< کارهای رسولان 1 >

صحیفه اول را انشا نمودم، ای تیوفلس، درباره همه اموری که عیسی به عمل نمودن و تعلیم دادن آنها شروع کرد. ۱ 1
Katika kitabu changu cha kwanza nilikuandikia, mpendwa Theofilo, kuhusu mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu mwanzo,
تا آن روزی که رسولان برگزیده خود را به روح‌القدس حکم کرده، بالا برده شد. ۲ 2
hadi siku ile alipochukuliwa kwenda mbinguni, baada ya kuwapa maagizo kupitia kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
که بدیشان نیز بعد از زحمت کشیدن خود، خویشتن را زنده ظاهر کرد به دلیلهای بسیار که در مدت چهل روز بر ایشان ظاهر می‌شد و درباره امور ملکوت خدا سخن می‌گفت. ۳ 3
Baada ya mateso yake, alijionyesha kwao na kuwathibitishia kwa njia nyingi kwamba yeye yu hai. Katika muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake aliwatokea na kunena kuhusu Ufalme wa Mungu.
و چون با ایشان جمع شد، ایشان راقدغن فرمود که «از اورشلیم جدا مشوید، بلکه منتظر آن وعده پدر باشید که از من شنیده‌اید. ۴ 4
Wakati mmoja alipokuwa pamoja nao, aliwapa amri hii, “Msitoke Yerusalemu, bali ingojeni ahadi ya Baba, ambayo mmenisikia nikisema habari zake.
زیرا که یحیی به آب تعمید می‌داد، لیکن شمابعد از اندک ایامی، به روح‌القدس تعمید خواهیدیافت.» ۵ 5
Yohana aliwabatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
پس آنانی که جمع بودند، از او سوال نموده، گفتند: «خداوندا آیا در این وقت ملکوت را براسرائیل باز برقرار خواهی داشت؟» ۶ 6
Mitume walipokuwa wamekusanyika pamoja, wakamuuliza Yesu, “Bwana, je, huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme?”
بدیشان گفت: «از شما نیست که زمانها و اوقاتی را که پدردر قدرت خود نگاه داشته است بدانید. ۷ 7
Yesu akawaambia, “Si juu yenu kujua nyakati na majira ambayo Baba ameyaweka katika mamlaka yake mwenyewe.
لیکن چون روح‌القدس بر شما می‌آید، قوت خواهیدیافت و شاهدان من خواهید بود، در اورشلیم وتمامی یهودیه و سامره و تا اقصای جهان.» ۸ 8
Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, Uyahudi kote na Samaria, hadi miisho ya dunia.”
و چون این را گفت، وقتی که ایشان همی نگریستند، بالا برده شد و ابری او را از چشمان ایشان در ربود. ۹ 9
Baada ya kusema mambo haya, walipokuwa wanatazama, akachukuliwa juu mbinguni mbele ya macho yao na wingu likampokea wasimwone tena.
و چون به سوی آسمان چشم دوخته می‌بودند، هنگامی که او می‌رفت، ناگاه دومرد سفیدپوش نزد ایشان ایستاده، ۱۰ 10
Walipokuwa bado wakikaza macho yao kuelekea juu alipokuwa akienda zake Mbinguni, tazama ghafula, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama karibu nao,
گفتند: «ای مردان جلیلی چرا ایستاده، به سوی آسمان نگرانید؟ همین عیسی که از نزد شما به آسمان بالابرده شد، باز خواهد آمد به همین طوری که او رابه سوی آسمان روانه دیدید.» ۱۱ 11
wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama mkitazama juu angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda Mbinguni, atarudi tena jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake Mbinguni.”
آنگاه به اورشلیم مراجعت کردند، از کوه مسمی به زیتون که نزدیک به اورشلیم به مسافت سفر یک روز سبت است. ۱۲ 12
Ndipo waliporudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, uliokuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa mwendo wa Sabato kutoka mjini.
و چون داخل شدند، به بالاخانه‌ای برآمدند که در آنجا پطرس و یوحناو یعقوب و اندریاس و فیلپس و توما و برتولما ومتی و یعقوب بن حلفی و شمعون غیور و یهودای برادر بعقوب مقیم بودند. ۱۳ 13
Walipowasili mjini Yerusalemu, walikwenda ghorofani kwenye chumba walichokuwa wakiishi. Wale waliokuwepo walikuwa: Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
و جمیع اینها با زنان و مریم مادر عیسی و برادران او به یکدل درعبادت و دعا مواظب می‌بودند. ۱۴ 14
Hawa wote waliungana pamoja katika maombi. Pamoja nao walikuwepo wanawake kadha, na Maria mama yake Yesu, pamoja na ndugu zake Yesu.
و در آن ایام، پطرس در میان برادران که عدد اسامی ایشان جمله قریب به صد و بیست بود برخاسته، گفت: ۱۵ 15
Katika siku hizo Petro akasimama katikati ya waumini (jumla yao wote walikuwa watu wapatao 120), akasema,
«ای برادران، می‌بایست آن نوشته تمام شود که روح‌القدس از زبان داودپیش گفت درباره یهودا که راهنما شد برای آنانی که عیسی را گرفتند. ۱۶ 16
“Ndugu zangu, ilibidi Andiko litimie ambalo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.
که او با ما محسوب شده، نصیبی در این خدمت یافت. ۱۷ 17
Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.”
پس او از اجرت ظلم خود، زمینی خریده، به روی درافتاده، ازمیان پاره شد و تمامی امعایش ریخته گشت. ۱۸ 18
(Basi Yuda alinunua shamba kwa zile fedha za uovu alizopata; akiwa huko shambani akaanguka, akapasuka na matumbo yote yakatoka nje.
وبر تمام سکنه اورشلیم معلوم گردید چنانکه آن زمین در لغت ایشان به حقل دما، یعنی زمین خون نامیده شد. ۱۹ 19
Kila mtu Yerusalemu akasikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani Shamba la Damu).
زیرا در کتاب زبور مکتوب است که خانه او خراب بشود و هیچ‌کس در آن مسکن نگیرد و نظارتش را دیگری ضبط نماید. ۲۰ 20
“Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Zaburi, “‘Mahali pake na pawe ukiwa, wala asiwepo yeyote atakayeishi humo,’ na, “‘Mtu mwingine aichukue nafasi yake ya uongozi.’
الحال می‌باید از آن مردمانی که همراهان ما بودند، درتمام آن مدتی که عیسی خداوند با ما آمد و رفت می‌کرد، ۲۱ 21
Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine miongoni mwa wale ambao wamekuwa pamoja nasi wakati wote Bwana Yesu alipoingia na kutoka katikati yenu,
از زمان تعمید یحیی، تا روزی که ازنزد ما بالا برده شد، یکی از ایشان با ما شاهدبرخاستن او بشود.» ۲۲ 22
kuanzia ubatizo wa Yohana mpaka siku aliyochukuliwa kutoka kwetu kwenda Mbinguni. Kwa kuwa mmoja wao inabidi awe shahidi pamoja nasi wa ufufuo wake.”
آنگاه دو نفر یعنی یوسف مسمی به برسباکه به یوستس ملقب بود و متیاس را برپا داشتند، ۲۳ 23
Wakapendekeza majina ya watu wawili: Yosefu, aitwaye Barsaba (ambaye pia alijulikana kama Yusto) na Mathiya.
و دعا کرده، گفتند: «تو‌ای خداوند که عارف قلوب همه هستی، بنما کدام‌یک از این دو رابرگزیده‌ای ۲۴ 24
Kisha wakaomba, wakasema, “Bwana, wewe waujua moyo wa kila mtu. Tuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
تا قسمت این خدمت و رسالت رابیابد که یهودا از آن باز افتاده، به مکان خودپیوست.» ۲۵ 25
ili achukue nafasi ya huduma ya utume ambayo Yuda aliiacha ili aende mahali pake mwenyewe.”
پس قرعه به نام ایشان افکندند وقرعه به نام متیاس برآمد و او با یازده رسول محسوب گشت. ۲۶ 26
Kisha wakawapigia kura, nayo kura ikamwangukia Mathiya, naye akaongezwa kwenye wale mitume kumi na mmoja.

< کارهای رسولان 1 >