< استر 1 >

در ایام اخشورش (این امور واقع شد). این همان اخشورش است که از هند تا حبش، بر صد و بیست و هفت ولایت سلطنت می‌کرد. ۱ 1
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
در آن ایام حینی که اخشورش پادشاه، بر کرسی سلطنت خویش در دارالسلطنه شوشن نشسته بود. ۲ 2
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
در سال سوم از سلطنت خویش، ضیافتی برای جمیع سروران و خادمان خود برپا نمود و حشمت فارس ومادی از امرا و سروران ولایتها، به حضور او بودند. ۳ 3
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
پس مدت مدید صد و هشتاد روز، توانگری جلال سلطنت خویش و حشمت مجد عظمت خود را جلوه می‌داد. ۴ 4
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
پس بعد از انقضای آنروزها، پادشاه برای همه کسانی که دردارالسلطنه شوشن از خرد و بزرگ یافت شدند، ضیافت هفت روزه در عمارت باغ قصر پادشاه برپا نمود. ۵ 5
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
پرده‌ها از کتان سفید و لاجورد، با ریسمانهای سفید و ارغوان در حلقه های نقره بر ستونهای مرمر سفید آویخته وتختهای طلا و نقره بر سنگفرشی از سنگ سماق و مرمر سفید و در و مرمر سیاه بود. ۶ 6
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
و آشامیدن، از ظرفهای طلابود و ظرفها را اشکال مختلفه بود و شرابهای ملوکانه برحسب کرم پادشاه فراوان بود. ۷ 7
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
و آشامیدن برحسب قانون بود که کسی بر کسی تکلف نمی نمود، زیرا پادشاه درباره همه بزرگان خانه‌اش چنین امر فرموده بود که هر کس موافق میل خود رفتار نماید. ۸ 8
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
و وشتی ملکه نیز ضیافتی برای زنان خانه خسروی اخشورش پادشاه برپا نمود. ۹ 9
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
در روز هفتم، چون دل پادشاه از شراب خوش شد، هفت خواجه‌سرا یعنی مهومان و بزتا و حربونا و بغتا و ابغتا و زاتر و کرکس را که درحضور اخشورش پادشاه خدمت می‌کردند، امر فرمود ۱۰ 10
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
که وشتی ملکه را با تاج ملوکانه به حضور پادشاه بیاورندتا زیبایی او را به خلایق و سروران نشان دهد، زیرا که نیکو منظر بود. ۱۱ 11
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
اما وشتی ملکه نخواست که برحسب فرمانی که پادشاه به‌دست خواجه‌سرایان فرستاده بود بیاید. پس پادشاه بسیار خشمناک شده، غضبش در دلش مشتعل گردید. ۱۲ 12
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
آنگاه پادشاه به حکیمانی که از زمانها مخبر بودند تکلم نموده، (زیرا که عادت پادشاه با همه کسانی که به شریعت و احکام عارف بودند چنین بود. ۱۳ 13
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
و مقربان او کرشنا و شیتار و ادماتا و ترشیش و مرس و مرسنا ومموکان، هفت رئیس فارس و مادی بودند که روی پادشاه را می‌دیدند و در مملکت به درجه اول می‌نشستند) ۱۴ 14
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
گفت: «موافق شریعت، به وشتی ملکه چه باید کرد؟ چونکه به فرمانی که اخشورش پادشاه به‌دست خواجه‌سرایان فرستاده است، عمل ننموده.» ۱۵ 15
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
آنگاه مموکان به حضور پادشاه و سروران عرض کرد که «وشتی ملکه، نه‌تنها به پادشاه تقصیر نموده، بلکه به همه روسا و جمیع طوایفی که در تمامی ولایتهای اخشورش پادشاه می‌باشند، ۱۶ 16
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
زیرا چون این عمل ملکه نزد تمامی زنان شایع شود، آنگاه شوهرانشان در نظر ایشان خوار خواهند شد، حینی که مخبر شوند که اخشورش پادشاه امر فرموده است که وشتی ملکه را به حضورش بیاورند و نیامده است. ۱۷ 17
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
و در آنوقت، خانمهای فارس و مادی که این عمل ملکه را بشنوند، به جمیع روسای پادشاه چنین خواهند گفت و این مورد بسیار احتقار و غضب خواهد شد. ۱۸ 18
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
پس اگر پادشاه این رامصلحت داند، فرمان ملوکانه‌ای از حضور وی صادر شود و در شرایع فارس و مادی ثبت گردد، تا تبدیل نپذیرد، که وشتی به حضور اخشورش پادشاه دیگر نیاید و پادشاه رتبه ملوکانه او را به دیگری که بهتر از او باشد بدهد. ۱۹ 19
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
وچون فرمانی که پادشاه صادر گرداند در تمامی مملکت عظیم او مسموع شود، آنگاه همه زنان شوهران خود را ازبزرگ و کوچک، احترام خواهند نمود.» ۲۰ 20
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
و این سخن در نظر پادشاه و روسا پسندآمد و پادشاه موافق سخن مموکان عمل نمود. ۲۱ 21
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
و مکتوبات به همه ولایتهای پادشاه به هرولایت، موافق خط آن و به هر قوم، موافق زبانش فرستاد تا هر مرد در خانه خود مسلط شود و درزبان قوم خود آن را بخواند. ۲۲ 22
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< استر 1 >