< یوشع 20 >

و خداوند یوشع را خطاب کرده، گفت: ۱ 1
Baada ya hayo, Yahweh akamwambia Yoshua,
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، بگو: شهرهای ملجایی را که درباره آنها به واسطه موسی به شما سخن گفتم، برای خود معین سازید ۲ 2
“Waambia watu wa Israeli, na kusema, 'Chagueni miji ya makimbilio ambayo niliwaambia kupitia kwa Musa.
تا قاتلی که کسی را سهو و ندانسته کشته باشدبه آنها فرار کند، و آنها برای شما از ولی مقتول ملجا باشد. ۳ 3
Fanyeni hivi ili mtu akiua mtu bila kukusudia aweze kwenda huko. Miji hii itakuwa ni sehemu ya kukimbilia kutoka kwa mtu yeyote yule anayetaka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa.
و او به یکی از این شهرها فرار کرده، و به مدخل دروازه شهر ایستاده، به گوش مشایخ شهر ماجرای خود را بیان کند، و ایشان او را نزدخود به شهر درآورده، مکانی به او بدهند تا باایشان ساکن شود. ۴ 4
Atakimbilia kwa mji mmoja miongoni mwa miji hiyo na atasimama mlangoni mwa lango la mji, na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule. Kisha watamwingiza ndani ya mji na watampatia sehemu yake ya kuishi miongoni mwao.
و اگر ولی مقتول او را تعاقب کند، قاتل را به‌دست او نسپارند، زیرا که همسایه خود را از نادانستگی کشته، و او را پیش از آن دشمن نداشته بود. ۵ 5
Na kama mtu akija akataka kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa, ndipo watu wa mji hawatatakiwa kumtoa kwa wenye mamlaka mtu huyo aliyeua. Hawaruhusiwi kufanya hivyo kwasababu alimwua jirani bila kukusudia na hakuwa na chuki naye hapo awali.
و در آن شهر تا وقتی که به جهت محاکمه به حضور جماعت حاضر شود تاوفات رئیس کهنه که در آن ایام می‌باشد توقف نماید، و بعد از آن قاتل برگشته، به شهر و به خانه خود یعنی به شهری که از آن فرار کرده بود، داخل شود. ۶ 6
Ni lazima akae katika mji ule mpaka pale atakapokuwa amesimama mbele ya kusanyiko kwa ajili ya kuhukumiwa, hadi pale atakapokufa mtu yule anayetumika katika nafasi ya kuhani mkuu katka siku hizo. Na kisha mtu yule aliyeua bila kukusudia aweza kurudi nyumbani kwake, katika mji ule ulikotoka.
پس قادش را در جلیل در کوهستان نفتالی وشکیم را در کوهستان افرایم و قریه اربع را که درحبرون باشد در کوهستان یهودا، تقدیس نمودند. ۷ 7
Kwahiyo, Waisraeli wakaichaguia Kedeshi iliyoko Galilaya katika nchi ya milima ya Nafutali, Shekemu katika nchi ya milima ya Efraimu, na Kiriathi Arba (ambayo ndio Herbroni) katika nchi ya milima ya Yuda.
و از آن طرف اردن به سمت مشرق اریحا باصررا در صحرا در بیابان از سبط روبین و راموت را درجلعاد از سبط جاد و جولان را در باشان از سبطمنسی تعیین نمودند. ۸ 8
Katika ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko, walichagua mji wa Bezeri huko nyikani katika nyanda za kabila la Rubeni; na Ramothi Gileadi kutoka kabila la Gadi; na Golani katika Bashani, kutoka katika kabila la Manase.
اینهاست شهرهایی که برای تمامی بنی‌اسرائیل و برای غریبی که در میان ایشان ماوا گزیند معین شده بود، تا هر‌که کسی راسهو کشته باشد به آنجا فرار کند، و به‌دست ولی مقتول کشته نشود تا وقتی که به حضور جماعت حاضر شود. ۹ 9
Hii ni miji iliyochaguliwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwao, ili kwamba mtu yeyote amwuaye mtu bila kukusudia aweza kukimbilia huko kwa ajili ya kupata usalama. Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule anayetake kulipiza kisasi cha damu iliyomwagwa, mpaka hapo kwanza mtuhumiwa atakaposimama mbele ya kusanyiko la watu.

< یوشع 20 >