مسح شده است گناهی ورزد و قوم را مجرم سازد، پس برای گناهی که کرده است، گوساله‌ای بی‌عیب از رمه برای قربانی گناه نزد خداوند بگذراند. ۳ 3
“‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
و گوساله را به درخیمه اجتماع به حضور خداوند بیاورد، و دست خود را بر سر گوساله بنهد و گوساله را به حضورخداوند ذبح نماید. ۴ 4
Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana.
و کاهن مسح شده از خون گوساله گرفته، آن را به خیمه اجتماع درآورد. ۵ 5
Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania.
وکاهن انگشت خود را در خون فرو برد، و به حضور خداوند پیش حجاب قدس قدری ازخون را هفت مرتبه بپاشد. ۶ 6
Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu.
و کاهن قدری ازخون را بر شاخه های مذبح بخور معطر که درخیمه اجتماع است، به حضور خداوند بپاشد، و همه خون گوساله را بر بنیان مذبح قربانی سوختنی که به در خیمه اجتماع است بریزد. ۷ 7
Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
وتمامی پیه گوساله قربانی گناه، یعنی پیهی که احشا را می‌پوشاند و همه پیه را که بر احشاست ازآن بردارد. ۸ 8
Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo,
و دو گرده و پیهی که بر آنهاست که بردو تهیگاه است و سفیدی را که بر جگر است باگرده‌ها جدا کند. ۹ 9
figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote,
چنانکه از گاو ذبیحه سلامتی برداشته می‌شود و کاهن آنها را بر مذبح قربانی سوختنی بسوزاند. ۱۰ 10
kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
و پوست گوساله و تمامی گوشتش با سرش و پاچه هایش و احشایش وسرگینش، ۱۱ 11
Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo,
یعنی تمامی گوساله را بیرون لشکرگاه در مکان پاک جایی که خاکستر رامی ریزند ببرد، و آن را بر هیزم به آتش بسوزاند. در جایی که خاکستر را می‌ریزند سوخته شود. ۱۲ 12
yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.
«و هرگاه تمامی جماعت اسرائیل سهو گناه کنند و آن امر از چشمان جماعت مخفی باشد، و کاری را که نباید کرد از جمیع نواهی خداوند کرده، مجرم شده باشند. ۱۳ 13
“‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia.
چون گناهی که کردند معلوم شود، آنگاه جماعت گوساله‌ای ازرمه برای قربانی گناه بگذرانند و آن را پیش خیمه اجتماع بیاورند. ۱۴ 14
Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania.
و مشایخ جماعت دستهای خود را بر سر گوساله به حضور خداوند بنهند، وگوساله به حضور خداوند ذبح شود. ۱۵ 15
Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana.
و کاهن مسح شده، قدری از خون گوساله را به خیمه اجتماع درآورد. ۱۶ 16
Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania.
و کاهن انگشت خود را درخون فروبرد و آن را به حضور خداوند پیش حجاب هفت مرتبه بپاشد. ۱۷ 17
Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia.
و قدری از خون رابر شاخه های مذبح که به حضور خداوند درخیمه اجتماع است بگذارد، و همه خون را بربنیان مذبح قربانی سوختنی که نزد در خیمه اجتماع است بریزد. ۱۸ 18
Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania.
و همه پیه آن را از آن برداشته، بر مذبح بسوزاند. ۱۹ 19
Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu,
و با گوساله عمل نماید چنانکه با گوساله قربانی گناه عمل کرد، همچنان با این بکند و کاهن برای ایشان کفاره کند، و آمرزیده خواهند شد. ۲۰ 20
naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa.
و گوساله را بیرون لشکرگاه برده، آن را بسوزاند چنانکه گوساله اول را سوزانید. این قربانی گناه جماعت است. ۲۱ 21
Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.
«و هرگاه رئیس گناه کند، و کاری را که نباید کرد از جمیع نواهی یهوه خدای خود سهو بکند و مجرم شود، ۲۲ 22
“‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia.
چون گناهی که کرده است بر او معلوم شود، آنگاه بز نر بی‌عیب برای قربانی خود بیاورد. ۲۳ 23
Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake.
و دست خود را بر سر بز بنهد وآن را در جایی که قربانی سوختنی را ذبح کنند به حضور خداوند ذبح نماید. این قربانی گناه است. ۲۴ 24
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi.
و کاهن قدری از خون قربانی گناه را به انگشت خود گرفته، بر شاخهای مذبح قربانی سوختنی بگذارد، و خونش را بر بنیان مذبح سوختنی بریزد. ۲۵ 25
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
و همه پیه آن را مثل پیه ذبیحه سلامتی بر مذبح بسوزاند، و کاهن برای او گناهش را کفاره خواهد کرد و آمرزیده خواهد شد. ۲۶ 26
Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.
«و هرگاه کسی از اهل زمین سهو گناه ورزدو کاری را که نباید کرد از همه نواهی خداوندبکند و مجرم شود، ۲۷ 27
“‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia.
چون گناهی که کرده است بر او معلوم شود، آنگاه برای قربانی خود بز ماده بی‌عیب بجهت گناهی که کرده است بیاورد. ۲۸ 28
Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda.
ودست خود را بر سر قربانی گناه بنهد و قربانی گناه را در جای قربانی سوختنی ذبح نماید. ۲۹ 29
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka.
و کاهن قدری از خونش را به انگشت خود گرفته، آن را برشاخهای مذبح قربانی سوختنی بگذارد، و همه خونش را بر بنیان مذبح بریزد. ۳۰ 30
Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu.
و همه پیه آن راجدا کند چنانکه پیه از ذبیحه سلامتی جدامی شود، و کاهن آن را بر مذبح بسوزاند برای عطر خوشبو بجهت خداوند و کاهن برای او کفاره خواهد کرد و آمرزیده خواهد شد. ۳۱ 31
Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.
و اگر برای قربانی خود بره‌ای بجهت قربانی گناه بیاورد آن راماده بی‌عیب بیاورد. ۳۲ 32
“‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari.
و دست خود را بر سرقربانی گناه بنهد و آن را برای قربانی گناه در جایی که قربانی سوختنی ذبح می‌شود ذبح نماید. ۳۳ 33
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa.
وکاهن قدری از خون قربانی گناه را به انگشت خودگرفته، بر شاخهای مذبح قربانی سوختنی بگذاردو همه خونش را بر بنیان مذبح بریزد. ۳۴ 34
Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu.
و همه پیه آن را جدا کند، چنانکه پیه بره ذبیحه سلامتی جدا می‌شود، و کاهن آن را بر مذبح بر هدایای آتشین خداوند بسوزاند، و کاهن برای او بجهت گناهی که کرده است کفاره خواهد کرد و آمرزیده خواهد شد. ۳۵ 35
Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.

< لاویان 4 >