< Psalmorum 17 >

1 oratio David exaudi Domine iustitiam meam intende deprecationem meam auribus percipe orationem meam non in labiis dolosis
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 de vultu tuo iudicium meum prodeat oculi tui videant aequitates
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 probasti cor meum visitasti nocte igne me examinasti et non est inventa in me iniquitas
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 ut non loquatur os meum opera hominum propter verba labiorum tuorum ego custodivi vias duras
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 perfice gressus meos in semitis tuis ut non moveantur vestigia mea
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 ego clamavi quoniam exaudisti me Deus inclina aurem tuam mihi et exaudi verba mea
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 mirifica misericordias tuas qui salvos facis sperantes in te
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 a resistentibus dexterae tuae custodi me ut pupillam oculi sub umbra alarum tuarum proteges me
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 a facie impiorum qui me adflixerunt inimici mei animam meam circumdederunt super me;
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 adipem suum concluserunt os eorum locutum est superbia
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 proicientes me nunc circumdederunt me oculos suos statuerunt declinare in terram
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 susceperunt me sicut leo paratus ad praedam et sicut catulus leonis habitans in abditis
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 exsurge Domine praeveni eum et subplanta eum eripe animam meam ab impio frameam tuam
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 ab inimicis manus tuae Domine a paucis de terra divide eos in vita eorum de absconditis tuis adimpletus est venter eorum saturati sunt filiis et dimiserunt reliquias suas parvulis suis
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 ego autem in iustitia apparebo conspectui tuo satiabor cum apparuerit gloria tua
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Psalmorum 17 >