< Luk 19 >

1 Jisu ah Jeriko hadaang ni wangta eno erah lam ih daankhoomta.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 Erah di phokhothoon sokse seete heh men ah Jakaias, changteng wah angta.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 Heh ih Jisu ah o angla ih jat suh taatwoot sokta, ang abah uh heh ah etho ang thoidi midung nawa ih Jisu ah tajap tupta.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 Erah thoidi miloong ngah ko ih soonkah ano Jisu daankhoom ah japtup suh puksak bangni duungta.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 Jisu ah erah rum adi thokkhoom haano, rangko ih toonsokta, eno Jakaias suh baatta, “Echaan ih dat raaho, Jakaias, tumeah chiinyah ngah an nok nah tong jaatjaat eh ang.”
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 Jakaias ah echaan ih dat kah no Jisu ah tenroon lam ih poon kaatta.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Miloong loongtang erah sok rum ano tuwaan rumta, “Arah mih ah rangdah mina nok ni wenwah ih hoon kala nih!”
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Jakaias toonchap ano Teesu asuh baatta, Chuupha! “Boichaat uh! Nga nyamka thotli ko ah changthih loong suh phe koh ang, erah damdoh ngah ih o mina dowa huda ih thaang phaksatang loong asuh lekbaji than ehan we ih boot korum ang.”
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Jisu ih heh suh baatta, “Khopiiroidong ah chiinyah arah nok adi thok hala, tumeah arah mih rah uh, Abraham sutoom satoom.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 Mina Sah ah emat ete loong jam suh nyia pangsuh ra taha.”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 Miloong ih erah banchaat rum adi, Jisu ih tiitthaak tiit wakbaat rumta. Heh ah erah di Jerusalem mong ni ejen thok eta, eno miloong ah ih Rangte Hasong ah thok nanah heh ang kola ih samthun rumta.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 Eno heh ih liita, “Teewadi men anaam pan mih wasiit deek hoh haloot nah luungwang ih hoon kah ano heh nok nah we ngaak wangsuh thunta.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 Eno heh maang dokkhoom ngakhoh ni, heh laksuh wah asih ah lompoon rum ano heh ih hun jaan ngun esiit esiit ih koh ano baat rumta, ‘Ngah moongkhoom angdoh sen ih arah ngun rah ih jaat phe kaat an.’
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 Amadi, heh mina loong ah ih heh ah miksuk et rumta, erah thoidi heh lilih ruurang baatte ah daapkaat rum ano jeng thuk rumta, ‘Arah mih ah seng ih seng luungwang et hoon suh tanookke.’
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 “Eno erah mih ah luungwang jen hoon kah ano we ngaakwangta. Erah damdam heh ih heh laksuh loong ah heh jiinni lompoon thukta, neng ih mathan than et dongniik rumta erah jat suh ah.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Phangkhothoon wah ah wangha no baatta, ‘Chuupha, an ih esiit kotahang dowa ih ngah ih hun lo asih boot niik tang,’
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 ‘Ese ih reetu,’ heh ih liita, ‘An ah wah se laksuh! An amasah di tuungmaang uno jen reetu bah, Ngah ih an samnuthung hah asih soksamte ih thiinha.’
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 Erah lilih laksuh wasiit ah wangha no liita, ‘Chuupha, An ih lo siit kotahang dowa ih hun jaan ngun lo banga boot niik tang.’
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 Erah wah asuh liita, ‘An ah hah banga soksamte ang uh!’
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 “Laksuh wasiit ah wangha no we baatta, “Chuupha, arah an hun jaan ngunsah rah ah; ngah ih nyulep ni thoopkhak angno huthiin tang.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 Ngah ih an ah mithih ih jat eh taha, eno cho etang. An ih andi lah angka ah kapte nyia an ih lakiiko dowa huite mina.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 Heh ih laksuh asuh liita, “Lajak, laksuh an ah! Ngah ih an jengjeng nawa dut haat hala! An ih jat et hu ngah mih chaan eah, ngah ih ngah di lah angka rah kakap ang nyia ngah ih lakiikang dowa kahui ang eah.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Ese ang ah, erah bah uh, an ih ngunnok ni taan lathiin wan mamet tu? Erah dobah ngunnok adoh hesut heboot taan ngah ngaakwang tokdoh eje ang thengta.”
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 “Eno heh ih erah di chaapte loong asuh baatta, ‘Hun ngunsah ah heh dowa esiit ah nge anno asih niikte laksuh asuh bootkoh an.’
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 Eno neng ih liita, ‘Chuupha, heh di hun ngunsah asih eje laangma ah!’
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 Heh ih ngaakbaat rumta, ‘Ngah ih amiisak tiit baat rumhala,’ ‘O di amasah jeela, erah suh ehaan et bootkoh ah, enoothong o di tajeeka, amasah taat angta rah uh ethoon nge et ah.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Amadoh, nga pi nga ra loong ah o ih ngah suh seng luungwang naktoom ang ah ih liite loong ah, adoh siitwan hanno nga pandoh tek haat an!’”
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 Jisu ih erah baat rum ano nengngah nengngah Jerusalem ko ih wangta.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 Neng Betpheej nyia Bethani reeni Olip kong ko ih thokrum adi, heliphante wanyi neng ngani daap wanta
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 amet baat ano ah: “Set ngah ni hadaang esiit je ah erah doh wang ansih; erah wang ansih doh, set ih moktosah bonthiincho tupwang ansih babah uh lathaak tumsiitka rah ah. Ja ansih no anah siitjah hansih.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 Mih ih tumet suh ja hansih, et cheng hansih bah, erah suh baat theng changte ih jamha eah.”
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 Eno nyi ah kah nyu ano Jisu ih baat nyuuta jun ih japtup nyuuta.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 Eno moktosah ah ja nyu adi changte wah ih cheng nyuuta, “Tumet suh ja hansih?”
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 Nyi ih ngaakbaat nyuuta, “Changte ih jamha,”
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 eno moktosah ah Jisu jiinni hoom wan nyuuta. Eno moktosah sakkhoh adi neng nyuh ah dekoh rum ano Jisu ah dung thuk rumta.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 Eno Jisu ah moktosah khoni wang damdam, miloong ih nengnyuh nengkhat loong ah lam adi ban dam wanrumta.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 Neng Jerusalem reeni thokrum ano, Olip Kong lamko dat kata adi, mih hantek heliphante loong ah erong rongwah ih Rangte rangphoong lam ih lakookmi ih liirumta epaatja theng reeraang loong japtup rumta asuh ah:
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 “Rangte mendi ra taha luungwang asuh Teesu ih romseetam koh ah!” Rangmong nah semroongroong ang ah eno Rangte aju phaak ah!”
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Eno mararah Pharisi ih midung nawa ih Jisu suh liita. “Chuupha,” neng ih liita, “An liphante loong ah nak toom cheekti rum ih baat uh!”
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 Jisu ih ngaakbaatta, “Ngah ih baat rumhala, nga liphante loong ah suusu taat ih tong rum abah uh, jong loong we toonriing rum ah.”
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 Heh samnuthung ko ih tiitkhoom ano, sokta eno heh mikse ah jan eta,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 eno liita, “Semroongroong ah mamah ang adoh se ih sen ih chiinyah taan ba lajattan! Enoothong amadoh ba sen ih takah tupkan!
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Senpi senra loong ih kooknak hanno sen lam ah wanrep nawa ih tangpa han rah saapoot ah thok eha.
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 Neng ih sen nyia sen noksong loong ah tek haat et han; jongteh tesiit taan uh erah nah tadakka, tumeah sen pangsuh Rangte ra taha saapoot ah tasamjattan!”
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 Eno Jisu ah Rangteenok nok ni wang ano thaangsangte loong ah dokphan wang rumta,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 neng suh amet liirumta, “Rangteele ni raang arah Rangte amet liita, ‘Nga Rangsoomnok ah rangsoom theng ang ah.’ Enoothong sen ih ehuh loong hottong theng et hoon han!”
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 Saarookwih Jisu ih Rangteenok ni nyootsoot rumta. Romwaphokhoh loong, Hootthe nyootte loong, nyia phokhoh mihak loong ih heh tek haat chung rumta,
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 enoothong neng ih heh tek haat lampo ah tajap jam rumta, tumeah miloong rah heh jeng ban boichaat ruh et rumta, tiitkhaap esiit taan laphut haat ih boichaat thung ang rumta.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luk 19 >