< Salmenes 113 >

1 Halleluja! Lov, I Herrens tjenere, lov Herrens navn!
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Herrens navn være lovet fra nu av og inntil evig tid!
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 Fra solens opgang til dens nedgang er Herrens navn høilovet.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 Herren er ophøiet over alle hedninger, hans ære er over himmelen.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Hvem er som Herren vår Gud, han som troner så høit,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 som ser så dypt ned, i himmelen og på jorden,
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 som reiser den ringe av støvet, ophøier den fattige av skarnet
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 for å sette ham hos fyrster, hos sitt folks fyrster,
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 han som lar den ufruktbare hustru bo som glad barnemor! Halleluja!
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Salmenes 113 >