< هوشع 9 >

ای اسرائیل مثل قوم‌ها شادی و وجد منمازیرا از خدای خود زنا نمودی و در همه خرمنها اجرت را دوست داشتی. ۱ 1
Usifurahie, ee Israeli; usishangilie kama mataifa mengine. Kwa kuwa hukuwa mwaminifu kwa Mungu wako; umependa ujira wa kahaba kwenye kila sakafu ya kupuria nafaka.
خرمنها وچرخشتها ایشان را پرورش نخواهد داد و شیره در آن ضایع خواهد شد. ۲ 2
Sakafu za kupuria nafaka na mashinikizo ya kukamulia divai havitalisha watu, divai mpya itawapungukia.
در زمین خداوند ساکن نخواهند شد بلکه افرایم به مصر خواهد برگشت و ایشان در آشور چیزهای نجس خواهند خورد. ۳ 3
Hawataishi katika nchi ya Bwana, Efraimu atarudi Misri na atakula chakula kilicho najisi huko Ashuru.
برای خداوند شراب نخواهند ریخت و مقبول او نخواهند شد. قربانی های ایشان مثل خوراک ماتمیان خواهد بود و هرکه از آنها بخورد نجس خواهد شد، زیرا خوراک ایشان برای اشتهای ایشان است. پس آن در خانه خداوند داخل نخواهد شد. ۴ 4
Hawatammiminia Bwana sadaka ya divai wala dhabihu zao hazitampendeza. Dhabihu kama hizo zitakuwa kwao kama mkate wa waombolezaji; nao wote wazilao watakuwa najisi. Chakula hiki kitakuwa kwa ajili yao wenyewe; kisije katika Hekalu la Bwana.
پس در ایام مواسم و در ایام عیدهای خداوند چه خواهید کرد؟ ۵ 5
Mtafanya nini katika siku ya sikukuu zenu zilizoamriwa, katika siku za sikukuu za Bwana?
زیرا اینک از ترس هلاکت رفته‌اند، اما مصر ایشان را جمع خواهدکرد و موف ایشان را دفن خواهد نمود. مکانهای نفیسه نقره ایشان را خارها به تصرف خواهندگرفت و در منازل ایشان شوکها خواهد بود. ۶ 6
Hata ikiwa wataokoka maangamizi, Misri atawakusanya, nayo Memfisi itawazika. Hazina zao za fedha zitasongwa na michongoma, nayo miiba itafunika mahema yao.
ایام عقوبت می‌آید. ایام مکافات می‌رسد و اسرائیل این را خواهند دانست. نبی احمق گردید و صاحب روح دیوانه شد به‌سبب کثرت گناه وفراوانی بغض تو. ۷ 7
Siku za adhabu zinakuja, siku za malipo zimewadia. Israeli na afahamu hili. Kwa sababu dhambi zenu ni nyingi sana na uadui wenu ni mkubwa sana, nabii anadhaniwa ni mpumbavu, mtu aliyeongozwa na Mungu anaonekana mwendawazimu.
افرایم از جانب خدای من دیده بان بود. دام صیاد بر تمامی طریقهای انبیاگسترده شد. در خانه خدای ایشان عداوت است. ۸ 8
Nabii, pamoja na Mungu wangu, ndiye mlinzi juu ya Efraimu, hata hivyo mitego inamngojea katika mapito yake yote, na uadui katika nyumba ya Mungu wake.
مثل ایام جبعه فساد را به نهایت رسانیده‌اند، پس عصیان ایشان را بیاد می‌آورد و گناه ایشان رامکافات خواهد داد. ۹ 9
Wamezama sana katika rushwa, kama katika siku za Gibea. Mungu atakumbuka uovu wao na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.
اسرائیل را مثل انگورها در بیابان یافتم. پدران شما را مثل نوبر انجیر در ابتدای موسمش دیدم. اما ایشان به بعل فغور رفتند و خویشتن رابرای رسوایی نذیره ساختند و مانند معشوقه خود مکروه شدند. ۱۰ 10
“Nilipompata Israeli, ilikuwa kama kupata zabibu jangwani; nilipowaona baba zenu, ilikuwa kama kuona matunda ya kwanza katika mtini. Lakini walipofika Baal-Peori, walijiweka wakfu kwa ile sanamu ya aibu, nao wakawa najisi kama kitu kile walichokipenda.
جلال افرایم مثل مرغ می‌پرد. زاییدن و حامله شدن و در رحم قرارگرفتن نخواهد شد. ۱۱ 11
Utukufu wa Efraimu utaruka kama ndege: hakuna kuzaa, hakuna kuchukua mimba, hakuna kutunga mimba.
و اگر فرزندان را بپرورانندایشان را بی‌اولاد خواهم ساخت به حدی که انسانی نخواهد ماند. وای بر ایشان حینی که من نیز از ایشان دور شوم. ۱۲ 12
Hata wakilea watoto, nitamuua kila mmoja. Ole wao nitakapowapiga kisogo!
افرایم حینی که او رابرگزیدم مثل صور در مرتع نیکو مغروس بود، اماافرایم پسران خود را برای قاتل بیرون خواهدآورد. ۱۳ 13
Nimemwona Efraimu, kama Tiro, aliyeoteshwa mahali pazuri. Lakini Efraimu wataleta watoto wao kwa mchinjaji.”
‌ای خداوند به ایشان بده. چه بدهی؟ رحم سقط کننده و پستانهای خشک به ایشان بده. ۱۴ 14
Wape, Ee Bwana, je, utawapa nini? Wape matumbo ya kuharibu mimba na matiti yaliyokauka.
تمامی شرارت ایشان در جلجال است زیراکه در آنجا از ایشان نفرت داشتم. پس ایشان را به‌سبب اعمال زشت ایشان از خانه خود خواهم راند و ایشان را دیگر دوست نخواهم داشت چونکه جمیع سروران ایشان فتنه انگیزند. ۱۵ 15
“Kwa sababu ya uovu wao wote huko Gilgali, niliwachukia huko. Kwa sababu ya matendo yao ya dhambi, nitawafukuza katika nyumba yangu. Sitawapenda tena, viongozi wao wote ni waasi.
افرایم خشک شده است و ریشه ایشان خشک گردیده، میوه نمی آورند و اگر نیز بزایند نتایج مرغوب رحم ایشان را خواهم کشت. ۱۶ 16
Efraimu ameharibiwa, mzizi wao umenyauka, hawazai tunda. Hata kama watazaa watoto, nitawachinja watoto wao waliotunzwa vizuri.”
خدای من ایشان را ترک خواهد نمود چونکه او را نشنیدند، پس در میان امت‌ها آواره خواهند شد. ۱۷ 17
Mungu wangu atawakataa kwa sababu hawakumtii; watakuwa watu wa kutangatanga miongoni mwa mataifa.

< هوشع 9 >