< 1 تیموتاوس 3 >

این سخن امین است که اگر کسی منصب اسقفی را بخواهد، کار نیکو می‌طلبد. ۱ 1
Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kazi ya uangalizi, atamani kazi nzuri.
پس اسقف باید بی‌ملامت و صاحب یک زن و هشیارو خردمند و صاحب نظام و مهمان‌نواز و راغب به تعلیم باشد؛ ۲ 2
Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,
نه میگسار یا زننده یا طماع سودقبیح بلکه حلیم و نه جنگجو و نه زرپرست. ۳ 3
asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.
مدبر اهل خانه خود، به نیکویی و فرزندان خویش را در کمال وقار مطیع گرداند، ۴ 4
Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.
زیراهرگاه کسی نداند که اهل خانه خود را تدبیر کند، چگونه کلیسای خدا را نگاهبانی می‌نماید؟ ۵ 5
(Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu?)
و نه جدیدالایمان که مبادا غرور کرده، به حکم ابلیس بیفتد. ۶ 6
Asiwe mtu aliyeokoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.
اما لازم است که نزد آنانی که خارجند هم نیک نام باشد که مبادا در رسوایی و دام ابلیس گرفتار شود. ۷ 7
Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.
همچنین شماسان باوقار باشند، نه دو زبان ونه راغب به شراب زیاده و نه طماع سود قبیح؛ ۸ 8
Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.
دارندگان سر ایمان در ضمیر پاک. ۹ 9
Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.
اما بایداول ایشان آزموده شوند و چون بی‌عیب یافت شدند، کار شماسی را بکنند. ۱۰ 10
Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.
و به همینطورزنان نیز باید باوقار باشند و نه غیبت‌گو بلکه هشیارو در هر امری امین. ۱۱ 11
Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.
و شماسان صاحب یک زن باشند و فرزندان و اهل خانه خویش را نیکو تدبیرنمایند، ۱۲ 12
Shemasi awe mume wa mke mmoja na inampasa aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.
زیرا آنانی که کار شماسی را نیکو کرده باشند، درجه خوب برای خویشتن تحصیل می‌کنند و جلادت کامل در ایمانی که به مسیح عیسی است. ۱۳ 13
Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Kristo Yesu.
این به تو می‌نویسم به امید آنکه به زودی نزد تو آیم. ۱۴ 14
Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili kwamba,
لیکن اگر تاخیر اندازم، تا بدانی که چگونه باید در خانه خدا رفتار کنی که کلیسای خدای حی و ستون و بنیاد راستی است. ۱۵ 15
kama nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo kanisa la Mungu aliye hai, lililo nguzo na msingi wa kweli.
وبالاجماع سر دینداری عظیم است که خدا درجسم ظاهر شد و در روح، تصدیق کرده شد و به فرشتگان، مشهود گردید و به امتها موعظه کرده ودر دنیا ایمان آورده و به جلال بالا برده شد. ۱۶ 16
Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.

< 1 تیموتاوس 3 >