< Psalmorum 3 >

1 psalmus David cum fugeret a facie Abessalon filii sui Domine quid multiplicati sunt qui tribulant me multi insurgunt adversum me
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 multi dicunt animae meae non est salus ipsi in Deo eius diapsalma
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 tu autem Domine susceptor meus es gloria mea et exaltans caput meum
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 voce mea ad Dominum clamavi et exaudivit me de monte sancto suo diapsalma
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 ego dormivi et soporatus sum exsurrexi quia Dominus suscipiet me
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 non timebo milia populi circumdantis me exsurge Domine salvum me fac Deus meus
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 quoniam tu percussisti omnes adversantes mihi sine causa dentes peccatorum contrivisti
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Domini est salus et super populum tuum benedictio tua
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.

< Psalmorum 3 >