< Esaias 15 >

1 Utsagn om Moab. Ja, i en natt blir Ar-Moab ødelagt, gjort til intet; ja, i en natt blir Kir-Moab ødelagt, gjort til intet.
Neno kuhusu Moabu: Ari iliyo Moabu imeangamizwa: imeharibiwa kwa usiku mmoja! Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, imeharibiwa kwa usiku mmoja!
2 De stiger op til huset og til Dibon på offerhaugene for å gråte; på Nebo og på Medeba skal Moab hyle; hvert hode er skallet, hvert skjegg avskåret.
Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, mpaka mahali pake pa juu ili walie, Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. Kila kichwa kimenyolewa na kila ndevu limeondolewa.
3 På dets gater binder de sekk om sig; på dets tak og på dets streder skal alle hyle og la sine tårer strømme.
Wamevaa nguo za magunia barabarani, juu ya mapaa na kwenye viwanja wote wanaomboleza, wamelala kifudifudi kwa kulia.
4 Hesbon og El'ale skriker så det høres like til Jahas; derfor klager Moabs krigsmenn, Moabs sjel skjelver.
Heshboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikika hadi Yahazi. Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, nayo mioyo yao imezimia.
5 Mitt hjerte klager over Moab, dets flyktninger kommer like til Soar, den treårige kvige; for de går gråtende opover bakken til Luhit, på veien til Horona'im løfter de klagerop over ødeleggelsen.
Moyo wangu unamlilia Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Soari, hadi Eglath-Shelishiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, wanakwenda huku wanalia; barabarani iendayo Horonaimu wanaombolezea maangamizi yao.
6 Nimrims vann blir til ørkener, gresset tørker bort, med urtene er det forbi, det finnes ikke mere et grønt strå.
Maji ya Nimrimu yamekauka na majani yamenyauka; mimea imekauka wala hakuna kitu chochote kibichi kilichobaki.
7 Derfor bærer de det som de har samlet sammen, sitt opsparte gods, over Vidjebekken.
Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.
8 Ja, klagerop lyder rundt omkring i Moabs land; like til Egla'im når dets hyl, og til Be'er-Elim;
Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, maombolezo yao hadi Beer-Elimu.
9 for Dimons vann er fulle av blod. Ja, jeg vil la ennu mere komme over Dimon - en løve skal falle over de undkomne av Moab, over levningen i landet.
Maji ya Dimoni yamejaa damu, lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: simba juu ya wakimbizi wa Moabu na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

< Esaias 15 >