< هوشع 6 >

بیایید نزد خداوند بازگشت نماییم زیرا که او دریده است و ما را شفا خواهد داد؛ اوزده است و ما را شکسته بندی خواهد نمود. ۱ 1
“Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
بعداز دو روز ما را زنده خواهد کرد. در روز سوم ما راخواهد برخیزانید و در حضور او زیست خواهیم نمود. ۲ 2
Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
پس خداوند را بشناسیم و به جد و جهدمعرفت او را تعاقب نماییم. طلوع او مثل فجریقین است و بر ما مثل باران و مانند باران آخر که زمین را سیراب می‌کند خواهد آمد. ۳ 3
Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
‌ای افرایم با تو چه کنم؟ ای یهودا با تو چه کنم؟ زیرا نیکویی تو مثل ابرهای صبح و مانند شبنم است که بزودی می‌گذرد. ۴ 4
“Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
بنابراین من ایشان را بوسیله انبیا قطع نمودم و به سخنان دهان خود ایشان را کشتم و داوری من مثل نور ساطع می‌شود. ۵ 5
Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
زیرا که رحمت را پسند کردم و نه قربانی را و معرفت خدا را بیشتر از قربانی های سوختنی. ۶ 6
Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
اما ایشان مثل آدم از عهد تجاوزنمودند و درآنجا به من خیانت ورزیدند. ۷ 7
Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
جلعادشهر گناهکاران و خون آلود است. ۸ 8
Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
و چنانکه رهزنان برای مردم در کمین می‌باشند، همچنان جمعیت کاهنان در راه شکیم می‌کشند زیرا که ایشان مرتکب قباحت شده‌اند. ۹ 9
Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
در خاندان اسرائیل عملی هولناک دیدم: افرایم در آنجامرتکب زنا شده، اسرائیل خویشتن را نجس ساخته است. ۱۰ 10
Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
و برای تو نیز‌ای یهودا حصادی معین شده است هنگامی که اسیری قوم خود راخواهم برگردانید. ۱۱ 11
“Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,

< هوشع 6 >