< پیدایش 30 >

یعقوب، اولادی نزایید، راحیل برخواهر خود حسد برد. و به یعقوب گفت: «پسران به من بده والا می‌میرم.» ۱ 1
Raheli alipoona hamzalii Yakobo watoto, akamwonea ndugu yake wivu. Hivyo akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, la sivyo nitakufa!”
آنگاه غضب یعقوب برراحیل افروخته شد و گفت: «مگر من به‌جای خدا هستم که بار رحم را از تو باز داشته است؟» ۲ 2
Yakobo akamkasirikia, akamwambia, “Je, mimi ni badala ya Mungu, ambaye amekuzuia usizae watoto?”
گفت: «اینک کنیز من، بلهه! بدو درآ تا بر زانویم بزاید، و من نیز از او اولاد بیابم.» ۳ 3
Ndipo Raheli akamwambia, “Hapa yupo Bilha, mtumishi wangu wa kike. Kutana naye kimwili ili aweze kunizalia watoto na kwa kupitia yeye mimi pia niweze kuwa na uzao.”
پس کنیز خود، بلهه را به یعقوب به زنی داد. و او به وی درآمد. ۴ 4
Hivyo Raheli akampa Yakobo Bilha awe mke wake. Yakobo akakutana naye kimwili,
وبلهه آبستن شده، پسری برای یعقوب زایید. ۵ 5
Bilha akapata mimba, naye akamzalia Yakobo mwana.
وراحیل گفت: «خدا مرا داوری کرده است، و آوازمرا نیز شنیده، و پسری به من عطا فرموده است.» پس او را دان نام نهاد. ۶ 6
Ndipo Raheli akasema, “Mungu amenipa haki yangu, amesikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita Dani.
و بلهه، کنیز راحیل، بازحامله شده، پسر دومین برای یعقوب زایید. ۷ 7
Bilha mtumishi wa kike wa Raheli akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
وراحیل گفت: «به کشتیهای خدا با خواهر خودکشتی گرفتم و غالب آمدم.» و او را نفتالی نام نهاد. ۸ 8
Ndipo Raheli akasema, “Nilikuwa na mashindano makubwa na ndugu yangu, nami nimeshinda.” Kwa hiyo akamwita Naftali.
و اما لیه چون دید که از زاییدن باز‌مانده بود، کنیز خود زلفه را برداشته، او را به یعقوب به زنی داد. ۹ 9
Lea alipoona kuwa amekoma kuzaa watoto, alimchukua mtumishi wake wa kike Zilpa, naye akampa Yakobo awe mke wake.
و زلفه، کنیز لیه، برای یعقوب پسری زایید. ۱۰ 10
Mtumishi wa Lea yaani Zilpa, akamzalia Yakobo mwana.
و لیه گفت: «به سعادت!» پس او را جادنامید. ۱۱ 11
Ndipo Lea akasema, “Hii ni bahati nzuri aje!” Kwa hiyo akamwita Gadi.
و زلفه، کنیز لیه، پسر دومین برای یعقوب زایید. ۱۲ 12
Mtumishi wa kike wa Lea akamzalia Yakobo mwana wa pili.
و لیه گفت: «به خوشحالی من! زیرا که دختران، مرا خوشحال خواهند خواند.» واو را اشیر نام نهاد. ۱۳ 13
Ndipo Lea aliposema, “Jinsi gani nilivyo na furaha! Wanawake wataniita furaha.” Kwa hiyo akamwita Asheri.
و در ایام درو گندم، روبین رفت و مهرگیاهها در صحرا یافت و آنها را نزدمادر خود لیه، آورد. پس راحیل به لیه گفت: «ازمهرگیاههای پسر خود به من بده.» ۱۴ 14
Wakati wa kuvuna ngano, Reubeni akaenda shambani akakuta tunguja, ambazo alizileta kwa Lea mama yake. Raheli akamwambia Lea, “Tafadhali nakuomba unipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
وی را گفت: «آیا کم است که شوهر مرا گرفتی و مهر گیاه پسرمرا نیز می‌خواهی بگیری؟» راحیل گفت: «امشب به عوض مهر گیاه پسرت، با تو بخوابد.» ۱۵ 15
Lakini Lea akamwambia, “Haikukutosha kumtwaa mume wangu? Je, utachukua na tunguja za mwanangu pia?” Raheli akasema, “Vema sana! Yakobo atakutana nawe kimwili leo usiku, kwa malipo ya tunguja za mwanao.”
ووقت عصر، چون یعقوب از صحرا می‌آمد، لیه به استقبال وی بیرون شده، گفت: «به من درآ، زیرا که تو را به مهرگیاه پسر خود اجیر کردم.» پس آنشب با وی همخواب شد. ۱۶ 16
Kwa hiyo Yakobo alipokuja kutoka shambani jioni ile, Lea akaenda kumlaki, akamwambia, “Lazima ukutane nami kimwili. Nimekukodisha kwa tunguja za mwanangu.” Kwa hiyo akakutana naye kimwili usiku ule.
و خدا، لیه را مستجاب فرمود که آبستن شده، پسر پنجمین برای یعقوب زایید. ۱۷ 17
Mungu akamsikiliza Lea, naye akapata mimba akamzalia Yakobo mwana wa tano.
و لیه گفت: «خدا اجرت به من داده است، زیرا کنیز خود را به شوهر خود دادم.» و او را یساکار نام نهاد. ۱۸ 18
Ndipo Lea akasema, “Mungu amenizawadia kwa kumpa mume wangu mtumishi wangu wa kike.” Kwa hiyo akamwita Isakari.
و بار دیگر لیه حامله شده، پسر ششمین برای یعقوب زایید. ۱۹ 19
Lea akapata mimba tena akamzalia Yakobo mwana wa sita.
و لیه گفت: «خدا عطای نیکو به من داده است. اکنون شوهرم با من زیست خواهد کرد، زیرا که شش پسر برای او زاییدم.» پس او را زبولون نامید. ۲۰ 20
Ndipo Lea aliposema, “Mungu amenizawadia kwa zawadi ya thamani sana. Wakati huu mume wangu ataniheshimu kwa sababu nimemzalia wana sita.” Kwa hiyo akamwita Zabuloni.
و بعد از آن دختری زایید، و او را دینه نام نهاد. ۲۱ 21
Baadaye akamzaa mtoto wa kike akamwita Dina.
پس خداراحیل را بیاد آورد، و دعای او را اجابت فرموده، خدا رحم او را گشود. ۲۲ 22
Ndipo Mungu akamkumbuka Raheli, akasikia maombi yake na akafungua tumbo lake.
و آبستن شده، پسری بزاد و گفت: «خدا ننگ مرا برداشته است.» ۲۳ 23
Akapata mimba na akamzaa mwana na kusema, “Mungu ameniondolea aibu yangu.”
و اورا یوسف نامیده، گفت: «خداوند پسری دیگربرای من مزید خواهد کرد.» ۲۴ 24
Akamwita Yosefu na kusema, “Bwana na anipe mwana mwingine.”
و واقع شد که چون راحیل، یوسف رازایید، یعقوب به لابان گفت: «مرا مرخص کن، تا به مکان و وطن خویش بروم. ۲۵ 25
Baada ya Raheli kumzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani, “Nipe ruhusa nirudi katika nchi yangu.
زنان و فرزندان مراکه برای ایشان، تو را خدمت کرده‌ام به من واگذار، تا بروم زیرا خدمتی که به تو کردم، تو می‌دانی.» ۲۶ 26
Nipe wake zangu na watoto, ambao nimetumika kuwapata, nami niende zangu. Unajua ni kazi kiasi gani ambayo nimekufanyia.”
لابان وی را گفت: «کاش که منظور نظر توباشم، زیرا تفالا یافته‌ام که بخاطر تو، خداوند مرابرکت داده است.» ۲۷ 27
Lakini Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, tafadhali ukae. Nimegundua kwa njia ya uaguzi kwamba Bwana amenibariki kwa sababu yako.”
و گفت: «اجرت خود را برمن معین کن تا آن را به تو دهم.» ۲۸ 28
Akaongeza kumwambia, “Taja ujira wako nami nitakulipa.”
وی را گفت: «خدمتی که به تو کرده‌ام، خود می‌دانی، ومواشی ات چگونه نزد من بود. ۲۹ 29
Yakobo akamwambia, “Unajua jinsi ambavyo nimekutumikia na jinsi ambavyo wanyama wako walivyolishwa vizuri chini ya uangalizi wangu.
زیرا قبل ازآمدن من، مال تو قلیل بود، و به نهایت زیاد شد، وبعد از آمدن من، خداوند تو را برکت داده است. واکنون من نیز تدارک خانه خود را کی ببینم؟» ۳۰ 30
Kidogo ulichokuwa nacho kabla sijaja kimeongezeka sana, naye Bwana amekubariki popote nilipokuwa. Lakini sasa, ni lini nitashughulikia mambo ya nyumba yangu mwenyewe?”
گفت: «پس تو را چه بدهم؟» یعقوب گفت: «چیزی به من مده، اگر این کار را برای من بکنی، بار دیگر شبانی و پاسبانی گله تو را خواهم نمود. ۳۱ 31
Labani akamuuliza, “Nikupe nini?” Yakobo akamjibu, “Usinipe chochote lakini kama utanifanyia jambo hili moja, nitaendelea kuchunga na kuyaangalia makundi yako.
امروز در تمامی گله تو گردش می‌کنم، و هرمیش پیسه و ابلق و هر میش سیاه را از میان گوسفندان، و ابلق‌ها و پیسه‌ها را از بزها، جدامی سازم، و آن، اجرت من خواهد بود. ۳۲ 32
Niruhusu nipite katika makundi yako yote leo niondoe humo kila kondoo mwenye mabakabaka au madoadoa, kila mwana-kondoo mweusi na kila mbuzi mwenye madoadoa au mabakabaka. Hawa watakuwa ujira wangu.
و درآینده عدالت من، بر من شهادت خواهد داد، وقتی که بیایی تا اجرت مرا پیش خود ببینی، آنچه ازبزها، پیسه و ابلق، و آنچه از گوسفندان، سیاه نباشد، نزد من به دزدی شمرده شود.» ۳۳ 33
Uadilifu wangu utanishuhudia siku zijazo, kila utakapochunguza ujira ambao umenilipa mimi. Mbuzi yeyote wangu ambaye hana mabakabaka wala madoadoa, au mwana-kondoo ambaye si mweusi, atahesabika ameibwa.”
لابان گفت: «اینک موافق سخن تو باشد.» ۳۴ 34
Labani akasema, “Ninakubali na iwe kama ulivyosema.”
و در همان روز، بزهای نرینه مخطط و ابلق، و همه ماده بزهای پیسه و ابلق، یعنی هر‌چه سفیدی در آن بود، و همه گوسفندان سیاه را جدا کرده، به‌دست پسران خود سپرد. ۳۵ 35
Siku ile ile Yakobo akawaondoa beberu wote waliokuwa na mistari au madoadoa na mbuzi wake wote waliokuwa na mistari au madoadoa (wote waliokuwa na alama nyeupe juu yao) na wana-kondoo weusi wote, akawaweka chini ya uangalizi wa wanawe.
و در میان خود و یعقوب، سه روز راه، مسافت گذارد. و یعقوب باقی گله لابان را شبانی کرد. ۳۶ 36
Kisha Labani akamwacha Yakobo kwa mwendo wa safari ya siku tatu kati yake na Yakobo, wakati Yakobo akiendelea kuchunga lile kundi la Labani lililobaki.
و یعقوب چوبهای تر و تازه از درخت کبوده و بادام و چنار برای خود گرفت، و خطهای سفید در آنها کشید، و سفیدی را که در چوبها بود، ظاهر کرد. ۳۷ 37
Hata hivyo, Yakobo, akachukua fito mbichi zilizokatwa wakati huo huo za miti ya mlubna, mlozi na mwaramoni akazibambua ili mistari myeupe ionekane katika fito hizo.
و وقتی که گله‌ها، برای آب خوردن می‌آمدند، آن چوبهایی را که خراشیده بود، درحوضها و آبخورها پیش گله‌ها می‌نهاد، تا چون برای نوشیدن بیایند، حمل بگیرند. ۳۸ 38
Kisha akaweka fito alizozibambua kwenye mabirika yote ya kunyweshea mifugo, ili ziwe mbele ya makundi walipokuja kunywa maji. Wanyama walipokuja kunywa maji, hali wakiwa wanahitaji mbegu,
پس گله هاپیش چوبها بارآور می‌شدند، و بزهای مخطط وپیسه و ابلق می‌زاییدند. ۳۹ 39
wakapandwa hizo fito zikiwa mbele yao. Wanyama waliopata mimba mbele ya hizo fito walizaa wanyama wenye mistari, madoadoa na mabakabaka.
و یعقوب، بزها را جداکرد، و روی گله‌ها را بسوی هر مخطط و سیاه درگله لابان واداشت، و گله های خود را جدا کرد و باگله لابان نگذاشت. ۴۰ 40
Yakobo akawatenga wadogo wa kundi peke yao, lakini akazielekeza nyuso za hao waliobaki kwenye wale wenye mistari na weusi waliokuwa mali ya Labani. Hivyo akatenga makundi yake mwenyewe, na wala hakuwachanganya na wanyama wa Labani.
و هرگاه حیوان های تنومندحمل می‌گرفتند، یعقوب چوبها را پیش آنها درآبخورها می‌نهاد، تا در میان چوبها حمل گیرند. ۴۱ 41
Kila mara wanyama wenye nguvu walipohitaji mbegu, Yakobo aliweka zile fito kwenye mabirika mbele ya hao wanyama, ili wapandwe karibu na hizo fito,
و هر گاه حیوانات ضعیف بودند، آنها رانمی گذاشت، پس ضعیف‌ها از آن لابان، وتنومندها از آن یعقوب شدند. ۴۲ 42
lakini ikiwa wanyama walikuwa wadhaifu hakuziweka hizo fito. Hivyo wanyama wadhaifu wakawa wa Labani, na wanyama wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
و آن مرد بسیارترقی نمود، و گله های بسیار و کنیزان و غلامان وشتران و حماران بهم رسانید. ۴۳ 43
Kwa njia hii Yakobo akastawi sana, tena akawa na makundi makubwa, watumishi wa kike na wa kiume na ngamia na punda.

< پیدایش 30 >