< Salmenes 135 >

1 Halleluja! Lov Herrens navn, lov, I Herrens tjenere,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 I som står i Herrens hus, i forgårdene til vår Guds hus!
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Lov Herren! for Herren er god, lovsyng hans navn! for det er liflig.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 For Herren har utvalgt sig Jakob, Israel til sin eiendom.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Jeg vet at Herren er stor, og vår Herre større enn alle guder.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Herren gjør alt det han vil, i himmelen og på jorden, i havene og alle dyp,
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 han som lar regnskyer stige op fra jordens ende, gjør lyn til regn, fører vind ut av sine forrådshus,
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 han som slo de førstefødte i Egypten, både mennesker og fe.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 som sendte tegn og under midt i dig, Egypten, mot Farao og mot alle hans tjenere,
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 han som slo mange hedningefolk og drepte mektige konger,
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sihon, amorittenes konge, og Og, Basans konge, og alle Kana'ans kongeriker,
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 og gav deres land til arv, gav Israel, sitt folk, det til arv.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Herre, ditt navn blir til evig tid, Herre, ditt minne fra slekt til slekt.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 For Herren skal dømme sitt folk, og han skal miskunne sig over sine tjenere.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Hedningenes avguder er sølv og gull, et verk av menneskers hender.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 De har munn, men taler ikke; de har øine, men ser ikke;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 de har ører, men hører ikke, og det er ikke nogen ånde i deres munn.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Som de selv er, blir de som gjør dem, hver den som setter sin lit til dem.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Israels hus, lov Herren! Arons hus, lov Herren!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Levis hus, lov Herren! I som frykter Herren, lov Herren!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Lovet være Herren fra Sion, han som bor i Jerusalem! Halleluja!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salmenes 135 >