< کارهای رسولان 4 >

و چون ایشان با قوم سخن می‌گفتند، کهنه وسردار سپاه هیکل و صدوقیان بر سر ایشان تاختند، ۱ 1
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakisema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo wakawajia,
چونکه مضطرب بودند از اینکه ایشان قوم را تعلیم می‌دادند و در عیسی به قیامت ازمردگان اعلام می‌نمودند. ۲ 2
huku wakiwa wamekasirika sana kwa sababu mitume walikuwa wanawafundisha watu na kuhubiri kwamba kuna ufufuo wa wafu ndani ya Yesu.
پس دست بر ایشان انداخته، تا فردا محبوس نمودند زیرا که آن، وقت عصر بود. ۳ 3
Wakawakamata Petro na Yohana na kuwatia gerezani mpaka kesho yake kwa kuwa ilikuwa jioni.
اما بسیاری از آنانی که کلام را شنیدند ایمان آوردند و عدد ایشان قریب به پنج هزاررسید. ۴ 4
Lakini wengi waliosikia lile neno waliamini, idadi yao ilikuwa yapata wanaume 5,000.
بامدادان روسا و مشایخ و کاتبان ایشان دراورشلیم فراهم آمدند، ۵ 5
Kesho yake, viongozi wa Kiyahudi, wazee na walimu wa sheria wakakusanyika Yerusalemu.
با حنای رئیس کهنه وقیافا و یوحنا و اسکندر و همه کسانی که از قبیله رئیس کهنه بودند. ۶ 6
Walikuwepo kuhani mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda, na wengi wa jamaa ya kuhani mkuu.
و ایشان را در میان بداشتند واز ایشان پرسیدند که «شما به کدام قوت و به چه نام این کار را کرده‌اید؟» ۷ 7
Baada ya kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au kwa jina la nani mmefanya jambo hili?”
آنگاه پطرس ازروح‌القدس پر شده، بدیشان گفت: «ای روسای قوم و مشایخ اسرائیل، ۸ 8
Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akajibu, “Enyi watawala na wazee wa watu,
اگر امروز از ما بازپرس می‌شود درباره احسانی که بدین مرد ضعیف شده، یعنی به چه سبب او صحت یافته است، ۹ 9
kama leo tukihojiwa kwa habari ya mambo mema aliyotendewa yule kiwete na kuulizwa jinsi alivyoponywa,
جمیع شما و تمام قوم اسرائیل را معلوم باد که به نام عیسی مسیح ناصری که شما مصلوب کردید و خدا او را از مردگان برخیزانید، در او این کس به حضور شما تندرست ایستاده است. ۱۰ 10
ijulikane kwenu nyote na kwa watu wote wa Israeli kwamba: Ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa.
این است آن سنگی که شما معماران آن را رد کردید والحال سر زاویه شده است. ۱۱ 11
Huyu ndiye “‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’
و در هیچ‌کس غیراز او نجات نیست زیرا که اسمی دیگر زیر آسمان به مردم عطانشده که بدان باید ما نجات یابیم.» ۱۲ 12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
پس چون دلیری پطرس و یوحنا را دیدندو دانستند که مردم بی‌علم و امی هستند، تعجب کردند و ایشان را شناختند که از همراهان عیسی بودند. ۱۳ 13
Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kujua ya kuwa walikuwa watu wa kawaida, wasio na elimu, walishangaa sana, wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu.
و چون آن شخص را که شفا یافته بود باایشان ایستاده دیدند، نتوانستند به ضد ایشان چیزی گویند. ۱۴ 14
Lakini kwa kuwa walikuwa wanamwona yule kiwete aliyeponywa amesimama pale pamoja nao, hawakuweza kusema lolote kuwapinga.
پس حکم کردند که ایشان ازمجلس بیرون روند و با یکدیگر مشورت کرده، گفتند ۱۵ 15
Wakawaamuru watoke nje ya Baraza la Wayahudi wakati wakisemezana jambo hilo wao kwa wao.
که «با این دو شخص چه کنیم؟ زیرا که برجمیع سکنه اورشلیم واضح شد که معجزه‌ای آشکار از ایشان صادر گردید و نمی توانیم انکار کرد. ۱۶ 16
Wakaulizana, “Tuwafanyie nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu.
لیکن تا بیشتر در میان قوم شیوع نیابد، ایشان را سخت تهدید کنیم که دیگر با هیچ‌کس این اسم را به زبان نیاورند.» ۱۷ 17
Lakini ili kuzuia jambo hili lisiendelee kuenea zaidi kwa watu, ni lazima tuwaonye watu hawa ili wasiseme tena na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
پس ایشان راخواسته قدغن کردند که هرگز نام عیسی را بر زبان نیاورند و تعلیم ندهند. ۱۸ 18
Kisha wakawaita tena ndani na kuwaamuru wasiseme wala kufundisha kamwe kwa hili jina la Yesu.
اما پطرس و یوحنا درجواب ایشان گفتند: «اگر نزد خدا صواب است که اطاعت شما را بر اطاعت خدا ترجیح دهیم حکم کنید. ۱۹ 19
Lakini Petro na Yohana wakajibu, “Amueni ninyi wenyewe iwapo ni haki mbele za Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii Mungu.
زیرا که ما را امکان آن نیست که آنچه دیده و شنیده‌ایم، نگوییم.» ۲۰ 20
Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
و چون ایشان رازیاد تهدید نموده بودند، آزاد ساختند چونکه راهی نیافتند که ایشان را معذب سازند به‌سبب قوم زیرا همه به واسطه آن ماجرا خدا را تمجیدمی نمودند، ۲۱ 21
Baada ya vitisho vingi, wakawaacha waende zao. Hawakuona njia yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu ya watu, kwa kuwa watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetukia.
زیرا آن شخص که معجزه شفا دراو پدید گشت، بیشتر از چهل ساله بود. ۲۲ 22
Kwa kuwa umri wa yule mtu aliyekuwa ameponywa kwa muujiza ulikuwa zaidi ya miaka arobaini.
و چون رهایی یافتند، نزد رفقای خودرفتند و ایشان را از آنچه روسای کهنه و مشایخ بدیشان گفته بودند، مطلع ساختند. ۲۳ 23
Punde Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waumini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na viongozi wa makuhani na wazee.
چون این راشنیدند، آواز خود را به یکدل به خدا بلند کرده، گفتند: «خداوندا، تو آن خدا هستی که آسمان وزمین و دریا و آنچه در آنها است آفریدی، ۲۴ 24
Watu waliposikia hayo, wakainua sauti zao, wakamwomba Mungu kwa pamoja, wakisema, “Bwana Mwenyezi, uliyeziumba mbingu na nchi na bahari, na vitu vyote vilivyomo.
که بوسیله روح‌القدس به زبان پدر ما و بنده خودداود گفتی “چرا امت‌ها هنگامه می‌کنند و قومها به باطل می‌اندیشند؛ ۲۵ 25
Wewe ulisema kwa Roho Mtakatifu kupitia kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ukasema: “‘Mbona mataifa wanaghadhibika, na kabila za watu zinawaza ubatili?
سلاطین زمین برخاستند وحکام با هم مشورت کردند، برخلاف خداوند وبرخلاف مسیحش.” ۲۶ 26
Wafalme wa dunia wamejipanga, na watawala wanakusanyika pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.’
زیرا که فی الواقع بر بنده قدوس تو عیسی که او را مسح کردی، هیرودیس و پنطیوس پیلاطس با امت‌ها و قومهای اسرائیل با هم جمع شدند، ۲۷ 27
Ni kweli Herode na Pontio Pilato pamoja na watu wa Mataifa na Waisraeli, walikusanyika katika mji huu dhidi ya mwanao mtakatifu Yesu uliyemtia mafuta.
تا آنچه را که دست و رای تو از قبل مقدر فرموده بود، به‌جا آورند. ۲۸ 28
Wao wakafanya yale ambayo uweza wako na mapenzi yako yalikuwa yamekusudia yatokee tangu zamani.
و الان ای خداوند، به تهدیدات ایشان نظر کن و غلامان خود را عطا فرما تا به دلیری تمام به کلام تو سخن گویند، ۲۹ 29
Sasa, Bwana angalia vitisho vyao na utuwezeshe sisi watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri mkuu.
به دراز کردن دست خود، بجهت شفادادن و جاری کردن آیات و معجزات به نام بنده قدوس خود عیسی.» ۳۰ 30
Nyoosha mkono wako ili kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miujiza kwa jina la Mwanao mtakatifu Yesu.”
و چون ایشان دعا کرده بودند، مکانی که درآن جمع بودند به حرکت آمد و همه به روح‌القدس پر شده، کلام خدا را به دلیری می‌گفتند. ۳۱ 31
Walipokwisha kuomba, mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
و جمله مومنین را یک دل و یک جان بود، بحدی که هیچ‌کس چیزی از اموال خودرا از آن خود نمی دانست، بلکه همه‌چیز رامشترک می‌داشتند. ۳۲ 32
Wale walioamini wote walikuwa na moyo mmoja na nia moja. Wala hakuna hata mmoja aliyesema chochote alichokuwa nacho ni mali yake mwenyewe, lakini walishirikiana kila kitu walichokuwa nacho.
و رسولان به قوت عظیم به قیامت عیسی خداوند شهادت می‌دادند و فیضی عظیم برهمگی ایشان بود. ۳۳ 33
Mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa nguvu nyingi na neema ya Mungu ilikuwa juu yao wote.
زیرا هیچ‌کس از آن گروه محتاج نبود زیرا هر‌که صاحب زمین یا خانه بود، آنها را فروختند و قیمت مبیعات را آورده، ۳۴ 34
Wala hapakuwepo mtu yeyote miongoni mwao aliyekuwa mhitaji, kwa sababu mara kwa mara wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliviuza, wakaleta thamani ya vitu vilivyouzwa,
به قدمهای رسولان می‌نهادند و به هر یک بقدراحتیاجش تقسیم می‌نمودند. ۳۵ 35
wakaiweka miguuni pa mitume, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
و یوسف که رسولان او را برنابا یعنی ابن الوعظ لقب دادند، مردی از سبط لاوی و از طایفه قپرسی، ۳۶ 36
Yosefu, Mlawi kutoka Kipro, ambaye mitume walimwita Barnaba (maana yake Mwana wa Faraja),
زمینی را که داشت فروخته، قیمت آن را آورد و پیش قدمهای رسولان گذارد. ۳۷ 37
aliuza shamba alilokuwa nalo, akaleta hizo fedha alizopata na kuziweka miguuni pa mitume.

< کارهای رسولان 4 >