< یوشع 13 >

و یوشع پیر و سالخورده شد، و خداوندبه وی گفت: «تو پیر و سالخورده شده‌ای و هنوز زمین بسیار برای تصرف باقی می‌ماند. ۱ 1
Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
و این است زمینی که باقی می‌ماند، تمامی بلوک فلسطینیان و جمیع جشوریان. ۲ 2
Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
ازشیحور که در مقابل مصر است تا سرحد عقرون به سمت شمال که از کنعانیان شمرده می‌شود، یعنی پنج سردار فلسطینیان از غزیان و اشدودیان و اشقلونیان و جتیان و عقرونیان و عویان. ۳ 3
(tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
و ازجنوب تمامی زمین کنعانیان و مغاره‌ای که ازصیدونیان است تا افیق و تا سرحد اموریان. ۴ 4
Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
وزمین جبلیان و تمامی لبنان به سمت مطلع آفتاب از بعل جاد که زیر کوه حرمون است تا مدخل حمات. ۵ 5
nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
تمامی ساکنان کوهستان از لبنان تامصرفوت مایم که جمیع صیدونیان باشند، من ایشان را از پیش بنی‌اسرائیل بیرون خواهم کرد، لیکن تو آنها را به بنی‌اسرائیل به ملکیت به قرعه تقسیم نما چنانکه تو را امر فرموده‌ام. ۶ 6
Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
پس الان این زمین را به نه سبط و نصف سبط منسی برای ملکیت تقسیم نما.» ۷ 7
Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
با او روبینیان و جادیان ملک خود را گرفتندکه موسی در آن طرف اردن به سمت مشرق به ایشان داد، چنانکه موسی بنده خداوند به ایشان بخشیده بود. ۸ 8
Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
از عروعیر که بر کناره وادی ارنون است، و شهری که در وسط وادی است، و تمامی بیابان میدبا تا دیبون. ۹ 9
kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
و جمیع شهرهای سیهون ملک اموریان که در حشبون تا سرحد بنی عمون حکمرانی می‌کرد. ۱۰ 10
miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
و جلعاد و سرحدجشوریان و معکیان و تمامی کوه حرمون وتمامی باشان تا سلخه. ۱۱ 11
Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
و تمامی ممالک عوج در باشان که در اشتاروت و ادرعی حکمرانی می‌کرد، و او از بقیه رفائیان بود. پس موسی ایشان را شکست داد و بیرون کرد. ۱۲ 12
ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
اما بنی‌اسرائیل جشوریان و معکیان را بیرون نکردند، پس جشور و معکی تا امروز در میان اسرائیل ساکنند. ۱۳ 13
Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
لیکن به سبط لاوی هیچ ملکیت نداد، زیراهدایای آتشین یهوه خدای اسرائیل ملکیت وی است چنانکه به او گفته بود. ۱۴ 14
Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
و موسی به سبط بنی روبین برحسب قبیله های ایشان داد. ۱۵ 15
Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
و حدود ایشان از عروعیربود که به کنار وادی ارنون است و شهری که دروسط وادی است و تمامی بیابان که پهلوی میدبااست. ۱۶ 16
Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
حشبون و تمامی شهرهایش که در بیابان است و دیبون و باموت بعل و بیت بعل معون. ۱۷ 17
Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
ویهصه و قدیموت و میفاعت. ۱۸ 18
na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
و قریتایم و سبمه و سارت شحر که در کوه دره بود. ۱۹ 19
na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
و بیت فغورو دامن فسجه و بیت یشیموت. ۲۰ 20
Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
و تمامی شهرهای بیابان و تمامی ممالک سیهون، ملک اموریان، که در حشبون حکمرانی می‌کرد، وموسی او را با سرداران مدیان یعنی اوی و راقم وصور و حور و رابع، امرای سیهون، که در آن زمین ساکن بودند، شکست داد. ۲۱ 21
miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
و بلعام بن بعور فالگیر را بنی‌اسرائیل در میان کشتگان به شمشیرکشتند. ۲۲ 22
Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
و سرحد بنی روبین اردن و کناره‌اش بود. این ملکیت بنی روبین برحسب قبیله های ایشان بود یعنی شهرها و دهات آنها. ۲۳ 23
Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
و موسی به سبط جاد یعنی به بنی جادبرحسب قبیله های ایشان داد. ۲۴ 24
Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
و سرحد ایشان یعزیز بود و تمامی شهرهای جلعاد و نصف زمین بنی عمون تا عروعیر که در مقابل ربه است. ۲۵ 25
Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
واز حشبون تا رامت مصفه و بطونیم و از محنایم تاسرحد دبیر. ۲۶ 26
kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
و در دره بیت هارام و بیت نمره وسکوت و صافون و بقیه مملکت سیهون، ملک حشبون، و اردن و کناره آن تا انتهای دریای کنرت در آن طرف اردن به سمت مشرق. ۲۷ 27
Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
این است ملکیت بنی جاد برحسب قبیله های ایشان یعنی شهرها و دهات آنها. ۲۸ 28
Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
و موسی به نصف سبط منسی داد و برای نصف سبط بنی منسی برحسب قبیله های ایشان برقرار شد. ۲۹ 29
Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
و حدود ایشان از محنایم تمامی باشان یعنی تمامی ممالک عوج، ملک باشان وتمامی قریه های یائیر که در باشان است، شصت شهر بود. ۳۰ 30
Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
و نصف جلعاد و عشتاروت و ادرعی شهرهای مملکت عوج در باشان برای پسران ماکیر بن منسی یعنی برای نصف پسران ماکیربرحسب قبیله های ایشان بود. ۳۱ 31
nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
اینهاست آنچه موسی در عربات موآب درآن طرف اردن در مقابل اریحا به سمت مشرق برای ملکیت تقسیم کرد. ۳۲ 32
Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
لیکن به سبط لاوی، موسی هیچ نصیب نداد زیرا که یهوه، خدای اسرائیل، نصیب ایشان است چنانکه به ایشان گفته بود. ۳۳ 33
Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.

< یوشع 13 >