< Psalmorum 57 >

1 in finem ne disperdas David in tituli inscriptione cum fugeret a facie Saul in spelunca miserere mei Deus miserere mei quoniam in te confidit anima mea et in umbra alarum tuarum sperabo donec transeat iniquitas
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 clamabo ad Deum altissimum Deum qui benefecit mihi
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 misit de caelo et liberavit me dedit in obprobrium conculcantes me diapsalma misit Deus misericordiam suam et veritatem suam
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 et eripuit animam meam de medio catulorum leonum dormivi conturbatus filii hominum dentes eorum arma et sagittae et lingua eorum gladius acutus
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 exaltare super caelos Deus et in omnem terram gloria tua
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 laqueum paraverunt pedibus meis et incurvaverunt animam meam foderunt ante faciem meam foveam et inciderunt in eam diapsalma
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 paratum cor meum Deus paratum cor meum cantabo et psalmum dicam
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 exsurge gloria mea exsurge psalterium et cithara exsurgam diluculo
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 confitebor tibi in populis Domine psalmum dicam tibi in gentibus
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 quoniam magnificata est usque ad caelos misericordia tua et usque ad nubes veritas tua
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 exaltare super caelos Deus et super omnem terram gloria tua
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psalmorum 57 >