< 1 Kongebok 15 >

1 I kong Jeroboams, Nebats sønns attende år blev Abiam konge over Juda.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Han regjerte tre år i Jerusalem. Hans mor hette Ma'aka; hun var datter til Abisalom.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Han vandret i alle de synder som hans far hadde gjort før ham, og hans hjerte var ikke helt med Herren hans Gud, som hans far Davids hjerte hadde vært;
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 men for Davids skyld lot Herren hans Gud en lampe brenne for ham i Jerusalem, idet han opreiste hans sønn efter ham og lot Jerusalem bli stående,
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 fordi David gjorde hvad rett var i Herrens øine, og i hele sitt liv ikke vek av fra noget av det han hadde befalt ham, undtagen det som hendte med hetitten Uria.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 Mellem Rehabeam og Jeroboam var det krig så lenge han levde.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 Hvad som ellers er å fortelle om Abiam og om alt det han gjorde, er opskrevet i Judas kongers krønike. Mellem Abiam og Jeroboam var det også krig.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 Og Abiam la sig til hvile hos sine fedre, og de begravde ham i Davids stad; og hans sønn Asa blev konge i hans sted.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 I Jeroboams, Israels konges tyvende år blev Asa konge over Juda.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 Han regjerte en og firti år i Jerusalem. Hans mor hette Ma'aka; hun var datter til Abisalom.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 Asa gjorde hvad rett var i Herrens øine, likesom hans far David hadde gjort.
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 Han drev tempel-bolerne ut av landet og fikk bort alle de motbydelige avguder som hans fedre hadde gjort.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Han avsatte endog sin mor Ma'aka fra hennes verdighet, fordi hun hadde gjort et gruelig avgudsbillede for Astarte; Asa hugg hennes gruelige avgudsbillede ned og brente det i Kidrons dal.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 Men offerhaugene blev ikke nedlagt; dog var Asas hjerte helt med Herren så lenge han levde.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 Han lot de ting hans far hadde helliget, og dem han selv hadde helliget, føre inn i Herrens hus, både sølv og gull og andre ting.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 Mellem Asa og Baesa, Israels konge, var det krig så lenge de levde.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Baesa, Israels konge, drog op mot Juda og bygget festningsverker i Rama for å hindre enhver fra å dra fra eller til Asa, Judas konge.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Da tok Asa alt det sølv og gull som var tilbake i skattkammerne i Herrens hus, og likeså skattene i kongens hus og overgav dem til sine tjenere; så sendte kong Asa dem til Benhadad, kongen i Syria, som bodde i Damaskus og var sønn til Tabrimmon, Hesjons sønn, med de ord:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 Mellem mig og dig er det jo et forbund, som det var mellem min far og din far. Her sender jeg dig en gave av sølv og gull; bryt nu ditt forbund med Baesa, Israels konge, så han må dra bort fra mig!
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 Benhadad lød kong Asa og sendte sine hærførere mot Israels byer og inntok Ijon og Dan og Abel-Bet-Ma'aka og hele Kinneret med hele Naftalis land.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Da Baesa hørte det, holdt han op med å bygge festningsverker i Rama og gav sig til i Tirsa.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Men kong Asa opbød hele Juda - ingen var fritatt - og de førte bort stenene og tømmeret som Baesa hadde brukt til festningsarbeidet i Rama; med det bygget kong Asa festningsverker i Geba i Benjamin og i Mispa.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 Hvad som ellers er å fortelle om Asa, om alle hans store gjerninger og alt det han gjorde, og om de byer han bygget, det er opskrevet i Judas kongers krønike. Men i sin alderdom fikk han en sykdom i føttene.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 Og Asa la sig til hvile hos sine fedre og blev begravet hos sine fedre i sin far Davids stad, og hans sønn Josafat blev konge i hans sted.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Nadab, Jeroboams sønn, blev konge over Israel i Asas, Judas konges annet år, og han regjerte over Israel i to år.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 Han gjorde hvad ondt var i Herrens øine, og vandret på sin fars vei og i hans synd, den som han hadde fått Israel til å gjøre.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 Men Baesa, Akias sønn, av Issakars hus, fikk i stand en sammensvergelse mot ham; og Baesa slo ham ihjel ved Gibbeton, som tilhørte filistrene, mens Nadab og hele Israel holdt Gibbeton kringsatt.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Baesa drepte ham i Asas, Judas konges tredje år og blev så konge i hans sted.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 Og da han var blitt konge, slo han hele Jeroboams hus ihjel; han lot ikke en levende sjel bli tilbake av Jeroboams hus, men utryddet det efter det ord som Herren hadde talt ved sin tjener Akia fra Silo;
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 dette skjedde for de synders skyld som Jeroboam hadde gjort, og som han hadde fått Israel til å gjøre, og fordi han hadde vakt Herrens, Israels Guds harme.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Hvad som ellers er å fortelle om Nadab og om alt det han gjorde, er opskrevet i Israels kongers krønike.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 Mellem Asa og Israels konge Baesa var det krig så lenge de levde.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 I Asas, Judas konges tredje år blev Baesa, Akias sønn, konge over hele Israel i Tirsa, og han var konge i fire og tyve år.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 Han gjorde hvad ondt var i Herrens øine, og vandret på Jeroboams vei og i hans synd, den som han hadde fått Israel til å gjøre.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Kongebok 15 >