< Josvas 4 >

1 Da nu hele folket var kommet vel over Jordan, sa Herren til Josva:
Wakati taifa lote lilipokwisha kuvuka Mto Yordani, Bwana akamwambia Yoshua,
2 Velg ut tolv menn av folket, én mann av hver stamme,
“Chagua watu kumi na wawili miongoni mwa watu, kila kabila mtu mmoja,
3 og byd dem og si: Ta op her fra Jordans bunn tolv stener, fra det sted hvor prestenes føtter står, og hold dem ferdige, og bær dem med eder over og legg dem ned på det sted hvor I blir denne natt over!
nawe uwaambie wachukue mawe kumi na mawili katikati ya Mto Yordani, palepale makuhani waliposimama, wayachukue na kuyaweka mahali mtakapokaa usiku huu wa leo.”
4 Da lot Josva de tolv menn kalle som han hadde valgt blandt Israels barn, én mann for hver stamme.
Basi Yoshua akawaita watu kumi na wawili ambao alikuwa amewachagua kutoka miongoni mwa Waisraeli, mtu mmoja kutoka kila kabila,
5 Og Josva sa til dem: Gå foran Herrens, eders Guds ark ut i Jordan og ta hver sin sten op på skulderen, efter tallet på Israels barns stammer!
naye akawaambia, “Mtangulie mbele ya Sanduku la Bwana Mungu wenu, mwende katikati ya Mto Yordani. Kila mmoja wenu atainua jiwe begani mwake, kufuatana na hesabu ya makabila ya Waisraeli,
6 Disse stener skal være et tegn blandt eder. Når eders barn i fremtiden spør: Hvad er dette for stener?
kuwa kama ishara katikati yenu. Siku zijazo, wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Ni nini maana ya mawe haya?’
7 da skal I si til dem: Jordans vann delte sig foran Herrens pakts-ark; da den drog ut i Jordan, delte Jordans vann sig, og disse stener skal være til et minne om dette for Israels barn til evig tid.
waambieni kwamba maji ya Mto Yordani yaliyokuwa yakitiririka yalitindika mbele ya Sanduku la Agano la Bwana. Wakati lilipovuka Yordani, maji ya Yordani yalitindika. Mawe haya yatakuwa kumbukumbu kwa watu wa Israeli milele.”
8 Israels barn gjorde som Josva bød, og tok tolv stener op av Jordan, således som Herren hadde sagt til Josva, efter tallet på Israels barns stammer, og de bar dem med sig over til det sted hvor de blev natten over, og la dem ned der.
Hivyo Waisraeli wakafanya kama Yoshua alivyowaagiza. Wakachukua mawe kumi na mawili kutoka katikati ya Mto Yordani, kulingana na hesabu ya kabila za Waisraeli kama Bwana alivyomwambia Yoshua, nao wakayabeba hadi kambini mwao, mahali walipoyatua chini.
9 Og ute i Jordan, på det sted hvor de prester som bar paktens ark, stod med sine føtter, reiste Josva tolv stener op, og de står der den dag idag.
Yoshua akayasimamisha yale mawe kumi na mawili ambayo yalikuwa katikati ya Mto Yordani, mahali pale ambapo miguu ya makuhani waliobeba Sanduku la Agano iliposimama. Nayo yako huko mpaka leo.
10 Prestene som bar paktens ark, blev stående ute i Jordan, til det var skjedd alt det som Herren hadde befalt Josva å si til folket, efter alt det som Moses hadde befalt Josva. Og folket skyndte sig og gikk over.
Makuhani waliobeba lile Sanduku walibakia wakiwa wamesimama katikati ya Mto Yordani mpaka kila kitu Bwana alichomwamuru Yoshua kilipokuwa kimefanywa na watu, sawasawa na vile Mose alivyokuwa amemwamuru Yoshua. Watu wakafanya haraka kuvuka,
11 Og da hele folket var kommet vel over, drog Herrens ark og prestene frem foran folket.
na mara tu watu wote walipokwisha kuvuka, Sanduku la Bwana na makuhani wakavuka watu wakiwa wanatazama.
12 Og Rubens barn og Gads barn og den halve Manasse stamme drog fullt rustet frem foran Israels barn, således som Moses hadde sagt til dem.
Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase wakavuka mbele ya Waisraeli, wakiwa wamevaa silaha, kama Mose alivyowaamuru.
13 Det var omkring firti tusen menn som væbnet til strid drog frem for Herrens åsyn til kamp på Jerikos ødemarker.
Kiasi cha watu 40,000 waliojiandaa kwa vita walivuka mbele za Bwana hadi nchi tambarare za Yeriko kwa ajili ya vita.
14 Den dag gjorde Herren Josva stor for hele Israels øine, og de fryktet ham, likesom de hadde fryktet Moses, alle hans livs dager.
Siku ile Bwana akamtukuza Yoshua mbele ya Israeli yote, nao wakamheshimu siku zote za maisha yake, kama vile walivyomheshimu Mose.
15 Og Herren sa til Josva:
Basi Bwana akamwambia Yoshua,
16 Byd prestene som bærer vidnesbyrdets ark, at de skal stige op av Jordan!
“Waamuru hao makuhani wanaolibeba Sanduku la Ushuhuda, wapande kutoka ndani ya Mto Yordani.”
17 Og Josva bød prestene og sa: Stig op av Jordan!
Kwa hiyo Yoshua akawaamuru hao makuhani akisema, “Pandeni kutoka ndani ya Mto Yordani.”
18 Da nu prestene som bar Herrens pakts-ark, steg op av Jordan og hadde satt sine føtter på det tørre land, da vendte Jordans vann tilbake til sitt leie og gikk som før over alle sine bredder.
Nao makuhani wakapanda kutoka ndani ya Mto Yordani wakilibeba hilo Sanduku la Agano la Bwana. Mara tu walipoiweka miguu yao penye kingo, nje ya mto, maji ya Yordani yakarudi kufurika kama ilivyokuwa kabla.
19 Det var den tiende dag i den første måned at folket steg op av Jordan, og de leiret sig ved Gilgal, lengst mot øst i landet omkring Jeriko.
Siku ya kumi ya mwezi wa kwanza watu walipanda kutoka Yordani na kupiga kambi huko Gilgali, kwenye mpaka wa mashariki ya Yeriko.
20 Og der i Gilgal reiste Josva op de tolv stener som de hadde tatt op av Jordan.
Naye Yoshua akayasimamisha huko Gilgali yale mawe kumi na mawili ambayo walikuwa wameyachukua katikati ya Mto Yordani.
21 Og han sa til Israels barn: Når eders barn i fremtiden spør sine fedre: Hvad er dette for stener?
Akawaambia Waisraeli, “Wazao wenu watakapowauliza baba zao siku zijazo wakisema, ‘Mawe haya maana yake ni nini?’
22 da skal I fortelle eders barn det og si: Israel gikk tørrskodd over Jordan her,
Basi waambieni, ‘Israeli ilivukia mahali pakavu katika Mto Yordani.’
23 fordi Herren eders Gud lot Jordans vann tørke bort foran eder til I kom over, likesom Herren eders Gud gjorde med det Røde Hav, som han lot tørke bort foran oss til vi kom over,
Kwa maana Bwana Mungu wenu alikausha maji ya Yordani mbele yenu, hadi mlipomaliza kuvuka. Bwana Mungu wenu alifanya haya kwa Mto Yordani sawasawa na kile alichoifanyia Bahari ya Shamu wakati alipoikausha mbele yetu hadi tulipomaliza kuvuka.
24 forat alle folk på jorden skal kjenne at Herrens hånd er sterk, og forat I alle dager skal frykte Herren eders Gud.
Alifanya hivi ili kwamba mataifa yote ya dunia yapate kujua kuwa mkono wa Bwana ni wenye nguvu, na ili kwamba kila wakati mpate kumcha Bwana Mungu wenu.”

< Josvas 4 >