< Salomos Høisang 5 >

1 Jeg er kommet til min have, min søster, min brud! Jeg har plukket min myrra og min balsam, jeg har ett min honningkake og min honning, jeg har drukket min vin og min melk. Et, venner, og drikk! Drikk eder lystige, mine elskede!
Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
2 Jeg sover, men mitt hjerte våker; da lyder min elskedes røst - han banker på: Lukk op for mig, min søster, min venninne, min due, du rene! For mitt hode er fullt av dugg, mine lokker av nattens dråper.
Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
3 Jeg sa: Jeg har tatt av mig min kjortel, skulde jeg da ta den på igjen? Jeg har tvettet mine føtter, skulde jeg da skitne dem til?
Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
4 Min elskede rakte sin hånd inn gjennem luken; da blev mitt hjerte rørt for hans skyld.
Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
5 Jeg stod op for å lukke op for min elskede, og mine hender dryppet av myrra, mine fingrer av flytende myrra, som vætte låsens håndtak.
Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
6 Jeg lukket op for min elskede, men min elskede hadde vendt om og gått bort; min sjel var ute av sig selv over hans ord; jeg lette efter ham, men fant ham ikke; jeg ropte på ham, men han svarte mig ikke.
Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
7 Vekterne, som går omkring i byen, møtte mig, de slo mig, de såret mig; de tok mitt slør fra mig, vekterne på murene.
Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
8 Jeg ber eder inderlig, I Jerusalems døtre! Om I finner min elskede, hvad skal I si ham? - At jeg er syk av kjærlighet.
Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
9 Hvad er din elskede fremfor andre elskede, du fagreste blandt kvinner, hvad er din elskede fremfor andre elskede, siden du ber oss så inderlig?
Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
10 Min elskede er hvit og rød, utmerket fremfor ti tusen.
Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
11 Hans hode er som det fineste gull; hans lokker er kruset, sorte som ravnen.
Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
12 Hans øine er som duer ved rinnende bekker; de bader sig i melk, de hviler i sin ramme.
Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
13 Hans kinner er som velluktende blomstersenger, som det vokser krydderurter i; hans leber er som liljer, de drypper av flytende myrra.
Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
14 Hans hender er gullringer med innlagte krysolitter, hans midje er et kunstverk av elfenben, dekket med safirer.
Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
15 Hans ben er marmorstøtter, som står på fotstykker av fineste gull; hans skikkelse er som Libanon, herlig som sedrene.
Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
16 Hans gane er sødme, og alt ved ham er liflighet. Slik er min elskede, slik er min venn, I Jerusalems døtre!
Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.

< Salomos Høisang 5 >