< Nechemijas 3 >

1 Un augstais priesteris Elijašibs cēlās ar saviem brāļiem, tiem priesteriem, un uztaisīja Avju vārtus; tie tos iesvētīja un iecēla viņu durvis; tos tie iesvētīja līdz Meas(Simtnieku) tornim, līdz Hananeēļa tornim.
Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani, wakajenga lango la kondoo. Walitakasa na kuweka milango yake. Waliweka wakfu hadi mnara wa Hamea na hadi mnara wa Hananeli.
2 Un viņiem sānis strādāja Jērikus vīri, un viņiem sānis strādāja Zakurs, Imra dēls.
Baada yao watu wa Yeriko walijenga, na baada yao Zakuri mwana wa Imri alijenga.
3 Un Zivju vārtus taisīja Senaās bērni; tie tos salaida un iecēla viņu durvis, viņu atslēgas un aizšaujamos.
Wana wa Senaa wakajenga lango la samaki. Wanaweka mihimili yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
4 Un viņiem sānis strādāja Meremots, Ūrijas dēls, Akoca dēla dēls. Un viņiem sānis strādāja Mešulams, Bereķijas dēls, Mešezabeēļa dēla dēls. Un viņiem sānis strādāja Cadoks, Baēnas dēls,
Meremoth aliandaa sehemu inayofuata. Yeye ni mwana wa Uria mwana wa Hakosi. Na baada yao Meshulamu akatengeneza. Yeye ni mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli. Karibu nao Sadoki akatengeneza. Yeye ni mwana wa Baana.
5 Un viņiem sānis strādāja Tekoieši, bet viņu cienīgie nepadeva savu kaklu, kalpot savam Kungam.
Baada yao Watekoi wakatengeneza, lakini viongozi wao walikataa kufanya kazi iliyoagizwa na wakuu wao.
6 Un Vecpilsētas vārtus taisīja Jojadus, Paseas dēls, un Mešulams, Besodijas dēls, tie tos salaida un iecēla viņu durvīs ar viņu atslēgām un viņu aizšaujamiem.
Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya, walitengeneza lango la Kale. Wanaweka mihimili, na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake.
7 Un viņiem sānis strādāja Gibeonietis Melatija un Meronietis Jadons, Gibeona un Micpas vīri (kas pieder) pie zemes valdnieka tiesas viņpus upes.
Nao, Melatia Mgibeoni, na Yadoni Meronothi, watu wa Gibeoni na Mispa, walifanyia matengenezo juu ya sehemu ambapo mkuu wa mkoa wa ng'ambo ya Mto aliishi.
8 Viņiem sānis strādāja Uziēls, Harhajas dēls, no tiem sudraba kalējiem. Viņiem sānis strādāja Hananija, zāļu pārdevēja dēls, un Jeruzālemi atkal uztaisīja līdz tam Platajam mūrim.
Na baada yake Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa wafua dhahabu, akatengeneza; na baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato. Wakajenga tena Yerusalemu mpaka Ukuta mpana.
9 Viņiem sānis strādāja Revaja, Ura dēls, Jeruzālemes pusapriņķa virsnieks.
Na baada yao Refaya mwana wa Huri akajenga. Alikuwa mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu.
10 Un viņiem sānis strādāja Jedaja, Arumava dēls, savam namam iepretim. Un viņam sānis strādāja Hatus, Azabenijas dēls.
Na baada yao Yedaya mwana wa Harumafu akajenga karibu na nyumba yake. Na baada yake Hatushi mwana wa Hashabneya akajenga.
11 Otru gabalu uztaisīja Malhija, Harima dēls, un Hašubs, PaātMoaba dēls, un arī to cepļa torni.
Malkiya mwana wa Harimu na Hashubu mwana wa Pahat Moabu, wajenga sehemu nyingine pamoja na mnara wa tanuu.
12 Un viņiem sānis strādāja Šalums, Āloēs dēls, Jeruzālemes pusapriņķa virsnieks, viņš un viņa meitas.
Baada yao Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akajenga, pamoja na binti zake.
13 Ielejas vārtus taisīja Hanuns un Zanoas iedzīvotāji; tie tos taisīja un iecēla viņu durvis, viņu atslēgas un viņu aizšaujamos, arī tūkstoš olektis mūra līdz Mēslu vārtiem.
Hanuni na wenyeji wa Zanoa walijenga lango la bondeni. Walijenga tena na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake. Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.
14 Un Mēslu vārtus taisīja Malhija, Rekaba dēls, vīna dārzu apgabala virsnieks; viņš tos uztaisīja, un iecēla viņu durvis, viņu atslēgas un viņu aizšaujamos.
Malkiya, mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-Hakeremu, akajenga lango la jaa. Alijenga na kuweka milango yake, na vyuma vyake na makomeo yake.
15 Un Akas vārtus taisīja Šalums, KalKosus dēls, Micpas apriņķa virsnieks; viņš tos uztaisīja un tos apsedza un iecēla viņu durvis, viņu atslēgas un viņu aizšaujamos, tā arī to mūri pie Šelahas dīķa, pie ķēniņa dārza, līdz tām pakāpēm, kas nonāk no Dāvida pilsētas.
Shalumu mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa, akajenga lango la Chemchemi. Alijenga, na kuweka kifuniko juu yake na kuweka milango yake na vyuma vyake na makomeo yake. Alijenga upya ukuta wa Pwani wa Silowamu kwa bustani ya mfalme, hadi ngazi ya kuongoza kutoka mji wa Daudi.
16 Aiz viņa taisīja Nehemija, Azbuka dēls, Betzura pusapriņķa virsnieks, līdz pret Dāvida kapam un līdz Azujas dīķim un līdz varoņu namam.
Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-suri, akajenga mahali hapo, toka maburini ya Daudi, mpaka birika lililojengwa na watu, na nyumba ya watu wenye nguvu.
17 Aiz viņa taisīja leviti, Rehums, Banus dēls. Viņam sānis strādāja Hašabija, Ķeģilas pusapriņķa virsnieks par savu apgabalu.
Baada yake, Walawi walijenga, pamoja na Rehumi mwana wa Bani na baada yake, Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, kwa wilaya yake.
18 Aiz viņa strādāja viņu brāļi, Bavajus, EnHadada dēls, Ķeģilas pusapriņķa virsnieks.
Baada yake watu wa nchi zao walijenga, ikiwa ni pamoja na Binui mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila.
19 Viņam sānis strādāja Ezers, Ješuūs dēls, Micpas virsnieks, otru gabalu, turpat pretī, kur uzkāpj pie bruņu nama pašā stūrī.
Baada yake alijenga Ezeri, mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alijenga sehemu nyingine kuelekea ghala ya silaha, kwenye kona ya ukuta.
20 Aiz viņa strādāja uzcītīgi Bāruks, Zebajus dēls, otru gabalu, no tā stūra līdz Elijašiba, augstā priestera, nama durvīm.
Baada yake Baruki, mwana wa Zakai, akajenga kwa hiari sehemu nyingine, toka kona ya ukuta mpaka mlango wa nyumba ya Eliashibu, kuhani mkuu.
21 Aiz viņa strādāja Merimots, Ūrijas dēls, Akoca dēla dēls, otru gabalu, no Elijašiba nama durvīm līdz Elijašiba nama galam.
Baada yake Meremothi, mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, akajenga sehemu nyingine, toka mlango wa nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
22 Un aiz viņa strādāja priesteri, tie vīri no (Jardānes) ielejas.
Kisha baada yake makuhani, watu wa eneo hilo karibu na Yerusalemu, walijenga.
23 Aiz tiem strādāja Benjamins un Hašubs savam namam iepretim. Aiz tiem strādāja Azarija, Maāsejas dēls, Ananijas dēla dēls, pie sava nama.
Baada yao Benyamini na Hashubu walijenga kuielekea nyumba yao. Baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania, alijenga karibu na nyumba yake.
24 Aiz viņa strādāja Binuūs, EnHadada dēls, otru gabalu, no Azarijas nama līdz kaktam un līdz stūrim,
Baada yake Binui mwana wa Henadadi akajenga sehemu nyingine, kutoka nyumba ya Azaria hadi kona ya ukuta.
25 Palals, Uzijus dēls, stūrim iepretim un tam augstam tornim iepretim, kas no augšēja ķēniņa nama izceļas un stāv pie cietuma pagalma. Aiz viņa Pedaja, Pareūs dēls.
Palali, mwana wa Uzai, akajenga juu ya kona ya ukuta na mnara unaoenea juu kutoka nyumba ya juu ya mfalme katika uwanda wa walinzi. Baada yake Pedaya mwana wa Paroshi akajenga.
26 Bet Dieva nama kalpotāji dzīvoja Ofelā līdz Ūdens vārtiem pret rīta pusi un pret to torni, kas tur izceļas.
Sasa watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli walijenga mpaka upande wa Hifadhi ya Maji upande wa mashariki wa mnara unaojitokeza.
27 Aiz tiem strādāja Tekoieši otru gabalu, tam lielam tornim iepretim, kas tur izceļas, un līdz Ofela mūrim.
Baada yake, Watekoi walijenga sehemu nyingine, kuelekea mnara mkubwa ulio nje, mpaka ukuta wa Ofeli.
28 Augšpus Zirgu vārtiem strādāja priesteri, ikviens savam namam iepretim.
Makuhani wakajenga juu ya lango la farasi, kila mmoja kuelekea nyumba yake.
29 Aiz tiem strādāja Cadoks, Imera dēls, savam namam iepretim. Un aiz viņa Šemaja, Šehanijas dēls, Rīta vārtu sargs.
Baada yao Sadoki, mwana wa Imeri, alijenga sehemu hiyo kuelekea nyumba yake. Na baada yake Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki, akajenga.
30 Aiz viņa strādāja Hananija, Šelemijas dēls, un Hanuns, Calafa sestais dēls, otru gabalu. Aiz viņiem strādāja Mešulams, Bereķijas, dēls, savam kambarim iepretim.
Baada yake Hanania, mwana wa Shelemia, na Hanuni, mwana wa sita wa Salafu, wakajenga sehemu nyingine. Meshulamu mwana wa Berekia akajenga kuelekea kwenye vyumba vyake.
31 Aiz viņa strādāja Malkija, sudraba kalēja dēls, līdz Dievu nama kalpotāju un zāļu pārdevēju namam, Tiesas vārtiem iepretim, līdz stūra uzkāpēm.
Baada yake Malkiya, mmoja wa wafua dhahabu, akajenga mpaka nyumba ya watumishi wa hekalu na wafanyabiashara waliokuwa wakielekea lango la gereza na mpaka chumba cha juu cha pembeni.
32 Un starp stūra uzkāpēm un Avju vārtiem strādāja sudraba kalēji un zāļu pārdevēji.
Wafanyabiashara wa dhahabu na wafanyabiashara walijenga kati ya chumba cha juu cha kona na Lango la Kondoo.

< Nechemijas 3 >