< Lioka 19 >

1 Ie tafazilike t’Iesoà le ho niranga Ieriko,
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 fe inge t’indaty atao Zakaiosy, bei’ o mpamory vili-lohao, toe mpañaleale,
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 nipay handrendreke Iesoà, fa aia te ho nimete amy lahialeñey, ie nibory.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 Aa le nihitrihitry mb’aolo ey re nanganike sakoañe hahaisake, ie hiary mb’eo.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 Aa naho nitandrifea’ Iesoà, le niandra naho niisa’e vaho nanoa’e ty hoe, O Zakaiosy, masikà! mizo­tsoa, fa tsi-mahay tsy hiantraño ama’o iraho te anito.
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 Nihavoa re, nizotso naho nampihovae’e añ’ anjomba’e ao an-kaehake.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Ie nahaisake, le niñeoñeoñe ty hoe i maroy: Nizilike ao re hiambahiny ami’ty ondaty beihakeo.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Fe niongake t’i Zakaiosy nanao ty hoe amy Talè: Intoa, Rañandria, hatoloko amo rarakeo ty an-tsasa’ o fanañakoo; aa naho eo t’ indaty nidramoteko le havahako in-empatse.
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Le hoe t’Iesoà tama’e: Anindroany te nizilik’ ami’ty anjomba toy ty famotsorañe, amy t’ie ka ro amori’ i Abraàme.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 Ty hi­tsoeke naho hañaha o rerekeo ty nivotraha’ i Ana’ondatiy atoy.
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 Ie nahajanjiñe izay iereo, le nitovoña’ Iesoà fandrazañañe amy te nitotoke Ierosaleme naho natao’ iereo te hatsatoke aniany i Fifehean’ Añaharey,
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 hoe re, Teo ty ana-donake nañavelo mb’ an-tane añe, handrambe fifeheañe, vaho himpoly.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 Aa le kinanji’e ty mpitoro’e folo, nitinolora’e tsanganolo folo vaho nanoa’e ty hoe, Manoa balike ampara’ ty fimpoliko.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 Ie amy zay, nalaiñe aze o boriza’eo vaho nampihitrife’ iereo ty hañorik’ aze mb’eo hanao ty hoe: Tsy no’ay itìañe te hifehe.
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 Aa ie tafampoly, naho fa ama’e i fifeheañey, le nampikanjie’e i mpitoroñe nitolora’e i volay rey hahafohiñe ty niazo’ iereo an-takinake.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Avy ty valoha’e nanao ty hoe: O Rañandria, fa nitovoñe tsanganolo folo i tsanganolo’oy.
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 Le hoe re tama’e: Fanjaka, ry mpitorom-bañoñeo, kanao nalili-po ami’ ty pini­nio’e irehe, mifeleha rova folo.
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 Avy ka ty faharoe nanao ty hoe: O Rañandria, nitovoñe tsanganolo lime i tsan­ga­nolo’o rey.
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 Le hoe re tama’e: Mamehea rova lime ka.
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 Pok’eo ka ty raike, nanao ty hoe: O Rañandria, intia i tsanganolo’oy fa nakafiko ami’ty masoara.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 Toe nañeveñako fa ondaty sarots’arofo: Mandrambe ty tsy nado’o, naho manifo ty tsy nitongise’o.
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 Aa hoe re ama’e: O vava’oo ty hizakako azo, ty mpitoroñe tembo tia, toe napota’o t’ie mpidiby, mandrambe ty tsy napoko, naho mitatake ty tsy nandrarahako;
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Aa vaho akore te tsy napo’o amy bankey i dralakoy, hangalako rekets’ ana’e amy fibalikoy?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 Le hoe re amo nijohañeo: Rambeso ama’e i tsanganoloy le atoloro amy aman-tsanganolo foloy.
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 (Aa hoe ty lie’ iareo: O Rañandria, ie amam-bogady folo!)
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 Itaroñako te mbe ho tolorañe ty manañe; fe hapontañ’ amy tsy manañey ndra ze ama’e.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Aa naho i rafelahiko nalaiñe ty hameheako rey, endeso mb’etoa, zamano añatrefako eo.
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 Ie fa nitsara, le niaolo am-pionjonañe mb’e Ierosaleme mb’eo.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 Aa naho nitotoke i Beit-Pagè naho i Betania ami’ty vohitse atao Oliva eo re, le nirahe’e ty mpiama’e roe
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 ami’ty hoe: Akia mb’ an-tanañe ey hoek’ey; ie mimoak’ ao, le hahaisake ty ana-borìke mirohy, mbe tsy niningira’ ondaty; idraito le endeso mb’atoa.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 Lehe eo ty mañontane ty hoe: Ino o añaha’ areo azeo? Le anò ty hoe ama’e: Ipaia’ i Talè.
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 Niongak’ amy zao i nampihitrifeñe rey vaho nizoe’ iereo hambañe amy sinaontsi’ey.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 Aa ie nañaha i ana-borìkey, le hoe o tompo’eo: Inoñe ty ampidraita’ areo o ana-borìkeo?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 Ipaia’ i Talè, hoe iereo.
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 Le nase­se’ iereo mb’ amy Iesoà mb’eo, naho nalama’ iereo amy ana-borìkey o lamba’ iareoo, vaho niningira’ Iesoà.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 Ie nañavelo le nandafike saroñe an-dalañe ey iereo.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 Aa naho nitotoke, toe fa am-pizo­tsoa’ i vohitse olivay, le fonga nirebeke o mpiama’e maroo, nandrenge an’ Andrianañahare, nipoña-peo ty amo hene raha tsitantane niisa’ iareoo
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 ami’ty hoe: Andriañeñe ty Mpanjaka ­mito­tsak’ ami’ty tahina’ Iehovà! Fierañerañañe abey ty andindìñe ao, vaho engeñe Andindimoneñe ey!
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Aa le hoe ty nanoa’ o Fariseo ila’e boak’ amy valobohòkeio: O Talè, endaho o mpiama’oo.
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 Fe hoe ty natoi’e: Itaroñako t’ie mianjiñe, le o vatoo ty hikoikoike.
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 Ie nañarine naho nahatalake i rovay, le niroveta’e,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 ami’ty hoe: Aa naho nahafohin-drehe, ndra androany, ty hampanintsiñe azo! f’ie mietak’ am-pihaino’o henaneo.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Fa hihavia’ ty andro hampitroara’ o rafelahi’oo fefe-tane hamalavala azo naho hiarikatok’ ama’o, vaho havoeboe’e mb’etia mb’atia.
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 Le hadasi’ iareo an-taneo, ihe naho o keleia’o ama’oo, le tsy hengàñe ama’o ty vato raike ambone’ ty ila’e, amy te tsy nirendre’o ty andro nitilihañ’ azo.
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 Ie nimoak’ an-Toe Masiñ’ ao le nata’e soike o mpanao balikeo naho o mpikaloo
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 nanoa’e ty hoe: Inay ty pinatetse: Anjombam-pitalahoañe ty anjombako toy, f’ie nanoe’ areo lakato fietaha’ ty malaso.
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 Ie nañoke boak’ andro añ’ Anjomban’ Añahare ao, le nikilily hañè-doza ama’e o mpisorom-beio naho o mpanoki-dilio vaho o roandriañeo;
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 f’ie tsy nahaoniñe ty hanoeñe, fa ama’e iaby ondatio nitsa­tsike o saontsi’eo.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Lioka 19 >