< دوم قرنتیان 3 >

آیا باز به سفارش خود شروع می‌کنیم؟ وآیا مثل بعضی احتیاج به سفارش نامه جات به شما یا از شما داشته باشیم؟ ۱ 1
Je, tunaanza tena kujisifu wenyewe? Au tunahitaji kupata barua za utambulisho kwenu au kutoka kwenu, kama watu wengine?
شما رساله ماهستید، نوشته شده در دلهای ما، معروف وخوانده شده جمیع آدمیان. ۲ 2
Ninyi wenyewe ndio barua yetu iliyoandikwa katika mioyo yetu, inayojulikana na kusomwa na kila mtu.
چونکه ظاهرشده‌اید که رساله مسیح می‌باشید، خدمت کرده شده از ما و نوشته شده نه به مرکب بلکه به روح خدای حی، نه بر الواح سنگ، بلکه بر الواح گوشتی دل. ۳ 3
Nanyi mwadhihirisha wazi kwamba ninyi ni barua itokayo kwa Kristo, matokeo ya huduma yetu, ambayo haikuandikwa kwa wino bali kwa Roho wa Mungu aliye hai, si katika vibao vya mawe, bali katika vibao ambavyo ni mioyo ya wanadamu.
اما بوسیله مسیح چنین اعتماد به خدا داریم. ۴ 4
Hili ndilo tumaini tulilo nalo mbele za Mungu kwa njia ya Kristo.
نه آنکه کافی باشیم که چیزی را به خود تفکر کنیم که گویا از ما باشد، بلکه کفایت مااز خداست. ۵ 5
Si kwamba sisi tunafikiri kuwa tunaweza kufanya jambo lolote wenyewe, lakini nguvu yetu inatoka kwa Mungu.
که او ما را هم کفایت داد تا عهدجدید را خادم شویم، نه حرف را بلکه روح رازیرا که حرف می‌کشد لیکن روح زنده می‌کند. ۶ 6
Ndiye alituwezesha sisi kuwa wahudumu wa Agano Jipya: si wa andiko, bali wa Roho; kwa kuwa andiko huua bali Roho hutia uzima.
اما اگر خدمت موت که در حرف بود و برسنگها تراشیده شده با جلال می‌بود، بحدی که بنی‌اسرائیل نمی توانستند صورت موسی را نظاره کنند به‌سبب جلال چهره او که فانی بود، ۷ 7
Basi ikiwa ile huduma iliyoleta mauti, iliyoandikwa kwa herufi juu ya jiwe ilikuja kwa utukufu, hata Waisraeli wakawa hawawezi kuutazama uso wa Mose kwa sababu ya ule utukufu wake ingawa ulikuwa ni wa kufifia,
چگونه خدمت روح بیشتر با جلال نخواهد بود؟ ۸ 8
je, huduma ya Roho haitakuwa na utukufu zaidi?
زیراهرگاه خدمت قصاص با جلال باشد، چند مرتبه زیادتر خدمت عدالت در جلال خواهد افزود. ۹ 9
Ikiwa huduma ile inayowahukumu wanadamu ina utukufu, je, ile huduma iletayo haki haitakuwa ya utukufu zaidi?
زیرا که آنچه جلال داده شده بود نیز بدین نسبت جلالی نداشت به‌سبب این جلال فایق. ۱۰ 10
Kwa maana kile kilichokuwa na utukufu sasa hakina utukufu ukilinganisha na huu utukufu unaozidi wa Agano Jipya.
زیرا اگر آن فانی با جلال بودی، هرآینه این باقی از طریق اولی در جلال خواهد بود. ۱۱ 11
Ikiwa kile kilichokuwa kinafifia kilikuja kwa utukufu, je, si zaidi utukufu wa kile kinachodumu?
پس چون چنین امید داریم، با کمال دلیری سخن می‌گوییم. ۱۲ 12
Kwa hiyo, kwa kuwa tunalo tumaini hili, tuna ujasiri sana.
و نه مانند موسی که نقابی برچهره خود کشید تا بنی‌اسرائیل، تمام شدن این فانی را نظر نکنند، ۱۳ 13
Sisi si kama Mose, ambaye ilimpasa kuweka utaji ili kufunika uso wake ili Waisraeli wasiuone ule mngʼao uliokuwa juu yake hadi ulipofifia na hatimaye kutoweka.
بلکه ذهن ایشان غلیظ شدزیرا که تا امروز همان نقاب در خواندن عهد عتیق باقی است و کشف نشده است، زیرا که فقط درمسیح باطل می‌گردد. ۱۴ 14
Lakini akili zao zilipumbazwa, kwa maana mpaka leo utaji ule ule hufunika wakati Agano la Kale linasomwa. Huo utaji haujaondolewa, kwa maana ni katika Kristo peke yake unaondolewa.
بلکه تا امروز وقتی که موسی را می‌خوانند، نقاب بر دل ایشان برقرارمی ماند. ۱۵ 15
Hata leo Sheria ya Mose inaposomwa, utaji hufunika mioyo yao.
لیکن هرگاه به سوی خداوند رجوع کند، نقاب برداشته می‌شود. ۱۶ 16
Lakini wakati wowote mtu anapomgeukia Bwana, utaji unaondolewa.
اما خداوند روح است و جایی که روح خداوند است، آنجا آزادی است. ۱۷ 17
Basi Bwana ndiye Roho. Mahali alipo Roho wa Bwana hapo pana uhuru.
لیکن همه ما چون با چهره بی‌نقاب جلال خداوند را در آینه می‌نگریم، از جلال تاجلال به همان صورت متبدل می‌شویم، چنانکه از خداوند که روح است. ۱۸ 18
Nasi sote, tukiwa na nyuso zisizotiwa utaji tunadhihirisha utukufu wa Bwana, kama kwenye kioo. Nasi tunabadilishwa ili tufanane naye, toka utukufu hadi utukufu mkuu zaidi, utokao kwa Bwana, ambaye ndiye Roho.

< دوم قرنتیان 3 >