< اول سموئیل 8 >

و واقع شد که چون سموئیل پیر شد، پسران خود را بر اسرائیل داوران ساخت. ۱ 1
Samweli alipokuwa mzee, akaweka wanawe kuwa waamuzi wa Israeli.
و نام پسر نخست زاده‌اش یوئیل بود و نام دومینش ابیاه؛ و در بئرشبع داور بودند. ۲ 2
Mzaliwa wa kwanza alikuwa Yoeli, na la wa pili lilikuwa Abiya, nao wakatumika huko Beer-Sheba.
اماپسرانش به راه او رفتار نمی نمودند بلکه در‌پی سود رفته، رشوه می‌گرفتند و داوری را منحرف می‌ساختند. ۳ 3
Lakini wanawe hawakuenenda katika njia zake. Waliziacha wakageukia faida za udanganyifu nao wakapokea rushwa na kupotosha haki.
پس جمیع مشایخ اسرائیل جمع شده، نزدسموئیل به رامه آمدند. ۴ 4
Basi wazee wote wa Israeli wakakusanyika pamoja na kumjia Samweli huko Rama.
و او را گفتند: «اینک توپیر شده‌ای و پسرانت به راه تو رفتار نمی نمایند، پس الان برای ما پادشاهی نصب نما تا مثل سایرامتها بر ما حکومت نماید.» ۵ 5
Wakamwambia, “Wewe umekuwa mzee, nao wanao hawaenendi katika njia zako, sasa tuteulie mfalme wa kutuongoza, kama ilivyo kwa mataifa mengine yote.”
و این امر در نظرسموئیل ناپسند آمد، چونکه گفتند: «ما راپادشاهی بده تا بر ما حکومت نماید.» و سموئیل نزد خداوند دعا کرد. ۶ 6
Lakini wao waliposema, “Tupe mfalme wa kutuongoza,” hili lilimchukiza Samweli, hivyo akamwomba Bwana.
و خداوند به سموئیل گفت: «آواز قوم را در هر‌چه به تو گفتند بشنو، زیرا که تو را ترک نکردند بلکه مرا ترک کردند تا برایشان پادشاهی ننمایم. ۷ 7
Naye Bwana akamwambia: “Sikiliza yale yote watu wanakuambia. Si wewe ambaye wamekukataa, bali wamenikataa mimi kuwa mfalme wao.
بر‌حسب همه اعمالی که از روزی که ایشان را از مصر بیرون آوردم، بجا آوردند و مرا ترک نموده، خدایان غیر را عبادت نمودند پس با تو نیز همچنین رفتار می‌نمایند. ۸ 8
Kama vile walivyofanya tangu siku nilipowapandisha kutoka Misri mpaka siku hii ya leo; wakiniacha mimi na kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokufanyia wewe.
پس الان آواز ایشان را بشنو لکن بر ایشان به تاکید شهادت بده، و ایشان را از رسم پادشاهی که بر ایشان حکومت خواهد نمود، مطلع ساز.» ۹ 9
Sasa wasikilize, lakini waonye kwa makini na uwafahamishe yale watakayotendewa na mfalme atakayewatawala.”
و سموئیل تمامی سخنان خداوند را به قوم که از او پادشاه خواسته بودند، بیان کرد. ۱۰ 10
Samweli akawaambia wale watu waliokuwa wakiomba wapewe mfalme maneno yote ya Bwana.
وگفت: «رسم پادشاهی که بر شما حکم خواهدنمود این است که پسران شما را گرفته، ایشان را برارابه‌ها و سواران خود خواهد گماشت و پیش ارابه هایش خواهند دوید. ۱۱ 11
Akasema, “Hivi ndivyo atakavyowatendea mfalme atakayewatawala. Atawachukua wana wenu na kuwafanya watumike kwa magari yake ya vita na farasi, nao watakimbia mbele ya magari yake.
و ایشان را سرداران هزاره و سرداران پنجاهه برای خودخواهدساخت، و بعضی را برای شیار کردن زمینش و درویدن محصولش و ساختن آلات جنگش و اسباب ارابه هایش تعیین خواهد نمود. ۱۲ 12
Baadhi yao atawaweka kuwa majemadari wa jeshi wa maelfu na majemadari wa jeshi wa hamsini, wengine kulima mashamba yake na kuvuna mavuno yake, pia na wengine kutengeneza silaha za vita na vifaa kwa ajili ya magari yake.
و دختران شما را برای عطرکشی و طباخی وخبازی خواهد گرفت. ۱۳ 13
Atawachukua binti zenu kuwa watengeneza manukato, wapishi na waokaji.
و بهترین مزرعه‌ها وتاکستانها و باغات زیتون شما را گرفته، به خادمان خود خواهد داد. ۱۴ 14
Atayachukua mashamba yenu yaliyo mazuri, mashamba ya mizabibu na mashamba yenu ya mizeituni na kuwapa watumishi wake.
و عشر زراعات وتاکستانهای شما را گرفته، به خواجه‌سرایان وخادمان خود خواهد داد. ۱۵ 15
Ataichukua sehemu ya kumi ya nafaka yenu na ya zabibu zenu na kuwapa maafisa wake na watumishi wake.
و غلامان و کنیزان ونیکوترین جوانان شما را و الاغهای شما را گرفته، برای کار خود خواهد گماشت. ۱۶ 16
Atawachukua watumishi wenu wa kiume na wa kike, na ngʼombe wenu walio wazuri sana na punda kwa matumizi yake mwenyewe.
و عشرگله های شما را خواهد گرفت و شما غلام اوخواهید بود. ۱۷ 17
Atachukua sehemu ya kumi ya makundi yenu ya kondoo na mbuzi, na ninyi wenyewe mtakuwa watumwa wake.
و در آن روز از دست پادشاه خودکه برای خویشتن برگزیده‌اید فریاد خواهید کرد وخداوند در آن روز شما را اجابت نخواهد نمود.» ۱۸ 18
Siku ile itakapowadia, mtalia kwa kutaka msaada kutokana na mfalme mliyemchagua, naye Bwana hatawajibu.”
اما قوم از شنیدن قول سموئیل ابا نمودند وگفتند: «نی بلکه می‌باید بر ما پادشاهی باشد. ۱۹ 19
Lakini watu wakakataa kumsikiliza Samweli wakasema, “Hapana! Tunataka mfalme wa kututawala.
تاما نیز مثل سایر امتها باشیم و پادشاه ما بر ماداوری کند، و پیش روی ما بیرون رفته، درجنگهای ما برای ما بجنگد.» ۲۰ 20
Kisha tutakuwa kama mataifa mengine yote, tukiwa na mfalme wa kutuongoza na kwenda mbele yetu na kutupigania vita vyetu.”
و سموئیل تمامی سخنان قوم را شنیده، آنها را به سمع خداوند رسانید. و خداوند به سموئیل گفت: «آواز ایشان را بشنو و پادشاهی بر ایشان نصب نما.» پس سموئیل به مردمان اسرائیل گفت: «شماهرکس به شهر خود بروید.» ۲۱ 21
Samweli aliposikia yote watu waliyosema, akarudia kuyasema mbele za Bwana.
۲۲ 22
Bwana akamjibu, “Wasikilize na uwape mfalme.” Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, “Kila mmoja arudi mjini kwake.”

< اول سموئیل 8 >