< دوم پادشاهان 19 >

و واقع شد که چون حزقیای پادشاه این را شنید، لباس خود را چاک زده، وپلاس پوشیده، به خانه خداوند داخل شد. ۱ 1
Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
والیاقیم، ناظر خانه و شبنه کاتب و مشایخ کهنه راملبس به پلاس نزد اشعیا ابن آموص نبی فرستاده، ۲ 2
Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
به وی گفتند: «حزقیا چنین می‌گوید که «امروزروز تنگی و تادیب و اهانت است زیرا که پسران به فم رحم رسیده‌اند و قوت زاییدن نیست. ۳ 3
Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
شاید یهوه خدایت تمامی سخنان ربشاقی را که آقایش، پادشاه آشور، او را برای اهانت نمودن خدای حی فرستاده است، بشنود و سخنانی را که یهوه، خدایت شنیده است، توبیخ نماید. پس برای بقیه‌ای که یافت می‌شوند، تضرع نما.» ۴ 4
Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
وبندگان حزقیای پادشاه نزد اشعیا آمدند. ۵ 5
Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
و اشعیابه ایشان گفت: «به آقای خود چنین گویید که خداوند چنین می‌فرماید: از سخنانی که شنیدی که بندگان پادشاه آشور به آنها به من کفرگفته‌اند، مترس. ۶ 6
Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
همانا روحی بر او می‌فرستم که خبری شنیده، به ولایت خود خواهد برگشت و اورا در ولایت خودش به شمشیر هلاک خواهم ساخت.» ۷ 7
Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
پس ربشاقی مراجعت کرده، پادشاه آشور را یافت که با لبنه جنگ می‌کرد، زیرا شنیده بود که ازلاکیش کوچ کرده است. ۸ 8
Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
و درباره ترهاقه، پادشاه حبش، خبری شنیده بود که به جهت مقاتله با توبیرون آمده است (پس چون شنید) بار دیگرایلچیان نزد حزقیا فرستاده، گفت: ۹ 9
Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
«به حزقیا، پادشاه یهودا چنین گویید: «خدای تو که به اوتوکل می‌نمایی، تو را فریب ندهد و نگوید که اورشلیم به‌دست پادشاه آشور تسلیم نخواهدشد. ۱۰ 10
“Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
اینک تو شنیده‌ای که پادشاهان آشور باهمه ولایتها چه کرده و چگونه آنها را بالکل هلاک ساخته‌اند، و آیا تو رهایی خواهی یافت؟ ۱۱ 11
Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
آیا خدایان امتهایی که پدران من، ایشان راهلاک ساختند، مثل جوزان و حاران و رصف وبنی عدن که در تلسار می‌باشند، ایشان را نجات دادند؟ ۱۲ 12
Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
پادشاه حمات کجاست؟ و پادشاه ارفاد و پادشاه شهر سفروایم و هینع و عوا؟» ۱۳ 13
Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
و حزقیا مکتوب را از دست ایلچیان گرفته، آن را خواند و حزقیا به خانه خداوند درآمده، آن را به حضور خداوند پهن کرد. ۱۴ 14
Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
و حزقیا نزدخداوند دعا نموده، گفت: «ای یهوه، خدای اسرائیل که بر کروبیان جلوس می‌نمایی، تویی که به تنهایی بر تمامی ممالک جهان خدا هستی و توآسمان و زمین را آفریده‌ای. ۱۵ 15
Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
‌ای خداوند گوش خود را فرا‌گرفته، بشنو. ای خداوند چشمان خودرا گشوده، ببین و سخنان سنحاریب را که به جهت اهانت نمودن خدای حی فرستاده است، استماع نما. ۱۶ 16
Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
‌ای خداوند، راست است که پادشاهان آشور امت‌ها و زمین ایشان را خراب کرده است، ۱۷ 17
“Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao.
و خدایان ایشان را به آتش انداخته، زیرا که خدا نبودند، بلکه ساخته دست انسان از چوب وسنگ. پس به این سبب آنها را تباه ساختند. ۱۸ 18
Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
پس حال یهوه، خدای ما، ما را از دست اورهایی ده تا جمیع ممالک جهان بدانند که تو تنهاای یهوه، خدا هستی.» ۱۹ 19
Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
پس اشعیا ابن آموص نزد حزقیا فرستاده، گفت: «یهوه، خدای اسرائیل، چنین می‌گوید: آنچه را که درباره سنحاریب، پادشاه آشور، نزدمن دعا نمودی اجابت کردم. ۲۰ 20
Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru.
کلامی که خداوند درباره‌اش گفته، این است: آن باکره، دختر صهیون، تو را حقیر شمرده، استهزا نموده است و دختر اورشلیم سر خود را به تو جنبانیده است. ۲۱ 21
Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
کیست که او را اهانت کرده، کفر گفته‌ای و کیست که بر وی آواز بلند کرده، چشمان خودرا به علیین افراشته‌ای؟ مگر قدوس اسرائیل نیست؟ ۲۲ 22
Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
به واسطه رسولانت، خداوند را اهانت کرده، گفته‌ای: به کثرت ارابه های خود بر بلندی کوهها و به اطراف لبنان برآمده‌ام و بلندترین سروهای آزادش و بهترین صنوبرهایش را قطع نموده، به بلندی اقصایش و به درختستان بوستانش داخل شده‌ام. ۲۳ 23
Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
و من، حفره کنده، آب غریب نوشیدم و به کف پای خود تمامی نهرهای مصر را خشک خواهم کرد. ۲۴ 24
Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.”
آیا نشنیده‌ای که من این را از زمان سلف کرده‌ام و از ایام قدیم صورت داده‌ام و الان، آن را به وقوع آورده‌ام تا توبه ظهور آمده و شهرهایی حصاردار را خراب نموده، به توده های ویران مبدل سازی؟ ۲۵ 25
“‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
از این جهت، ساکنان آنها کم قوت بوده، ترسان و خجل شدند، مثل علف صحرا و گیاه سبز و علف پشت بام و مثل غله‌ای که پیش از رسیدنش پژمرده شود، گردیدند. ۲۶ 26
Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
«اما من نشستن تو را و خروج و دخولت وخشمی را که بر من داری، می‌دانم. ۲۷ 27
“‘Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
چونکه خشمی که بر من داری و غرور تو، به گوش من برآمده است. بنابراین مهار خود را به بینی تو ولگام خود را به لبهایت گذاشته، تو را به راهی که آمده‌ای، برخواهم گردانید. ۲۸ 28
Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu, na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’
«و علامت، برای تو این خواهد بود که امسال غله خودرو خواهید خورد و سال دوم آنچه از آن بروید و در سال سوم بکارید و بدرویدو تاکستانها غرس نموده، میوه آنها را بخورید. ۲۹ 29
“Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
و بقیه‌ای که از خاندان یهودا رستگار شوند، باردیگر به پایین ریشه خواهند زد و به بالا میوه خواهند‌آورد. ۳۰ 30
Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
زیرا که بقیه‌ای از اورشلیم ورستگاران از کوه صهیون بیرون خواهند آمد. غیرت یهوه این را بجا خواهد آورد. ۳۱ 31
Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.
«بنابراین خداوند درباره پادشاه آشورچنین می‌گوید که «به این شهر داخل نخواهد شدو به اینجا تیر نخواهد انداخت و در مقابلش با سپرنخواهد آمد و منجنیق را در‌پیش آن بر نخواهدافراشت. ۳۲ 32
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kupanga majeshi kuuzingira.
به راهی که آمده است به همان برخواهد گشت و به این شهر داخل نخواهد شد. خداوند این را می‌گوید. ۳۳ 33
Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu, asema Bwana.
زیرا که این شهر راحمایت کرده، به‌خاطر خود و به‌خاطر بنده خویش داود، آن را نجات خواهم داد.» ۳۴ 34
Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”
پس فرشته خداوند در آن شب بیرون آمده، صد و هشتاد و پنج هزار نفر از اردوی آشور را زدو بامدادان چون برخاستند، اینک جمیع آنهالاشه های مرده بودند. ۳۵ 35
Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
و سنحاریب، پادشاه آشور کوچ کرده، روانه گردید و برگشته، درنینوی ساکن شد. ۳۶ 36
Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
و واقع شد که چون او درخانه خدای خویش، نسروک عبادت می‌کرد، پسرانش ادرملک و شرآصر او را به شمشیر زدند، و ایشان به زمین آرارات فرار کردند و پسرش آسرحدون به‌جایش سلطنت نمود. ۳۷ 37
Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.

< دوم پادشاهان 19 >