< لاویان 3 >

«و اگر قربانی او ذبیحه سلامتی باشد، اگر ازرمه بگذراند خواه نر و خواه ماده باشد، آن را بی‌عیب به حضور خداوند بگذراند. ۱ 1
“‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
و دست خود را بر سر قربانی خویش بنهد، و آن را نزد درخیمه اجتماع ذبح نماید، و پسران هارون کهنه خون را به اطراف مذبح بپاشند. ۲ 2
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
و از ذبیحه سلامتی، هدیه آتشین بجهت خداوند بگذراند، یعنی پیهی که احشا را می‌پوشاند و همه پیه را که بر احشاست. ۳ 3
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
و دو گرده و پیه که بر آنهاست که بر دو تهیگاه است، و سفیدی را که بر جگر است، با گرده‌ها جدا کند. ۴ 4
figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
و پسران هارون آن را برمذبح با قربانی سوختنی بر هیزمی که بر آتش است بسوزانند. این هدیه آتشین و عطر خوشبوبجهت خداوند است. ۵ 5
Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
و اگر قربانی او برای ذبیحه سلامتی بجهت خداوند از گله باشد، آن رانر یا ماده بی‌عیب بگذراند. ۶ 6
“‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
اگر بره‌ای برای قربانی خود بگذراند، آن را به حضور خداوندنزدیک بیاورد. ۷ 7
Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
و دست خود را بر سر قربانی خود بنهد، و آن را نزد در خیمه اجتماع ذبح نماید، و پسران هارون خونش را به اطراف مذبح بپاشند. ۸ 8
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
و از ذبیحه سلامتی هدیه آتشین بجهت خداوند بگذراند، یعنی پیه‌اش و تمامی دنبه را وآن را از نزد عصعص جدا کند، و پیهی که احشا رامی پوشاند و همه پیه را که بر احشاست. ۹ 9
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
و دوگرده و پیهی که بر آنهاست که بر دو تهیگاه است وسفیدی را که بر جگر است با گرده‌ها جدا کند. ۱۰ 10
figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
و کاهن آن را بر مذبح بسوزاند. این طعام هدیه آتشین بجهت خداوند است. ۱۱ 11
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
و اگر قربانی او بز باشد پس آن را به حضور خداوند نزدیک بیاورد. ۱۲ 12
“‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
و دست خود را برسرش بنهد و آن را پیش خیمه اجتماع ذبح نماید. و پسران هارون خونش را به اطراف مذبح بپاشند. ۱۳ 13
Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
و قربانی خود، یعنی هدیه آتشین را، بجهت خداوند از آن بگذراند، پیهی که احشا رامی پوشاند و تمامی پیهی که بر احشاست. ۱۴ 14
Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
و دوگرده و پیهی که بر آنهاست که بر دو تهیگاه است وسفیدی را که بر جگر است با گرده‌ها جدا کند. ۱۵ 15
figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
و کاهن آن را بر مذبح بسوزاند. این طعام هدیه آتشین برای عطر خوشبوست. تمامی پیه از آن خداوند است. ۱۶ 16
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
این قانون ابدی در همه پشتهای شما در جمیع مسکنهای شما خواهد بود که هیچ خون و پیه را نخورید.» ۱۷ 17
“‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”

< لاویان 3 >