< دوم قرنتیان 11 >

کاشکه مرا در اندک جهالتی متحمل شوید و متحمل من هم می‌باشید. ۱ 1
Laiti mngenivumilia kidogo katika upumbavu wangu! Naam, nivumilieni kidogo.
زیراکه من بر شما غیور هستم به غیرت الهی؛ زیرا که شما را به یک شوهر نامزد ساختم تا باکره‌ای عفیفه به مسیح سپارم. ۲ 2
Ninawaonea wivu, wivu wa Kimungu, kwa kuwa mimi niliwaposea mume mmoja, ili niwalete kwa Kristo kama mabikira safi.
لیکن می‌ترسم که چنانکه مار به مکر خود حوا را فریفت، همچنین خاطرشما هم از سادگی‌ای که در مسیح است، فاسدگردد. ۳ 3
Lakini nina hofu kuwa, kama vile Eva alivyodanganywa kwa ujanja wa yule nyoka, mawazo yenu yasije yakapotoshwa, mkauacha unyofu na usafi wa upendo wenu kwa Kristo.
زیرا هرگاه آنکه آمد، وعظ می‌کرد به عیسای دیگر، غیر از آنکه ما بدو موعظه کردیم، یا شما روحی دیگر را جز آنکه یافته بودید، یاانجیلی دیگر را سوای آنچه قبول کرده بودیدمی پذیرفتید، نیکو می‌کردید که متحمل می‌شدید. ۴ 4
Kwa sababu kama mtu akija na kuwahubiria Yesu mwingine ambaye si yule tuliyemhubiri, au kama mkipokea roho mwingine ambaye si yule mliyempokea, au Injili tofauti na ile mliyoikubali, ninyi mnaitii kwa urahisi.
زیرا مرا یقین است که از بزرگترین رسولان هرگز کمتر نیستم. ۵ 5
Lakini sidhani ya kuwa mimi ni dhalili sana kuliko hao “mitume wakuu.”
اما هرچند در کلام نیز امی باشم، لیکن در معرفت نی. بلکه در هر امری نزدهمه کس به شما آشکار گردیدیم. ۶ 6
Inawezekana mimi nikawa si mnenaji hodari, lakini ni hodari katika elimu. Jambo hili tumelifanya liwe dhahiri kwenu kwa njia zote.
آیا گناه کردم که خود را ذلیل ساختم تا شما سرافراز شوید دراینکه به انجیل خدا شما را مفت بشارت دادم؟ ۷ 7
Je, nilitenda dhambi kwa kujishusha ili kuwainua ninyi kwa kuwahubiria Injili ya Mungu pasipo malipo?
کلیساهای دیگر را غارت نموده، اجرت گرفتم تا شما را خدمت نمایم و چون به نزد شما حاضربوده، محتاج شدم، بر هیچ‌کس بار ننهادم. ۸ 8
Niliyanyangʼanya makanisa mengine kwa kupokea misaada kutoka kwao ili niweze kuwahudumia ninyi.
زیرابرادرانی که از مکادونیه آمدند، رفع حاجت مرانمودند و در هرچیز از بار نهادن بر شما خود رانگاه داشته و خواهم داشت. ۹ 9
Nami nilipokuwa pamoja nanyi, nikipungukiwa na chochote, sikuwa mzigo kwa mtu yeyote, kwa maana ndugu waliotoka Makedonia walinipatia mahitaji yangu. Kwa hiyo nilijizuia kuwa mzigo kwenu kwa njia yoyote, nami nitaendelea kujizuia.
به راستی مسیح که در من است قسم که این فخر در نواحی اخائیه از من گرفته نخواهد شد. ۱۰ 10
Kwa hakika kama vile kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, hakuna mtu yeyote katika Akaya nzima atakayenizuia kujivunia jambo hili.
از چه سبب؟ آیا ازاینکه شما را دوست نمی دارم؟ خدا می‌داند! ۱۱ 11
Kwa nini? Je, ni kwa sababu siwapendi? Mungu anajua ya kuwa nawapenda!
لیکن آنچه می‌کنم هم خواهم کرد تا از جویندگان فرصت، فرصت را منقطع سازم تا درآنچه فخر می‌کنند، مثل ما نیز یافت شوند. ۱۲ 12
Nami nitaendelea kufanya lile ninalofanya sasa ili nisiwape nafasi wale ambao wanatafuta nafasi ya kuhesabiwa kuwa sawa na sisi katika mambo wanayojisifia.
زیرا که چنین اشخاص رسولان کذبه و عمله مکار هستند که خویشتن را به رسولان مسیح مشابه می‌سازند. ۱۳ 13
Watu kama hao ni mitume wa uongo, ni wafanyakazi wadanganyifu, wanaojigeuza waonekane kama mitume wa Kristo.
و عجب نیست، چونکه خودشیطان هم خویشتن را به فرشته نور مشابه می‌سازد. ۱۴ 14
Wala hii si ajabu, kwa kuwa hata Shetani mwenyewe hujigeuza aonekane kama malaika wa nuru.
پس امر بزرگ نیست که خدام وی خویشتن را به خدام عدالت مشابه سازند که عاقبت ایشان برحسب اعمالشان خواهد بود. ۱۵ 15
Kwa hiyo basi si ajabu, kama watumishi wa Shetani nao hujigeuza ili waonekane kama watumishi wa haki. Mwisho wao utakuwa sawa na matendo yao yanavyostahili.
باز می‌گویم، کسی مرا بی‌فهم نداند والا مراچون بی‌فهمی بپذیرید تا من نیز اندکی افتخارکنم. ۱۶ 16
Nasema tena, mtu yeyote asidhani kwamba mimi ni mjinga. Lakini hata kama mkinidhania hivyo, basi nipokeeni kama mjinga ili nipate kujisifu kidogo.
آنچه می‌گویم از جانب خداوندنمی گویم، بلکه از راه بی‌فهمی در این اعتمادی که فخر ما است. ۱۷ 17
Ninayosema kuhusiana na huku kujisifu kwa kujiamini, sisemi kama vile ambavyo Bwana angesema, bali kama mjinga.
چونکه بسیاری از طریق جسمانی فخر می‌کنند، من هم فخر می‌نمایم. ۱۸ 18
Kwa kuwa wengi wanajisifu kama vile ulimwengu ufanyavyo, mimi nami nitajisifu.
زیرا چونکه خود فهیم هستید، بی‌فهمان را به خوشی متحمل می‌باشید. ۱۹ 19
Ninyi mwachukuliana na wajinga kwa sababu mna hekima sana!
زیرا متحمل می‌شوید هرگاه کسی شما را غلام سازد، یا کسی شما را فرو خورد، یا کسی شما را گرفتار کند، یاکسی خود را بلند سازد، یا کسی شما را بر رخسارطپانچه زند. ۲۰ 20
Kweli ni kwamba mnachukuliana na mtu akiwatia utumwani au akiwatumia kwa ajili ya kupata faida au akiwanyangʼanya au akijitukuza mwenyewe au akiwadanganya.
از روی استحقار می‌گویم که گویاما ضعیف بوده‌ایم. ۲۱ 21
Kwa aibu inanipasa niseme kwamba sisi tulikuwa dhaifu sana kwa jambo hilo! Lakini chochote ambacho mtu mwingine yeyote angethubutu kujisifia, nanena kama mjinga, nami nathubutu kujisifu juu ya hilo.
آیاعبرانی هستند؟ من نیز هستم! اسرائیلی هستند؟ من نیز هستم! از ذریت ابراهیم هستند؟ من نیزمی باشم! ۲۲ 22
Je, wao ni Waebrania? Mimi pia ni Mwebrania. Je, wao ni Waisraeli? Mimi pia ni Mwisraeli. Je, wao ni wazao wa Abrahamu? Mimi pia ni mzao wa Abrahamu.
آیا خدام مسیح هستند؟ چون دیوانه حرف می‌زنم، من بیشتر هستم! در محنتهاافزونتر، در تازیانه‌ها زیادتر، در زندانها بیشتر، در مرگها مکرر. ۲۳ 23
Je, wao ni watumishi wa Kristo? (Nanena kiwazimu.) Mimi ni zaidi yao. Nimefanya kazi kwa bidii kuwaliko wao, nimefungwa gerezani mara kwa mara, nimechapwa mijeledi sana, na nimekabiliwa na mauti mara nyingi.
از یهودیان پنج مرتبه از چهل یک کم تازیانه خوردم. ۲۴ 24
Mara tano nimechapwa na Wayahudi viboko arobaini kasoro kimoja.
سه مرتبه مرا چوب زدند؛ یک دفعه سنگسار شدم؛ سه کرت شکسته کشتی شدم؛ شبانه‌روزی در دریا بسر بردم؛ ۲۵ 25
Mara tatu nilichapwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nimevunjikiwa na meli, nimekaa kilindini usiku kucha na mchana kutwa,
درسفرها بارها؛ در خطرهای نهرها؛ در خطرهای دزدان؛ در خطرها از قوم خود و در خطرها ازامت‌ها؛ در خطرها در شهر؛ در خطرها دربیابان؛ در خطرها در دریا؛ در خطرها در میان برادران کذبه؛ ۲۶ 26
katika safari za mara kwa mara. Nimekabiliwa na hatari za kwenye mito, hatari za wanyangʼanyi, hatari kutoka kwa watu wangu mwenyewe, hatari kutoka kwa watu wa Mataifa; hatari mijini, hatari nyikani, hatari baharini; na hatari kutoka kwa ndugu wa uongo.
در محنت و مشقت، در بی‌خوابیها بارها؛ در گرسنگی و تشنگی، در روزه‌ها بارها؛ در سرماو عریانی. ۲۷ 27
Nimekuwa katika kazi ngumu na taabu, katika kukesha mara nyingi; ninajua kukaa njaa na kuona kiu; nimefunga kula chakula mara nyingi; nimehisi baridi na kuwa uchi.
بدون آنچه علاوه بر اینها است، آن باری که هر روزه بر من است، یعنی اندیشه برای همه کلیساها. ۲۸ 28
Zaidi ya hayo yote, nakabiliwa na mzigo wa wajibu wangu kwa makanisa yote.
کیست ضعیف که من ضعیف نمی شوم؟ که لغزش می‌خورد که من نمی سوزم؟ ۲۹ 29
Je, ni nani aliye mdhaifu, nami nisijisikie mdhaifu? Je, nani aliyekwazwa, nami nisiudhike?
اگر فخر می‌باید کرد از آنچه به ضعف من تعلق دارد، فخر می‌کنم. ۳۰ 30
Kama ni lazima nijisifu, basi nitajisifia yale mambo yanayoonyesha udhaifu wangu.
خدا و پدر عیسی مسیح خداوند که تا به ابد متبارک است، می‌داند که دروغ نمی گویم. (aiōn g165) ۳۱ 31
Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anahimidiwa milele, anajua ya kuwa mimi sisemi uongo. (aiōn g165)
در دمشق، والی حارث پادشاه، شهر دمشقیان را برای گرفتن من محافظت می‌نمود. ۳۲ 32
Huko Dameski, mtawala aliyekuwa chini ya Mfalme Areta aliulinda mji wa Dameski ili kunikamata.
و مرا از دریچه‌ای در زنبیلی از باره قلعه پایین کردند و از دستهای وی رستم. ۳۳ 33
Lakini nilishushwa kwa kapu kubwa kupitia katika dirisha ukutani, nikatoroka kutoka mikononi mwake.

< دوم قرنتیان 11 >