< Psalmorum 63 >

1 psalmus David cum esset in deserto Iudaeae Deus Deus meus ad te de luce vigilo sitivit in te anima mea quam multipliciter tibi caro mea
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 in terra deserta et invia et inaquosa sic in sancto apparui tibi ut viderem virtutem tuam et gloriam tuam
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 quoniam melior est misericordia tua super vitas labia mea laudabunt te
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 sic benedicam te in vita mea in nomine tuo levabo manus meas
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 sicut adipe et pinguidine repleatur anima mea et labia exultationis laudabit os meum
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 si memor fui tui super stratum meum in matutinis meditabar in te
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 quia fuisti adiutor meus et in velamento alarum tuarum exultabo
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 adhesit anima mea post te me suscepit dextera tua
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 ipsi vero in vanum quaesierunt animam meam introibunt in inferiora terrae
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 tradentur in manus gladii partes vulpium erunt
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 rex vero laetabitur in Deo laudabitur omnis qui iurat in eo quia obstructum est os loquentium iniqua
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalmorum 63 >