< تثنیه 30 >

و چون جمیع این چیزها، یعنی برکت ولعنتی که پیش روی تو گذاشتم بر توعارض شود، و آنها را در میان جمیع امتهایی که یهوه، خدایت، تو را به آنجا خواهد راند، بیادآوری. ۱ 1
Vitu hivi vitakavyokuja juu yako, baraka na laana nilizoziweka mbele yako, na utakapozirejea akilini miongoni mwa mataifa mengine ambapo Yahwe Mungu wako kawapeleka,
و تو با فرزندانت با تمامی دل و تمامی جان خود به سوی یهوه خدایت بازگشت نموده، قول او را موافق هر‌آنچه که من امروز به تو امرمی فرمایم، اطاعت نمایی. ۲ 2
na utakapomrudia Yahwe Mungu wako na kutii sauti yake, na kufuata yote ambayo nayokuamuru leo – wewe na watoto wako – kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote,
آنگاه یهوه خدایت اسیری تو را برگردانیده، بر تو ترحم خواهد کرد، و رجوع کرده، تو را از میان جمیع امتهایی که یهوه، خدایت، تو را به آنجا پراکنده کرده است، جمع خواهد نمود. ۳ 3
kisha Yahwe Mungu wako atageuza kutekwa kwako na kukuhurumia; atawarudisha na kuwakusanya kutoka kwa watu wote ambapo Yahwe Mungu wako aliwatawanya.
اگر آوارگی تو تا کران آسمان بشود، یهوه، خدایت، تو را از آنجا جمع خواهد کرد و تو را از آنجا خواهد آورد. ۴ 4
Iwapo yeyote ya watu walio uhamishoni wapo katika sehemu za mbali sana chini ya mbingu, kutoka huko Yawhe Mungu wako atawakusanya, na kutoka huko atawarejesha.
ویهوه، خدایت، تو را به زمینی که پدرانت مالک آن بودند خواهد آورد، و مالک آن خواهی شد، و برتو احسان نموده، تو را بیشتر از پدرانت خواهدافزود. ۵ 5
Yahwe Mungu wako atawaleta katika nchi ambayo mababu zenu walimiliki, nanyi mtaimiliki tena; atawatendea mema na kuwazidisha zaidi ya alivyofanya kwa mababu zenu.
«و یهوه خدایت دل تو و دل ذریت تو رامختون خواهد ساخت تا یهوه خدایت را به تمامی دل و تمامی جان خود دوست داشته، زنده بمانی. ۶ 6
Yahwe Mungu wako atatahiri moyo wako na moyo wa uzao wako, ili umpende Yahwe Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote, ili kwamba uweze kuishi.
و یهوه خدایت جمیع این لعنتها را بردشمنان و بر خصمانت که تو را آزردند، نازل خواهد گردانید. ۷ 7
Yahwe Mungu wako ataweka laana hizi zote kwa maadui zako na kwa wote wakuchukiayo, wale waliokutesa.
و تو بازگشت نموده، قول خداوند را اطاعت خواهی کرد، و جمیع اوامر او را که من امروز به تو امر می‌فرمایم، بجا خواهی آورد. ۸ 8
Utarudi na kutii sauti ya Yahwe, nawe utatenda amri zake zote ambazo ninakuamuru leo.
و یهوه، خدایت، تو را در تمامی اعمال دستت و در میوه بطنت و نتایج بهایمت ومحصول زمینت به نیکویی خواهد افزود، زیراخداوند بار دیگر بر تو برای نیکویی شادی خواهد کرد، چنانکه بر پدران تو شادی نمود. ۹ 9
Yahwe Mungu wako atakufanikisha katika kazi yote ya mkono wako, katika matunda ya mwili wako, katika matunda ya mifugo yako, na katika matunda ya nchi yako, kwa mafanikio; kwa maana Yahwe atafurahia tena mafanikio yako, kama alivyofurahia kwa baba zako.
اگر آواز یهوه خدای خود را اطاعت نموده، اوامر و فرایض او را که در طومار این شریعت مکتوب است، نگاه داری، و به سوی یهوه، خدای خود، با تمامی دل و تمامی جان بازگشت نمایی. ۱۰ 10
Atafanya hivi iwapo utatii sauti ya Yahwe Mungu wako, ili kuzishika amri zake na kanuni zake zilizoandikwa katika kitabu hiki cha sheria, iwapo utamgeukia Yahwe Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.
«زیرا این حکمی که من امروز به تو امرمی فرمایم، برای تو مشکل نیست و از تو دورنیست. ۱۱ 11
Kwa maana amri hii nayokuamuru leo sio ngumu sana, wala haipo nje ya uwezo wako kufikia.
نه در آسمان است تا بگویی کیست که به آسمان برای ما صعود کرده، آن را نزد ما بیاوردو آن را به ما بشنواند تا به عمل آوریم. ۱۲ 12
Haipo mbinguni, ili usije ukasema, “Nani atayekwenda kwa ajili yetu mbinguni na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kutekeleza?”
و نه آن طرف دریا که بگویی کیست که برای ما به آنطرف دریا عبور کرده، آن را نزد ما بیاورد و به ما بشنواندتا به عمل آوریم. ۱۳ 13
Wala haipo ng’ambo ya bahari, ili usije ukasema, “Nani atakwenda ng’ambo ya pili ya bahari kwa ajili yetu na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kuifanya?”.
بلکه این کلام، بسیار نزدیک توست و در دهان و دل توست تا آن را بجا آوری. ۱۴ 14
Lakini neno lipo karibu sana kwako, katika kinywa chako na moyo wako, ili uweze kutekeleza.
«ببین امروز حیات و نیکویی و موت و بدی را پیش روی تو گذاشتم. ۱۵ 15
Tazama, leo nimeweka mbele yako uzima na wema, mauti na uovu.
چونکه من امروز تورا امر می‌فرمایم که یهوه خدای خود را دوست بداری و در طریقهای او رفتار نمایی، و اوامر وفرایض و احکام او را نگاه داری تا زنده مانده، افزوده شوی، و تا یهوه، خدایت، تو را در زمینی که برای تصرفش به آن داخل می‌شوی، برکت دهد. ۱۶ 16
Iwapo utatii maagizo ya Yahwe Mungu wako, ambayo ninakuamuru leo kumpenda Yahwe Mungu wako, kutembea katika njia zake, na kushikilia amri zake, kanuni zake, na sheria zake, utaishi na kuongezeka, na Yahwe Mungu wako atakubariki katika nchi ambayo unaingia kumiliki.
لیکن اگر دل تو برگردد و اطاعت ننمایی و فریفته شده، خدایان غیر را سجده و عبادت نمایی، ۱۷ 17
Lakini moyo wako ukigeuka, na usisikilize na badala yake unavutwa na kusujudia miungu mingine na kuwaabudu,
پس امروز به شما اطلاع می‌دهم که البته هلاک خواهید شد، و در زمینی که از اردن عبور می‌کنید تا در آن داخل شده، تصرف نمایید، عمر طویل نخواهید داشت. ۱۸ 18
basi leo nakutangazia kwako ya kwamba hakika utaangamia; siku zako hazitaongezeka katika nchi unayoipita juu ya Yordani kuingia na kumiliki.
امروز آسمان وزمین را بر شما شاهد می‌آورم که حیات و موت وبرکت و لعنت را پیش روی تو گذاشتم، پس حیات را برگزین تا تو با ذریتت زنده بمانی. ۱۹ 19
Naziita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yako ya kuwa nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; kwa hiyo chagua uzima ili kwamba uweze kuishi, wewe na uzao wako.
و تایهوه خدای خود را دوست بداری و آواز او رابشنوی و با او ملصق شوی، زیرا که او حیات تو ودرازی عمر توست تا در زمینی که خداوند برای پدرانت، ابراهیم و اسحاق و یعقوب، قسم خوردکه آن را به ایشان بدهد، ساکن شوی.» ۲۰ 20
Fanya hivi ili umpende Yahwe Mungu wako, kutii sauti yake, na kung’ang’ania kwake. Kwa maana yeye ni uzima wako na urefu wa siku zako; fanya hivi ili kwamba uweze kuishi katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka, na kwa Yakobo, kuwapatia.

< تثنیه 30 >