< دوم پادشاهان 1 >

عاصی شدند. ۱ 1
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
و اخزیا از پنجره بالاخانه خود که در سامره بود افتاده، بیمار شد. پس رسولان را روانه نموده، به ایشان گفت: «نزد بعل زبوب، خدای عقرون رفته، بپرسید که آیا از این مرض شفا خواهم یافت؟» ۲ 2
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
و فرشته خداوند به ایلیای تشبی گفت: «برخیز و به ملاقات رسولان پادشاه سامره برآمده، به ایشان بگو که آیا از این جهت که خدایی دراسرائیل نیست، شما برای سوال نمودن از بعل زبوب، خدای عقرون می‌روید؟ ۳ 3
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
پس خداوند چنین می‌گوید: ازبستری که بر آن برآمدی، فرود نخواهی شد بلکه البته خواهی مرد.» ۴ 4
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
و ایلیا رفت و رسولان نزد وی برگشتند و او به ایشان گفت: «چرا برگشتید؟» ۵ 5
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
ایشان در جواب وی گفتند: «شخصی به ملاقات ما برآمده، ما را گفت: بروید و نزد پادشاهی که شما را فرستاده است، مراجعت کرده، او راگویید: خداوند چنین می‌فرماید: آیا از این جهت که خدایی در اسرائیل نیست، تو برای سوال نمودن از بعل زبوب، خدای عقرون می‌فرستی؟ بنابراین از بستری که به آن برآمدی، فرود نخواهی شد بلکه البته خواهی مرد.» ۶ 6
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
او به ایشان گفت: «هیات شخصی که به ملاقات شما برآمد و این سخنان را به شما گفت چگونه بود؟» ۷ 7
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
ایشان او را جواب دادند: «مرد موی دار بود و کمربند چرمی بر کمرش بسته بود.» او گفت: «ایلیای تشبی است.» ۸ 8
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
آنگاه سردار پنجاهه را با پنجاه نفرش نزد وی فرستاد و او نزد وی آمد در حالتی که او بر قله کوه نشسته بود وبه وی عرض کرد که «ای مرد خدا، پادشاه می‌گوید به زیر آی؟» ۹ 9
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
ایلیا در جواب سردار پنجاهه گفت: «اگر من مرد خدا هستم، آتش از آسمان نازل شده، تو را و پنجاه نفرت را بسوزاند.» پس آتش از آسمان نازل شده، او را وپنجاه نفرش را بسوخت. ۱۰ 10
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
و باز سردار پنجاهه دیگر را با پنجاه نفرش نزد وی فرستاد و او وی را خطاب کرده، گفت: «ای مرد خدا، پادشاه چنین می‌فرماید که به زودی به زیر آی؟» ۱۱ 11
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
ایلیا در جواب ایشان گفت: «اگر من مرد خدا هستم آتش ازآسمان نازل شده، تو را و پنجاه نفرت را بسوزاند.» پس آتش خدا از آسمان نازل شده، او را و پنجاه نفرش رابسوخت. ۱۲ 12
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
پس سردار پنجاهه سوم را با پنجاه نفرش فرستاد و سردار پنجاهه سوم آمده، نزد ایلیا به زانو درآمد و از اوالتماس نموده، گفت که «ای مرد خدا، تمنا اینکه جان من و جان این پنجاه نفر بندگانت در نظر تو عزیز باشد. ۱۳ 13
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
اینک آتش از آسمان نازل شده، آن دو سردار پنجاهه اول را با پنجاهه های ایشان سوزانید، اما الان جان من در نظر تو عزیز باشد.» ۱۴ 14
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
و فرشته خداوند به ایلیا گفت: «همراه او به زیر آی و از او مترس.» پس برخاسته، همراه وی نزد پادشاه فرود شد. ۱۵ 15
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
و وی را گفت: «خداوند چنین می‌گوید: چونکه رسولان فرستادی تا از بعل زبوب، خدای عقرون سوال نماید، آیا از این سبب بود که در اسرائیل خدایی نبود که از کلام او سوال نمایی؟ بنابراین از بستری که به آن برآمدی، فرود نخواهی شد البته خواهی مرد.» ۱۶ 16
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
پس او موافق کلامی که خداوند به ایلیا گفته بود، مرد و یهورام در سال دوم یهورام بن یهوشافاط، پادشاه یهودا در جایش پادشاه شد، زیرا که او را پسری نبود. ۱۷ 17
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
و بقیه اعمال اخزیا که کرد، آیا در کتاب تواریخ ایام پادشاهان اسرائیل مکتوب نیست؟ ۱۸ 18
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< دوم پادشاهان 1 >