< پیدایش 36 >

و پیدایش عیسو که ادوم باشد، این است: ۱ 1
Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
عیسو زنان خود را از دختران کنعانیان گرفت: یعنی عاده دختر ایلون حتی، واهولیبامه دختر عنی، دختر صبعون حوی، ۲ 2
Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
وبسمه دختر اسماعیل، خواهر نبایوت. ۳ 3
pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
و عاده، الیفاز را برای عیسو زایید، و بسمه، رعوئیل رابزاد، ۴ 4
Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
و اهولیبامه یعوش، و یعلام و قورح رازایید. اینانند پسران عیسو که برای وی در زمین کنعان متولد شدند. ۵ 5
Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
پس عیسو زنان و پسران ودختران و جمیع اهل بیت، و مواشی و همه حیوانات، و تمامی اندوخته خود را که در زمین کنعان اندوخته بود، گرفته، از نزد برادر خودیعقوب به زمین دیگر رفت. ۶ 6
Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
زیرا که اموال ایشان زیاده بود از آنکه با هم سکونت کنند. و زمین غربت ایشان بسبب مواشی ایشان گنجایش ایشان نداشت. ۷ 7
Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
و عیسو در جبل سعیر ساکن شد. وعیسو همان ادوم است. ۸ 8
Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
و این است پیدایش عیسو پدر ادوم در جبل سعیر: ۹ 9
Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
اینست نامهای پسران عیسو: الیفاز پسرعاده، زن عیسو، و رعوئیل، پسر بسمه، زن عیسو. ۱۰ 10
Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
و بنی الیفاز: تیمان و اومار و صفوا و جعتام وقناز بودند. ۱۱ 11
Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
و تمناع، کنیز الیفاز، پسر عیسوبود. وی عمالیق را برای الیفاز زایید. اینانندپسران عاده زن عیسو. ۱۲ 12
Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
و اینانند پسران رعوئیل: نحت و زارع و شمه و مزه. اینانند پسران بسمه زن عیسو. ۱۳ 13
Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
و اینانند پسران اهولیبامه دختر عنی، دختر صبعون، زن عیسو که یعوش ویعلام و قورح را برای عیسو زایید. ۱۴ 14
Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
اینانند امرای بنی عیسو: پسران الیفازنخست زاده عیسو، یعنی امیر تیمان و امیر اومار وامیر صفوا و امیر قناز، ۱۵ 15
Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
و امیر قورح و امیرجعتام و امیر عمالیق. اینانند امرای الیفاز در زمین ادوم. اینانند پسران عاده. ۱۶ 16
Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
و اینان پسران رعوئیل بن عیسو می‌باشند: امیر نحت و امیر زارح و امیر شمه و امیر مزه. اینهاامرای رعوئیل در زمین ادوم بودند. اینانند پسران بسمه زن عیسو. ۱۷ 17
Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
و اینانند بنی اهولیبامه زن عیسو: امیریعوش و امیر یعلام و امیر قورح. اینها امرای اهولیبامه دختر عنی، زن عیسو می‌باشند. ۱۸ 18
Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
اینانند پسران عیسو که ادوم باشد و اینهاامرای ایشان می‌باشند. ۱۹ 19
Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
و اینانند پسران سعیر حوری که ساکن آن زمین بودند، یعنی: لوطان و شوبال و صبعون وعنی، ۲۰ 20
Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
و دیشون و ایصر و دیشان. اینانند امرای حوریان و پسران سعیر در زمین ادوم. ۲۱ 21
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
و پسران لوطان: حوری و هیمام بودند وخواهر لوطان تمناع، بود. ۲۲ 22
Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
و اینانند پسران شوبال: علوان و منحت و عیبال و شفو و اونام. ۲۳ 23
Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
و اینانند بنی صبعون: ایه و عنی. همین عنی است که چشمه های آب گرم را در صحرا پیدانمود، هنگامی که الاغهای پدر خود، صبعون رامی چرانید. ۲۴ 24
Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
و اینانند اولاد عنی: دیشون واهولیبامه دختر عنی. ۲۵ 25
Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
و اینانند پسران دیشان: حمدان و اشبان و بتران و کران. ۲۶ 26
Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
و اینانند پسران ایصر: بلهان و زعوان و عقان. ۲۷ 27
Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
اینانند پسران دیشان: عوص و اران. ۲۸ 28
Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
اینها امرای حوریانند: امیر لوطان و امیرشوبال و امیر صبعون و امیر عنی، ۲۹ 29
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
امیر دیشون و امیر ایصر و امیر دیشان. اینها امرای حوریانند به حسب امرای ایشان در زمین سعیر. ۳۰ 30
Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
و اینانند پادشاهانی که در زمین ادوم سلطنت کردند، قبل از آنکه پادشاهی بربنی‌اسرائیل سلطنت کند: ۳۱ 31
Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
و بالع بن بعور درادوم پادشاهی کرد، و نام شهر او دینهابه بود. ۳۲ 32
Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
وبالع مرد، و در جایش یوباب بن زارح از بصره سلطنت کرد. ۳۳ 33
Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
و یوباب مرد، و در جایش حوشام از زمین تیمانی پادشاهی کرد. ۳۴ 34
Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
وحوشام مرد، و در جایش هداد بن بداد، که درصحرای موآب، مدیان را شکست داد، پادشاهی کرد، و نام شهر او عویت بود. ۳۵ 35
Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
و هداد مرد، و درجایش سمله از مسریقه پادشاهی نمود. ۳۶ 36
Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
وسمله مرد، و شاول از رحوبوت نهر در جایش پادشاهی کرد. ۳۷ 37
Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
و شاول مرد، و در جایش بعل حانان بن عکبور سلطنت کرد. ۳۸ 38
Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
و بعل حانان بن عکبور مرد، و در جایش، هدار پادشاهی کرد. ونام شهرش فاعو بود، و زنش مسمی به مهیطبئیل دختر مطرد، دختر می‌ذاهب بود. ۳۹ 39
Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
و اینست نامهای امرای عیسو، حسب قبائل ایشان و اماکن و نامهای ایشان: امیر تمناع وامیر علوه و امیر یتیت، ۴۰ 40
Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
و امیر اهولیبامه و امیرایله و امیر فینون، ۴۱ 41
Oholibama, Ela, Pinoni,
و امیر قناز و امیرتیمان و امیرمبصار، ۴۲ 42
Kenazi, Temani, Mibsari,
و امیر مجدیئیل و امیر عیرام. اینان امرای ادومند، حسب مساکن ایشان در زمین ملک ایشان. همان عیسو پدر ادوم است. ۴۳ 43
Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.

< پیدایش 36 >