< Daniel 5 >

1 Kong Belsasar gjorde et stort gjestebud for sine tusen stormenn, og han drakk vin for deres øine.
Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
2 Da vinen smakte Belsasar, bød han at de gull- og sølvkar som hans far Nebukadnesar hadde tatt bort fra templet i Jerusalem, skulde hentes, så kongen og hans stormenn, hans hustruer og hans medhustruer kunde drikke av dem.
Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
3 Så hentet de de gullkar som var tatt bort fra templet, fra Guds hus i Jerusalem; og kongen og hans stormenn, hans hustruer og hans medhustruer drakk av dem.
Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
4 De drakk vin og priste sine guder av gull og sølv, av kobber, jern, tre og sten.
Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
5 I samme stund kom det til syne fingrer av en menneskehånd, som skrev på den kalkede vegg i kongens palass, midt imot lysestaken. Og kongen så den hånd som skrev.
Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
6 Da skiftet kongen farve, og hans tanker forferdet ham; hans lenders ledemot slappedes, og hans knær slo mot hverandre.
Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
7 Og kongen ropte med høi røst at de skulde hente åndemanerne, kaldeerne og sannsigerne. Så tok han da til orde og sa til Babels vismenn: Den mann som leser denne skrift og kunngjør mig dens uttydning, han skal klæs i purpur og få en gullkjede om sin hals, og i makt skal han være den tredje i riket.
Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
8 Da alle kongens vismenn var kommet til stede, var de ikke i stand til å lese skriften og kunngjøre kongen dens uttydning.
Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
9 Da blev kong Belsasar storlig forferdet og skiftet farve, og hans stormenn blev aldeles forvirret.
Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
10 Ved kongens og hans stormenns ord kom dronningen inn i gjestebudssalen. Hun tok til orde og sa: Kongen leve evindelig! La ikke dine tanker forferde dig, og skift ikke farve!
Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
11 Det finnes i ditt rike en mann i hvem de hellige guders ånd er, og hos hvem det i din fars dager blev funnet oplysning og klokskap og en visdom som guders visdom; og kong Nebukadnesar, din far, gjorde ham til mester for tegnsutleggerne, åndemanerne, kaldeerne og sannsigerne. Således, konge, ophøiet din far ham,
Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
12 fordi det hos ham fantes en høi ånd og kunnskap og innsikt og evne til å tyde drømmer og løse gåter og utrede vanskelige spørsmål - jeg mener Daniel, han som kongen gav navnet Beltsasar. Send derfor bud efter Daniel! Så kunngjør han dig uttydningen.
Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
13 Så blev Daniel ført inn for kongen. Og kongen tok til orde og sa til Daniel: Er du Daniel, en av de jødiske fanger som kongen, min far, førte hit fra Juda?
Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
14 Jeg har hørt om dig at guders ånd er i dig, og at det hos dig er funnet oplysning og innsikt og høi visdom.
Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
15 Nu er vismennene og åndemanerne blitt ført inn for mig for å lese denne skrift og kunngjøre mig dens uttydning; men de er ikke i stand til å kunngjøre mig nogen uttydning av den.
Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
16 Men jeg har hørt om dig at du kan gi uttydninger og utrede vanskelige spørsmål; kan du nu lese denne skrift og kunngjøre mig dens uttydning, så skal du klæs i purpur og få en gullkjede om din hals, og i makt skal du være den tredje i riket.
Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
17 Da svarte Daniel og sa der han stod foran kongen: Dine gaver kan du selv ha, og dine foræringer kan du gi til en annen! Men skriften skal jeg lese for kongen og kunngjøre ham dens uttydning.
Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
18 Konge! Den høieste Gud gav Nebukadnesar, din far, riket og makten og æren og herligheten;
Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
19 og for den makts skyld han hadde gitt ham, bevet og fryktet alle folk, ætter og tungemål for ham; hvem han vilde, slo han ihjel, og hvem han vilde, lot han leve, og hvem han vilde, ophøiet han, og hvem han vilde, fornedret han.
Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
20 Men da hans hjerte ophøiet sig, og hans ånd blev stolt og overmodig, blev han nedstøtt fra sin kongetrone, og hans ære blev tatt fra ham.
Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
21 Han blev utstøtt fra menneskenes barn, og hans hjerte blev likt dyrenes, og hos villeslene var hans bolig; urter måtte han ete likesom oksene, og av himmelens dugg blev hans legeme vætet, inntil han sannet at den høieste Gud råder over kongedømmet blandt menneskene og setter den han vil, til å styre.
Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
22 Men du Belsasar, hans sønn, har ikke ydmyket ditt hjerte, enda du visste alt dette;
Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
23 du har ophøiet dig mot himmelens herre, og du har latt hente karene som var tatt fra hans hus, og du og dine stormenn, dine hustruer og dine medhustruer har drukket vin av dem, og du har prist dine guder av sølv og gull, av kobber, jern, tre og sten, som ikke ser og ikke hører og ikke har forstand; men den Gud i hvis hånd din livsånde er, og som råder over alle dine veier, har du ikke æret.
Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
24 Derfor blev nu denne hånd sendt fra ham, og denne skrift skrevet.
Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
25 Og dette er den skrift som er skrevet her: Mene, mene, tekel, ufarsin.
Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
26 Og så er uttydningen av dette ord: Mene: Tellet har Gud ditt kongedømmes dager og gjort ende på det.
Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
27 Tekel: Veid er du på vektskål og funnet for lett.
'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
28 Peres: Delt er ditt kongedømme og gitt til mederne og perserne.
'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
29 Da bød Belsasar at Daniel skulde klæs i purpur og en gullkjede legges om hans hals, og at det skulde utropes om ham at han i makt skulde være den tredje i riket.
Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
30 Samme natt blev kaldeerkongen Belsasar drept.
Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
31 Og mederen Darius mottok riket; han var da to og seksti år gammel.
na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.

< Daniel 5 >